Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20230106_062824_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20230106_062841_Opera%20Mini.jpg
 
VIFAA VYA WAAMUZI NI POSHO YA MECHI
.
Mwamuzi wa Ligi Kuu anapokuwa
kwenye mechi, inaelezwa analipwa kati ya Sh 300,000 hadi 350,000 kwa mechi, pesa ambayo inajumlisha nauli ya kutoka anakoishi kufika kwenye kituo cha kazi na gharama za malazi na chakula.
.
Ukipiga hesabu kwa haraka haraka, pesa ya posho kwa mwamuzi wa Ligi Kuu inaweza kufika gharama ya vitendea kazi vyake vyote anavyopaswa kuwa navyo.
.
Mfano gharama za kiatu kwa mwamuzi, kuwa cha bei ya chini uwa ni Sh 45,000 na kile cha bei kubwa ni Sh 120,000, lakini pia jezi ambayo moja ni Sh 25,000 mara nne, hivyo laki moja.
.
Kibendera ni Sh 35,000, kuna filimbi ambazo zinahitajika kuwa tofauti tofauti ili ikitokea mashabiki wana filimbi yenye mlio kama wa mwamuzi inabidi uweze kubadilisha, kadi na vifaa vingine vinavyohitajika kwa waamuzi.
Screenshot_20230106_063735_OGInsta%2B.jpg
 
Mwamuzi Mateu Lahoz ambaye aliweka rekodi ya kutoa kadi nyingi zaidi za njano kwenye derby ya Catalunya kati ya Barcelona na Espanyol ametangaza kustaafu rasmi mwishoni mwa msimu huu.
Screenshot_20230106_063849_OGInsta%2B.jpg
 
Nyota Hector Bellerin ameibua hoja kuhusu Wanasoka na kulipa kodi, anasema wana kasumba ya utajiri hawapo tayari kumiliki gari moja bali kumi, anasema kwakuwa wamejaliwa kipato basi wasiwe wazito kulipa kodi kwa ajili ya maendeleo ya Wananchi wa kawaida ambao hawawezi kuwa na maisha kama wao.
Screenshot_20230106_063952_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa shirikisho la soka nchini Cameroon, Samuel Eto'o aliwaondoa wachezaji 21 kati ya 30 wa timu ya vijana ya U17 ya Cameroon baada ya kufeli kwenye vipimo vya umri.

Kocha wa kikosi hicho Jean Fiala akaita wachezaji wengine wapya, nao baada ya vipimo 11 wamebainika wamevuka miaka 17.
Screenshot_20230106_064103_OGInsta%2B.jpg
 
Kwa mujibu wa Daily Mail ni kuwa Cristiano Ronaldo atazikosa mechi mbili za Al Nassr kutokana na kutumikia adhabu baada ya kutupa simu ya Shabiki mmoja wa Everton chini huku nchini England hivyo adhabu itaendelea mpaka alipohamia hivi sasa.
Screenshot_20230106_064210_OGInsta%2B.jpg
 
Ihefu imetangaza kuachana na nyota wake watano kwenye hili dirisha dogo na wamewatakia heri waendako.

Ally Ramadhan Oviedo anahusishwa na klabu kadhaa za ligi kuu na huenda akapata timu mapema zaidi ya kucheza.
Screenshot_20230106_064314_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Nimeona taarifa ya tuzo ambayo Striker tishio kwenye ligi yetu ameipata ambayo ni Mchezaji bora wa Kongo kwa 2022, lakini tunasahau kumalizia wa Website au page flani hapo unakuwa umemaliza.

Mfano ShaffihDauda, Millard Ayo, Soka Online, @qudabash_jr .com au Mwandishi au page ichuje wachezaji wasalie kadhaa halafu waweke link maalum ya watu kupiga kura, hii sio tuzo maalum ya mpira wa Kongo bali page flani ndani ya Kongo, inapaswa kusomeka hivyo.

Mchezaji bora wa Kongo anatangazwa na Chama chao cha soka (Federation Congolese de Football Association) na ukienda kwenye website yao rasmi taarifa ya mwisho ni December 23 ikihusu mambo ya CHAN kwa timu yao ya taifa.

Lazima tumpe pongezi Fiston lakini tuzo ya Mchezaji bora wa nchi fulani haipigwi na kila Mtu kutoka mataifa mengine, hii inatokana na link na yoyote duniani anaweza kupiga kura.

Nimeziona hizi tuzo hata kuna moja ya Beki bora alichukua Inonga ilikuwa ni ya page flani imepigisha kura na yoyote anapiga, kwetu inatrend lakini uje kwenye uhalisia tu Kongo ina talents ngapi? Hawazijui?

Ukienda kwenye hizo page zimejiweka wazi tu kwenye bio zao kuwa ni News and Media mfano hiyo Leopard Leader Foot, haipaswi kuwa stori kubwa mpaka page ya klabu ipost, ni vitu ambavyo hatupaswi kuvipa uzito sana, kuanzia ya Inonga mpaka hii, ni page tu hizo.

Ni sahihi kusherehekea lakini ni vyema zaidi kufahamu ni tuzo ya aina gani na imetokea wapi, kila nchi ina tuzo zake rasmi zinazotambulika na Shirikisho lao! Umeona taarifa ya Mayele au Inonga kwenye websites zao? Wapi walipublish? Hakuna.
Screenshot_20230106_064613_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Nimeona post ya Kaka angu Priva kuwa niombe radhi kwakuwa amehisi nimedharau tuzo aliyoshinda Fiston Mayele kutoka kwenye page moja nchini Kongo, sijaelewa kwanini niombe radhi ikiwa sijadharau tuzo hiyo.

Niombe radhi kwasababu nimesema ulichopost kwenye page ya klabu kilipaswa kuhitimishwa vyema? Kuwa Fiston Mayele ni Mchezaji bora wa Kongo kwa mujibu wa page flani huko kwao?

Page rasmi ya klabu imepost taarifa sahihi lakini sio kamili, MVPs wawili kwa maana ya Aucho na Mayele kwa context ile wametokana na page za mitandaoni, malizia tu statement hapo kuna shida gani? Priva napaswa kuomba radhi?

Tazama hata page za timu za Ulaya kama Mchezaji ameshinda tuzo ya FWA (Football Writer’s Association) watatoa credit, akishinda BBC Sports Personality watatoa credit, iwe Ballon au FIFA Best Men watatoa credit, Priva kama hizo tuzo ni kubwa na zina uzito huo kwanini hamjamalizia taarifa?

A simple logic tu Kaka angu, page nyingine Rwanda ikitoa tuzo, Kenya ikatoa, Tanzania, Namibia, Zambia hizo zote mtapost? Ndio maana kuna tuzo zinazofahamika na Mashirikisho pamoja na klabu na ndio hizo zinachapishwa kwenye kurasa zao, simple logic Kaka.

Umeitaja Ballon dor kikawaida sana yani kama vile kitu chepesi ila nenda kasome vizuri asili ya hizo tuzo, kasome vyema Waandishi wawili waanzilishi wa hizo Gabriel Hanot na Jacques Ferran, kisha kafuatilie Pioneers wa European Cup ni wakina nani, Euro Cup ilianza 1955 na hizo tuzo zikaja 1956.

Halafu kapitie tena kuhusu Ballon dor ya French Football Magazine, imeanza 1956 ifuatilie vyema Ulaya kama walikuwa na tuzo zaidi ya hizo, kisha nenda mpaka 1995 walibadili nini kisha fika tena miaka ya 2010 FIFA wakaomba nini kutoka kwao, kisha uje uconnect na unachosema.

Ukaitaja BBC na tuzo zao kirahisi sana, lakini pia tulia nenda kawasome vyema BBC, fuatilia panel inayokaa kuteua majina shindani, fuatilia wana blessings gani kutoka vyombo vya mpira kisha uje hapa tuzungumze vyema Kaka angu.

Halafu mwisho Bro angu kafuatilie utofauti wa MAGAZINE, Newspaper na hiyo page ya tuzo, nitaomba radhi baada ya hapo, nitachutama kama ulivyosema ukishakuja na hizo content.
Screenshot_20230106_064739_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom