Idadi ya watu wanaopoteza maisha kwa ugonjwa wa kipindupindu nchini Malawi imezidi kuongezeka kutoka watu 661 hadi kufikia vifo 687.
Kupitia taarifa iliyotolewa Jumamosi Januari 7,2023 kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Waziri wa Afya nchini Malawi Khumbize Chiponda Januari 5 tayari kulikuwa na vifo 661 na kufikia Januari 7, watu 687 wamepoteza maisha.
“Katika saa 24 zilizopita, kumeropotiwa maambukizi mapya 427 na vifo vipya 13 na watu tisa wanashukiwa kuwa na maambukizi ya ugonjwa huo,
Tayari maambukizi yameriopotiwa katika wilaya Blantyre watu 100, Mangonchi 79, Lilongwe 60, Machinga38 Balaka 36, Salima33, Dedza 16, Dowa 15, Zomba 13, Thyolo 9, Mulanje 6." Alisema Waziri Chiponda.
Mbali na wilaya hizo Waziri huyo ametaja wilaya zingine kuwa ni”Kasungu yenye maambukizi 5, Likoma 4, Neno 3, Phalombe 3, Nkhotakota2, Karoga 2, Mchinji 1, Chiradzulu 1 na Ntcheu 1.
Amebainisha kuwa hadi Januari 7 watu 20,527 wamekumbwa na ugonjwa huo nchini humo huku watu 19,031 wakirejea katika hali zao na wengine 809 wakiwa kwenye matibabu huku akiweka wazi kwamba hospitali zote za wilaya nchini humo zimeripoti kupokea wagonjwa wa kipindupindu.