Makapuku Forum

Makapuku Forum

NYIE HAMUOGOPI !?
.
Huko Dubai ROBERTINHO kazi imeanza na falsafa yake ni soka la kujilinda na kushambulia pamoja mwanzo mwisho
Screenshot_20230109_050332_OGInsta%2B.jpg
 
LUPEKENYA AVUNJIWA MKATABA COASTAL
.
Uongozi wa Coastal Union umevunja mkataba wa mwaka mmoja na miezi sita uliobakia wa aliyekuwa mshambuliaji wake, Optatus Lupekenya.
.
Taarifa kutoka ndani ya timu hiyo zinasema nyota huyo tayari amepewa barua ya kuachana na timu huku sababu kubwa ikielezwa ni kushindwa kuingia kwenye kikosi cha kwanza kama alivyotegemewa mwanzoni.

Screenshot_20230109_050420_OGInsta%2B.jpg
 
KALONDA, KADEDI WATEMWA MTIBWA
.
Mtibwa Sugar yenye masikani yake Manungu, Morogoro imeachana na kipa, Hamadi Kadedi pamoja na mshambuliaji wake, Matore Jeanpipi Kalonda.
.
Taarifa zimeeleza sababu kubwa ya viongozi kushindwa kuendelea nao hadi mwishoni mwa msimu huu ni kutokana na kushindwa kutimiza matakwa yao ya kimkataba.
Screenshot_20230109_050538_OGInsta%2B.jpg
 
WAJUMBE TFF WAGAWANYIKA, FEI AGOMA KURUDI YANGA
.
Wakati TFFl ikitoa taarifa iliyozua utata juu ya shauri la klabu ya Yanga dhidi ya kiungo Feisal Salum ‘Fei Toto’, upande wa nyota huyo kutoka Zanzibar umejipanga kukimbilia Mahakama ya Usuluhishi ya Kimataifa ya Michezo (CAS).
.
Hatua hiyo imekuja baada ya upande huo kuona hautatendewa haki baada ya TFF jana kutoa taarifa ikieleza Fei Toto ni mchezaji wa Yanga, huku ikieleza Kamati itatoa taarifa rasmi ya kesho Jumatatu.
.
Hata hivyo, kabla ya taarifa hiyo ya TFF taarifa ya kupenyeza kutoka kwa mmoja ya wajumbe wa kamati iliyosikiliza shauri hilo amedai wamegawanyika baadhi ya wajumbe wameweka mbele unazi wao kwa klabu wanazoshabikia na kuwavuruga wengine waliotaka kusimamia haki na sheria kuhukumu shauri hilo.
.
Kamati hiyo yenye watu saba, lakini zaidi ya nusu wameegemea upande mmoja, huku Fei akiweka bayana msimamo wake kwa wajumbe kwamba hawezi kurudi Yanga hata kama wameamua hivyo na kwamba ataitafuta haki yake mbele zaidi kwani anaamini yeye sio mchezaji wa Yanga kwa sasa.
.
Inaelezwa tayari Fei, alikuwa anasubiri hukumu ya shauri hilo kabla ya kuamua kwenda CAS kwani tayari ameshaukabidhi mkataba wake kwa wanasheria wa kigeni kwa kuamini kuwa wana nafasi kubwa ya kushinda shauri hilo hata kama TFF itaamua kupindisha kama ilivyotoa taarifa.
Screenshot_20230109_050633_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Kihamu

Kwanini kwenye taarifa ya Feisal Salum inasema hukumu kamili ni Jumatatu??

Nimepata wasaa wa kuwauliza Watalaam wa Sheria kuhusu hii statement, ni kuwa kwenye sheria kuna RATIO DECIDENDI ama RATIONALE FOR THE DECISION.

Kifupi ni kuwa Jumatatu Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji itaelezea SABABU za wao kusema Feisal ni Mchezaji halali wa Yanga kwa mujibu wa ushahidi na vielelezo lakini pia wataainisha vifungu vya Sheria ambavyo vinaonesha Feisal ni Mchezaji halali wa Yanga.

Hakuna majibu tofauti kati ya leo na Jumatatu kwakuwa ni siku tu ya kuelezea sababu za hukumu na watu waelewe sababu za kufikia maamuzi hayo.

Kwanini wamewahisha kutoa taarifa? Well ni interest ya jambo husika na kwakuwa haikuwa kesi ngumu sana kuisikiliza majibu yalipatikana mapema na umma umejulishwa.

Kilichosalia ni Feisal na Waajiri wake kufikia sehemu nzuri kama ataendelea Jangwani au ataondoka hiyo sisi wengine haituhusu sana
Screenshot_20230109_051242_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Kihamu

Baada ya majibu ya Kamati imeonekana wengi wanadai haki haijatendeka, maswali mengi nayojiuliza ni kuwa ili haki iwe imetendeka basi ilipaswa Yanga kuonekana imeshindwa? Bado kuna ukakasi kwenye tafakuri ya hili suala.

Maisha ya mpira wa miguu au hata taasisi yoyote watu huja na kuondoka ila taasisi zinasalia, sidhani kama Yanga wanamlazimisha Kiungo Maestro asalie kwenye timu yao bali wao wanataka taratibu tu zifuatwe, DEJAN ALIONDOKAJE SIMBA? Mnakumbuka?

Yanga ni klabu ambayo ina Wanachama na Mashabiki wake ambao wamechagua Viongozi kuwawakilisha kwa niaba yao, Yanga pia ina wabia kibiashara ambao wanataka kuona sura safi ya taasisi ambayo wameweka pesa zao, ulitarajia wakubali vitu viende kienyeji?

Mimi kama ningekuwa Mshauri wa Feisal najua ni ngumu yeye kuweka wazi timu ipi inamtaka kwakuwa FIFA wana mtego wa INFLUENCE OF THIRD PARTY yani shinikizo kutoka pande flani ndio maana huwezi kuona timu inayomtaka ikajitokeza ila kuna room ya Feisal na Yanga kuifikia.

Kwakuwa Feisal ana mkataba na Yanga kwa mujibu wa Kamati basi aende tu kuomba value yake pale Jangwani, watampa thamani yake halisi kwakuwa Feisal wa 2020 hawezi kuwa na value ile ile kwasasa kisha Kijana akasake maisha yake kwa kudeposit mzigo watakaosema.

Leo hii tutashangilia kwakuwa lipo Yanga ila kesho linaweza kutokea Simba, Mtibwa au Namungo kuwa Mchezaji kaamka tu anasema hana furaha na anahisi kuteswa hivyo anavunja mkataba na kuondoka, HAPANA vitu haviendi hivyo.

Kulipwa kidogo tofauti na wengine sio dharau kwakuwa kila Mtu ana namna yake ya kujadili mikataba yake, labda kutopewa gari sio dharau ukirejea kwenye mkataba kuna sehemu mliahidiana hivyo? Sio suala la kutokuwa na furaha bali suala na kimkataba mmekubaliana vipi.

Kila Kijana wa Kitanzania anamtakia heri Feisal na tunapenda kuona wenzetu wakipata maslahi mazuri sana ila mwisho wa siku kuwa na Menejimenti sahihi ambao watakupa thamani yako sahihi, mpira umebadilika sana kinachoandikwa ndicho kinapaswa kutekelezwa.

Tupo wengine ni Freelancers, wapo wengine wanalipwa ujira mdogo tu ila mwisho wa siku ni makubaliano yenu tu.

Screenshot_20230109_051242_OGInsta%2B.jpg
 
FT: Mlandege 1-1 Namungo (Bashima 45+5’) (Mkoko 7’)

Mlandege wanafuzu hatua ya fainali Mapinduzi Cup 2023 kwa kuifunga Namungo FC kwa mikwaju ya penati 5-4
Screenshot_20230110_044222_OGInsta%2B.jpg
 
Mbunge wa Muheza, Hamisi Mwinjuma maarufu Mwana FA amekutana na Wakuu wote wa Idara na vitengo ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Muheza katika kikao alichokiitisha kwa Wilayani humo.

Lengo kuu la kikao ilikua ni pamoja na kuweka mikakati ya pamoja na kujadili changamoto zinazojitokeza kwenye majukumu ya kila siku ya kuwatumikia Wananchi wa Jimbo la Muheza.

Katikati ya Kikao hicho cha Mwana FA na Watendani wenzake walipata ugeni wa ghafla wa Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tanga, Rajab Abdulrahman ambapo aliwasalimia na kuacha nasaha zake ikiwa ni katika kuhakikisha ilani ya Chama cha Mapinduzi, Chama chenye dhamana ya kuwatumikia Wananchi kwa sasa, inatekelezwa kwa ufanisi.

Wengine ni waliohudhuria Kikao hiki ni pamoja na Mwenyekiti wa Halmashauri na Sektetarieti ya CCM ya Wilaya ikiongozwa na Katibu wa CCM wilaya Ndugu Simon Leng’ese.
Screenshot_20230110_044321_OGInsta%2B.jpg
 
Serikali inatarajia kuanza kutekeleza mradi wa ukarabati wa kiwanja cha ndege Kigoma kwa gharama ya Tsh. Bilioni 46.68 utakaohusisha jengo la abiria lenye uwezo wa kuhudumia abiria laki nne kwa mwaka, Zimamoto na mnara wa kuongozea ndege pamoja na vifaa mbalimbali.

Serikali imetia saini mkataba na Mkandarasi wa kampuni ya China Railway Construction kwa ajili ya ujenzi kwa muda wa miezi 18 fedha ambazo ni mkopo wa riba nafuu kutoka Benki ya Uwekezaji ya ulaya EIB.

Mtendaji Mkuu wa TANROADs Mhandisi Rigatus Matavila amesema utawezesha uwanja huo kuanza kutumika kwa saa 24 lakini pia ndege kubwa kutua.
Screenshot_20230110_044429_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom