

Farhan Jr
Ukizungumza na Washindi wote watakwambia its lonely at the top, watakwambia pale juu pana upweke mkubwa sana, watakwambia kufanikiwa ni mateso sana.
Niliwahi kusimama darasani wakati nafundisha watoto wangu wa Kinondoni Islamic nakumbuka lilikuwa Form6 lile darasa, nikawaambia Watoto wangu dunia tunayoishi inataka kuona KIASI tu, usifanikiwe sana na usifeli sana.
Muulize Diamond wa Bibie Sandra, muulize Ali kijana wa Saleh Kiba au muulize Cristiano Ronaldo ukipata wasaa hata Mama yangu Lady Jay Dee, watakwambia its lonely at the top, juu pale pana upweke sana.
Wakati mwingine namtazama sana MO Hussein yupo juu mno kwasasa na tayari wengi wamemchoka kwakuwa tuna tabia ya kukinai mafanikio ya Mtu, amini usiamini watu wanasubiri MO akosee tu waseme, MO anafahamu kuwa pale juu pana upweke mkubwa sana ila hawezi kusema hadharani.
Nakumbuka niliwaambia watoto wangu siku ile darasani kuwa mafanikio yanatisha sana, nikawapa visa vingi mfano cha Whitney Huston, Michael Jackson niliwauliza maisha yao yaliishaje? Hata Mama yangu Brenda Fassie yaliishaje? Au hata Albert Mangwea, its lonely at the top.
Washindi wanapitia mengi sana, hawawezi kusema kirahisi! Leo hii wengine hawataki tu ngoma za Diamond ila hawana sababu, hawapendi tu uwezo wa MO Hussein bila sababu, hawamkubali tu Ronaldo bila sababu! Waulizeni watawaambia, pale juu panatisha sana.
Washindi wakisema kitu mbele ya waliofeli basi wanaambiwa wanajisikia, wakikaa kimya wataambiwa wanajiona, wakipatia watapondwa na wakikosea watatukanwa, wanafahamu hilo.
FORM 6 wa Kinondoni Islamic 2019 nadhani kama wanasoma hapa wanakumbuka wosia huu, niliwaambia mafanikio yanatisha sana! Its lonely at the top, siku moja nikirudi tena kushika chaki nitawaambia vizuri Wanafunzi wangu.
View attachment 2388705