Farhan Jr
Nimeona dhihaka nyingi kuhusu usajili wa Gael Bigirimana, lakini kwa heshima ya mpira wa miguu ni kuwa Mchezaji husajiliwa kwa vitu viwili Form (Kiwango) na Class (Daraja).
Mfano Hakim Ziyech hana kiwango kizuri Chelsea lakini Milan wanamtaka sana kwakuwa wanafahamu daraja lake, mfano Erikssen alipotoka kwenye shambulio la moyo Brentford na timu nyingi zilimtaka kwakuwa wanafahamu Daraja lake.
Leo hii Ismail Sawadogo hajacheza miezi zaidi ya miwili ila Simba wamemsajili simply ni Daraja lake wote tunalifahamu au profile yake inavutia! Hata Feisal asipocheza mwaka mzima ila akirejea kila timu itamtaka simply ni Daraja lake.
Yanga walimsaini Gael Bigirimana ambaye amewahi kucheza EPL lakini hajaclick kwenye mpira wetu, sio dhambi! Kama ambavyo waliwahi kumsaini Saido aliyewahi kucheza LIGUE 1 na ikawalipa, huku Azam walimsaini Ahmada wa Ligue1 ambaye haikuwalipa.
Sio kosa Gael kusajiliwa na sioni dhambi Yanga kumwacha kwakuwa hajakidhi mahitaji na sio kosa wao kumpa sifa zake wakati wanamsaini kwakuwa profile yake ilikuwa nzuri na inavutia sana, the same case hata kwa Dejan alipokuja Simba.
Sometimes mpira wa miguu huenda beyond na mpira hiyo ni kawaida, wakati mwingine ni biashara ya kuisukuma brand yako mbali zaidi, unakumbuka usajili wa Sheva pale Chelsea na ukaribu wake na Roman? Real Madrid kuna kipindi walikuwa na mpango maalum na visiwa vya Mallorca ili kuipenyeza brand zaidi kwakuwa hawakuwa wanakubalika zaidi.
Sajili ya Gael haijawalipa uwanjani which ni kawaida lakini nje ya uwanja imewalipa na inakuwa rahisi kwa klabu kuwa na ushawishi wa kuwahi kuwa na profile kama za Saido na Gael ndani ya timu zao, ni ngumu kuona kikawaida kama tunaishi kawaida.
Perez aliwahi kusema atamsajili Luis Figo kama zawadi endapo Madridistas watamchagua ni kawaida! Hujui kwanini Boss Todd Boehly alienda fasta dili la Mudryk na wakamruhusu aingie na bendera ya Ukraine pale Stamford Bridge?

One thing about football is not about football!
Sometimes it pays, sometimes it doesnt ndio football!