Makapuku Forum

Makapuku Forum

Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara limebaini mbinu mpya wanazotumia Wahalifu kusafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi Wilayani Babati Mkoani Manyara.

RPC wa Manyara George Katabazi amesema January 16 mwaka huu Mwanaume mmoja alikamatwa akiwa na bunda 20 za mirungi sawa na Kilo 10 akiwa amezifunga kifuani na tumboni kwa huku Mtuhumiwa mwingine wa Kike alikamatwa akiwa na bunda 25 sawa na Kilo 12 za dawa hizo za kulevya (Mirungi) akiwa amezifunga mapajani.

Katika hatua nyingine Polisi Mkoa wa Manyara kwa kushirikiana na Mahakama ya Mwanzo Wilaya ya Simanjiro imemuhukumu Lalahe Karoli kifungo cha miaka 30 kwenda Jela kwa kosa la Kumbaka Mwanafunzi wa darasa la saba.

RPC Katabazi amewaomba Wananchi wa Mkoa wa Manyara kuendelea kufichua uhalifu na wahalifu pamoja na kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi .
Screenshot_20230122_051445_OGInsta%2B.jpg
 
Imeelezwa kuwa uwezo wa mitambo ya kuzalisha umeme iliyoungwa katika mfumo wa Gridi ya Taifa umeongezeka na kufikia megawati 1,777.05 mwezi Desemba 2022 sawa na ongezeko la asilimia 4.87, ikilinganishwa na megawati 1,694.55 zilizokuwepo hadi kufikia mwezi Septemba 2022.

Aidha, katika kipindi cha mwezi Julai hadi Desemba 2022 jumla ya futi za ujazo milioni 38,172 za Gesi Asilia zilizalishwa katika vitalu vya Songosongo na Mnazi Bay ambapo uzalishaji wa Gesi asilia umeongezeka kwa asilimia 27 ikilinganishwa na kipindi Julai-Desemba, mwaka 2021 ambapo futi za ujazo 29,996 zilizalishwa.

Hayo yameelezwa Jijini Dodoma wakati Wizara ya Nishati ikiongozwa na Waziri wa Nishati, January Makamba ilipowasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati Taarifa ya Wizara kuhusu utekelezaji wa Bajeti kwa kipindi cha mwezi Julai-Desemba, 2022.

Waziri wa Nishati, amesema kuwa ongezeko la uwezo wa mitambo hiyo ya kuzalisha umeme iliyoungwa katika mfumo wa gridi limetokana kuingizwa katika Gridi ya Taifa megawati 90 za umeme zinazozalishwa katika Kituo cha Kinyerezi I Extension.

Aidha, amesema kuwa, uwezo wa kuzalisha umeme kwa mitambo ambayo haijaunganishwa katika Gridi ya Taifa umefikia megawati 39.302 na hivyo kufanya jumla ya uwezo wa mitambo ya kuzalisha umeme nchini kufikia megawati 1,816.352 ikilinganishwa na megawati 1,733.38 zilizokuwepo mwaka 2021/2022 sawa na ongezeko la asilimia 4.89.
Screenshot_20230122_051741_OGInsta%2B.jpg
 
Baraza la Mitihani la Zanzibar limetangaza matokeo ya darasa saba mwaka 2022 ambapo watahiniwa wa 21, 241 kati ya 24, 580 waliofanya mtihani sawa na asilimia 86.42 wamefaulu kwa madaraja ya A, B, na D.

Watahiniwa 18, 892 wamefaulu kwa kiwango cha alama D sawa na asilimia 76.86 na waliofaulu daraja C 2, 259 sawa ana silimia 9.1, waliopata daraja B ni 90 sawa na asilimia 0.37 na daraja F ni 3, 339 sawa na asilimia 13.58.

Akitangaza matokeo hayo leo Jumamosi Januri 21, 2023 mjini Unguja, Mkurugenzi Mtendaji Baraza hilo, Othman Omar Othman amesema somo la dini limeongoza kwa asilimia 92.75 ikifuatiwa an somo la sayansi ya jamii asilimia 92.27 na Kiswahili kwa asilimia 89.04 kingereza asilimia 84.57.
Screenshot_20230122_051846_OGInsta%2B.jpg
 
Mtoto wa Rais wa Uganda Yoweri Museveni, Muhoozi Kainerugaba amesisitiza baba yake akimaliza muda wa uongozi katika nchi hiyo atachuku kiti hicho.

Muhoozi aliandika ujumbe kupitia mtandao wake wa Twitter jana Januari 20,2023 huku akiwaambia wale wanaotaka nafasi hiyo wameisha.

“Nitakuwa Rais wa nchi hii baada ya baba yangu. Wale wanaopigania nafasi hiyo wamepotea. MK Movement itashinda!!!.” aliandika Muhooza.

Screenshot_20230122_051946_OGInsta%2B.jpg
 
Kocha Mkuu wa Newcastle United, Eddie Howe anakuwa Muingereza wa kwanza kufikisha mechi 15 za EPL bila kufungwa ndani ya karne hii.

Magpies are flying under him
Screenshot_20230122_053955_OGInsta%2B.jpg
 
MECHI 6 KAGERA BILA USHINDI

FT| KAGERA SUGAR 0-0 COASTAL UNION

Kikosi cha Kagera Sugar kimeshindwa kupata ushindi kwenye michezo sita (6) mfululizo ya Ligi Kuu 2022|23.

Katika mechi hizo sita zilizopita, Kagera Sugar imekusanya alama nne (4) kutokana na sare nne (4) huku ikiwa imepota mechi mbili.

Kagera Sugar 0-0 Coastal Union
Singida Big Stars 1-0 Kagera Sugar
Dodoma Jiji 2-0 Kagera Sugar
Kagera Sugar 2-2 Geita Gold
Kagera Sugar 1-1 Simba
Kagera Sigar 2-2 Azam FC
Screenshot_20230122_054124_OGInsta%2B.jpg
 
Siku zinavyozidi kusonga mbele, Ihefu inaendelea kubadilika kuendana na kasi ya Ligi Kuu. Kwenye mechi tano (5) zilizopita imeshinda mechi tatu (3) na kupoteza mechi mbili (2).

Tanzania Prisons 1-2 Ihefu
Yanga 1-0 Ihefu
Ihefu 1-0 KMC FC
Ihefu 3-0 Mtibwa Sugar
Namungo 2-0 Ihefu

Tusubiri kuona watafanya nini baada ya usajili wao wa dirisha dogo!
Screenshot_20230122_054532_OGInsta%2B.jpg
 
Yanga imemtambulisha beki mpya wa kati Mamadou Doumbia raia wa Mali tayari kuanza majukumu yake ya kuwatumikia Wananchi akitokea Algeria alikokuwa na timu ya taifa wakishiriki michuano ya CHAN 2022.

Ujio wa Doumbia unamaanisha mabeki wa kati wa Yanga [Job, Mwamnyeto na Bangala] wakae sawa kupambana kuwania nafasi!
Screenshot_20230122_054633_OGInsta%2B.jpg
 
JERRY TEGETE AIBUKIA PAMBA
.
Kama ulidhani Jerry Tegete amestaafu kucheza soka, basi ulikosea kwani mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga na Toto Africans amejiunga na Pamba ya Mwanza kupitia dirisha dogo la usajili lililofungwa Januari 15 akipewa mkataba wa miezi sita hadi mwisho wa msimu huu.
.
Mara ya mwisho Tegete alionekana kwenye ligi ya ushindani msimu wa mwaka 2021-2022, akikipiga African Lyon kisha akarejea Mwanza ambako amekuwa akifanya mazoezi na timu ya Star Veterans.
Screenshot_20230122_054902_OGInsta%2B.jpg
 
ROBERTINHO::
.
“Mwanzo niliwambia nina vitu viwili akilini mwangu ambavyo nataka kuviingiza hapa Simba, moja ni timu Kushinda kila mechi na mbili ni Kuchez vizuri kwa kasi. Kwa maana hiyo kila mchezaji anaweza kuwa bora kama atavitambua hivyo na kuvifanyia kazi,”

Screenshot_20230122_054958_OGInsta%2B.jpg
 
ROBERTINHO

ambaye ni kocha mwenye mzuka uwanjani amesema bado hajapata kikosi chake cha kwanza lakini anaona mwanga kutokana na wachezaji wengi waliokuwa majeruhi kupona na wale waliosajiliwa dirisha dogo kuungana pamoja na kuamini wataisaidia timu kuwa tishio zaidi.

Screenshot_20230122_055117_OGInsta%2B.jpg
 
JUST IN: CEO wa Yanga, Andrew Mtine amemtumia barua kiungo Feisal Salum akimtaka kujiunga na wenzie kambini.
.
Ikumbukwe Feitoto alivunja mkataba na Yanga akitumia kipengele namba 14.7 cha mkataba ambapo ilimpasa kuilipa klabu pesa ya usajili pamoja na mshahara wa miezi 3 tu.
Screenshot_20230122_055214_OGInsta%2B.jpg
 
Nahodha wa Dodoma Jiji Mbwana Kibacha amesema licha ya Simba kuwa timu bora lakini wamejipanga kupata pointi tatu katika mchezo wa kesho, unaotarajiwa kufanyika saa 1:00 usiku katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.

Dodoma Jiji inashika nafasi ya 12 kwenye msimamo ikiwa na pointi 21 huku Simba wakishika nafasi ya pili wakiwa na pointi 47.

Mchezo wa mzunguko wa kwanza, Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-0 goli la kujifunga la aliyekuwa beki wa Dodoma Jiji,Abdallah Shaibu ‘Ninja Habib Kyombo na Moses Phiri.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Januari 21, 2023 Kibacha amesema wanajua utakuwa mchezo mgumu lakini wamejiwekea malengo ya kupata pointi tatu.

“Tunacheza na timu ambayo ipo katika nafasi nzuri sisi kama wachezaji jukumu letu ni kucheza na kuhakikisha tunashinda,"
Screenshot_20230122_055332_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom