Makapuku Forum

Makapuku Forum

MBIO ZA UFUNGAJI NBC PL 2022|23

Orodha ya wachezaji wanaowania kiatu cha ufungaji bora Ligi Kuu 2022|23, mechi zinazidi kupungua Mayele anazidi kutengeneza gap kati yake na washindani wake. Je, kuna wa kumzua Mayela msimu huu kushinda GOLDEN BOOT?

Fiston Mayele [Yanga] 15
Moses Phiri [Simba] 10
John Bocco [Simba] 9
Said Ntibazonkiza [Simba] 9
Bruno Gomes [Singida BS] 8
Sixtus Sabilo [Mbeya City] 8
Idris Mbombo [Azam FC] 7
Screenshot_20230128_052841_OGInsta%2B.jpg
 
Shaffih Dauda

Wakati nikiwa Belgium nilikutana na CEO wa klabu ya K. Beerschot V.A Mr. Frederic Van den Steen, katika mazungumzo yetu kuhusu soko la wachezaji wa Afrika barani Ulaya aliniambia siku hizi hawaangaalii kipaji peke yake kuna vitu vingi wanazingatia ikiwa ni pamoja na aina ya uchezaji wa mchezaji husika na aina ya uchezaji wa timu yao.

Aliniambia siku hizi mambo yamebadilika sana, hatuendi tena Afrika kutafuta mchezaji mwenye kipaji tu! Bali tunaenda kutafuta mchezaji mwenye aina fulani ya uchezaji kulingana na aina ya uchezaji na mahitaji ya timu.

Kwa mfano timu inahitaji mshambuliaji, kipaumbele sio rekodi yake nzuri ya magoli aliyowahi kufunga huko nyuma au katoa assist ngapi kwenye msimu.

Wao wanataka mchezaji ambaye anapiga kazi kweli, timu yao inacheza high-line pressing, kwa hiyo wanahitaji aina ya mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa wa kufanya pressing kuanzia juu.

Wanajua hawezi kufaya pressing kwa dakika zote 90 lakini angalau aweze kufanya hivyo kwa dakika 55 hadi 60. Muda wote huo aweze kukimbia kati ya dakika 90.

Kwa hiyo wao wanahitaji mshambuliaji kulinagana na work-rate yake uwanjani sio kafunga magoli mangapi. Wakipata mchezaji wa aina hiyo wanamchukua kwa sababu atawasaidia, wakati anafanya pressing wachezaji wengine wanatengeneza nafasi za kufunga wakitokea nyuma bila ya kuwa na presha.
Screenshot_20230128_053120_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom