Makapuku Forum

Makapuku Forum

UMAFIA WA SIMBA ANGOLA BALAA
.
Mkubwa ni mkubwa tu na ndicho kilichojidhihirisha katika safari ya Simba kwenda Angola kucheza dhidi ya Primiero de Agosto. Simba iliamua kuwapima kipimo cha Uviko-19 wachezaji wake na benchi la ufundi ili kuwaepusha na usumbufu wa kulazimishwa kupima katika Uwanja wa Ndege wa Luanda kwa vile vipimo walivyofanya nyumbani, vinadumu kwa muda wa saa 72.
.
Iwapo vipimo vingefanyika katika Uwanja wa Ndege wa Luanda, Simba iangelazimika kutumia muda mrefu zaidi jambo ambalo lingewafanya wachezaji kuathirika kisaikolojia. Mara baada ya kufika uwanjani hapo, walikutana na basi kubwa la kubebea abiria ambalo waliandaliwa na wenyeji wao, lakini Simba waliamua kutolitumia na badala yake wakatumia lingine lililoandaliwa na wao wenyewe Simba huku lile la mwanzo wakipakizwa mashabiki walioambatana na Simba hapa.
.
Hotelini, Simba iliweka ulinzi mkali katika vyumba vya wachezaji na hata chakula cha wachezaji kilipikwa na wao wenyewe kupitia mpishi waliyeambatana naye.
Screenshot_20221010-093145_OGInsta%2B.jpg
 
CR7 HAKUNA TIMU ZINAMTAKA
.
Cristiano Ronaldo anaripotiwa ataendelea kubaki Manchester United kwa sababu hakuna klabu nyingine inayotaka kumsajili. CR7 alitaka kuondoka dirisha lililopita na huenda akahitaji hilo litokee pia Januari. Hata wachezaji wenzake wataka aondoke, lakini shida hakuna timu inayohitaji huduma yake kwa sasa.
Screenshot_20221010-094034_OGInsta%2B.jpg
 
CR7 HAKUNA TIMU ZINAMTAKA
.
Cristiano Ronaldo anaripotiwa ataendelea kubaki Manchester United kwa sababu hakuna klabu nyingine inayotaka kumsajili. CR7 alitaka kuondoka dirisha lililopita na huenda akahitaji hilo litokee pia Januari. Hata wachezaji wenzake wataka aondoke, lakini shida hakuna timu inayohitaji huduma yake kwa sasa. View attachment 2382315
Kazeeka
 
CAF CHAMPIONS LEAGUE
.
AL HILAL YANGA SC
21:00
Al Hilal stadium
.
YANGA itashuka Uwanja wa Al Hilal Omdurman, ikiwa na kibarua cha kusaka USHINDI wa aina yoyote au sare ya kuanzia mabao 2-2 ili waweze kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Mabingwa Afrika kwa mara ya kwanza tangu 1998.
.
Pamoja na kukiri ugumu wa mchezo huo wa ugenini, Yanga bado wana imani ya kupata matokeo mazuri katika mchezo wa leo yatakayowaingiza makundi. Kila la Kheri @yangasc
Screenshot_20221016-081650_OGInsta%2B.jpg
 
CAF CHAMPIONS LEAGUE
.
SIMBA SC DE AGOSTO
16:00
Benjamin Mkapa
.
SIMBA haitokuwa na mlima mrefu wa kupanda wakati watakapoikaribisha Agosto kwani ushindi wa mabao 3-1 ugenini umeifanya ihitaji sare yoyote kuwavusha kwenda makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika na kuwa mara ya tatu MFULULIZO huku ikifanya hivyo kwa mara nne katika misimu mitano ya hivi karibuni.
.
Pamoja na kuingia katika mchezo wa leo ikiwa na nafasi kubwa ya kusonga mbele, Simba imesema haitobweteka. Kila la kheri @simbasctanzania
Screenshot_20221016-081826_OGInsta%2B.jpg
 
MBAPPE SHIDA YAKE NI HII
.
Kylian Mbappe inadaiwa aliahidiwa na PSG ingewasajili Robert Lewandowski, Milan Skriniar na Bernardo Silva kwenye dirisha lililopita la uhamisho wa majira ya kiangazi na hivyo kukubali kusaini mkataba mpya wa miaka mitatu.
.
Dirisha limefungwa na hakuna hata mmoja kati ya nyota hao aliyesajiliwa Parc des Princes jambo linalomfanya Mbappe ahisi kusalitiwa.
Screenshot_20221016-081940_OGInsta%2B.jpg
 
KATUMBI AMTIMUA KOCHA UWANJANI
.
Bilionea wa TP Mazembe, Moise Katumbi kuonyesha kukerwa na Matokeo ya timu yake kutolewa katika Ligi ya Mabingwa Afrika amemtupia virago kocha mkuu Franck Dumas.
Screenshot_20221016-082140_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Ukizungumza na Washindi wote watakwambia its lonely at the top, watakwambia pale juu pana upweke mkubwa sana, watakwambia kufanikiwa ni mateso sana.

Niliwahi kusimama darasani wakati nafundisha watoto wangu wa Kinondoni Islamic nakumbuka lilikuwa Form6 lile darasa, nikawaambia Watoto wangu dunia tunayoishi inataka kuona KIASI tu, usifanikiwe sana na usifeli sana.

Muulize Diamond wa Bibie Sandra, muulize Ali kijana wa Saleh Kiba au muulize Cristiano Ronaldo ukipata wasaa hata Mama yangu Lady Jay Dee, watakwambia its lonely at the top, juu pale pana upweke sana.

Wakati mwingine namtazama sana MO Hussein yupo juu mno kwasasa na tayari wengi wamemchoka kwakuwa tuna tabia ya kukinai mafanikio ya Mtu, amini usiamini watu wanasubiri MO akosee tu waseme, MO anafahamu kuwa pale juu pana upweke mkubwa sana ila hawezi kusema hadharani.

Nakumbuka niliwaambia watoto wangu siku ile darasani kuwa mafanikio yanatisha sana, nikawapa visa vingi mfano cha Whitney Huston, Michael Jackson niliwauliza maisha yao yaliishaje? Hata Mama yangu Brenda Fassie yaliishaje? Au hata Albert Mangwea, its lonely at the top.

Washindi wanapitia mengi sana, hawawezi kusema kirahisi! Leo hii wengine hawataki tu ngoma za Diamond ila hawana sababu, hawapendi tu uwezo wa MO Hussein bila sababu, hawamkubali tu Ronaldo bila sababu! Waulizeni watawaambia, pale juu panatisha sana.

Washindi wakisema kitu mbele ya waliofeli basi wanaambiwa wanajisikia, wakikaa kimya wataambiwa wanajiona, wakipatia watapondwa na wakikosea watatukanwa, wanafahamu hilo.

FORM 6 wa Kinondoni Islamic 2019 nadhani kama wanasoma hapa wanakumbuka wosia huu, niliwaambia mafanikio yanatisha sana! Its lonely at the top, siku moja nikirudi tena kushika chaki nitawaambia vizuri Wanafunzi wangu.

Screenshot_20221016-082313_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Kupitia mtandao wa Instagram nilipata connection flani ya Jamaa yupo Atalanta, Georgia huko Marekani tukawa tunapiga stori mbili tatu kuhusu football akaniuliza kwanini Neymar Jr ndie mchezaji wako bora wa muda wote?

Alitaka kufahamu sababu, kwanza kabisa nikamkumbusha kwanza kuhusu De Toekomst, ndio hiyo shule maarufu ya soka inaitwa Ajax Youth Academy, iliyoanzishwa rasmi Machi 18, 1900 kisha nikamwambia dhumuni kubwa la academy hiyo na watu wa Ulaya.

Wenyewe wanakiits kiwanda ambacho Binadamu wanatengenezwa, baada ya ile kauli ya Mungu aliumba dunia kisha Mdachi aliitengeneza Uholanzi, hapa kuna elimu kidogo kuhusu Land Reclamation, tuiache kidogo.

Wazungu baada ya kuzunguka sana dunia kuanzia bahari ya Hindi mpaka Atlantic wakapata ripoti za kichunguzi kuhusu talents halisi zinazopatikana eneo hilo, walihitaji kuwahi mbele ya muda kuhakikisha mpira unachezwa na kuhusudiwa zaidi barani Ulaya lakini bado ilishindikana.

Baada ya tafiti mbalimbali za kisayansi wakaja na TIPS MODEL mfumo ambao binadamu mdogo anatengenezwa kuwa venye Ajax wanataka, wakiamini Uholanzi ni majaribio mazuri kisha isambae Ulaya nzima, hata uwanja wa ndege mkubwa Ulaya ni Schipol upo Amsterdam, kifupi Uholanzi ina maana kubwa sana.

Walishachungulia mbele ya muda na kuona kuwa baada ya Millitary Supremacy basi mpira utakuwa sababu moja wapo ya ukubwa wa mataifa duniani, walihofu Brazil na Afrika zitasogea kupunguza gap la umaskni kutokana na pesa za mpira.

Ilibidi isukwe plan ambapo hii ya academy na mifumo mikubwa ya kisayansi bado haikufua dafu mbele ya miguu ya Roger Milla, Jay Jay Okocha, Ronaldinho, De Lima, Maradona na mafundi wengine kutoka bahari ya Hindi na Pacific.

Bado maswali yakawa mengi kwenye maabara ya soka kuwa soka linahamiaje Ulaya? Afrika na Amerika Kusini watadondoka vipi? Hapo ndipo kilipo kisa changu na kwanini NEYMAR JR ndie Mchezaji wangu bora wa muda wote.

Leo usiku nikimaliza kuchat nae, nitarudi kuwasimulia hoja zangu na dunia iliyofichwa.

Screenshot_20221016-082443_OGInsta%2B.jpg
 
Shughuli za KIKUBWA hufanywa na WAKUBWA pekee, Mnyama ameingia kwenye jambo lake la wakubwa wenzie.

Kongole Kocha Mgunda
Mechi 4 CAF CL
Ushindi 4
Mabao kufunga 8
Mabao kufungwa 1

Simba imeshinda mechi zote 2 za ugenini kwa mara ya kwanza na kuingia hatua ya makundi.

Simba imeshinda mechi zote 4 na kuingia hatua ya makundi kwa mara ya kwanza.

Simba imefungwa mabao machache 1, kabla ya kuingia hatua ya makundi.

Mgunda ni Kocha wa 2 Mtanzania baada ya Marehemu TITO MWALUVANDA kuingiza timu ya Tanzania kwenye hatua ya makundi ya CAF CL. Mwaluvanda aliingia hatua hii na Yanga mwaka 1998.

Muda wa kumuamini Mgunda na Matola ni SASA, utaleta kocha wa Nje kuja kufanya nini zaidi ya hiki anachofanya Mgunda na Matola?

Asipofanikiwa huyo kocha utajiweka pabaya. Simba ya Mgunda imeimarika na Boli INATEMBEA SANA.

BIN KAZUMARI (Voice of the voiceless)
Screenshot_20221016-231449_OGInsta%2B.jpg
 
FT: Al Hilal 1-0 Yanga SC

Yanga SC wameondoshwa Ligi ya Mabingwa na sasa watacheza Kombe la Shirikisho.

Haikuwa rahisi sana namna Yanga ilivyotolewa kama ambavyo isingekuwa rahisi kushinda Omduraman.

Yote kwa yote bado kama Nchi tuna timu 2 mashindano ya CAF. Simba SC kwenye Ligi ya Mabingwa - CAF CL na Yanga SC kwenye kombe la Shirikisho - CAF CC.

Bado wananchi wanaweza kucheza makundi lakini ni Shirikisho, Ligi ya Mabingwa mpaka wakati ujao.

Mara ya mwisho ilikuwa 1998 wakati huo hatua ya makundi inaitwa robo fainali, lakini kwa Shirikisho walicheza makundi mara ya mwisho mwaka 2016.
Screenshot_20221016-231603_OGInsta%2B.jpg
 
FT: Al Hilal 1-0 Yanga SC

Yanga SC wameondoshwa Ligi ya Mabingwa na sasa watacheza Kombe la Shirikisho.

Haikuwa rahisi sana namna Yanga ilivyotolewa kama ambavyo isingekuwa rahisi kushinda Omduraman.

Yote kwa yote bado kama Nchi tuna timu 2 mashindano ya CAF. Simba SC kwenye Ligi ya Mabingwa - CAF CL na Yanga SC kwenye kombe la Shirikisho - CAF CC.

Bado wananchi wanaweza kucheza makundi lakini ni Shirikisho, Ligi ya Mabingwa mpaka wakati ujao.

Mara ya mwisho ilikuwa 1998 wakati huo hatua ya makundi inaitwa robo fainali, lakini kwa Shirikisho walicheza makundi mara ya mwisho mwaka 2016.View attachment 2389575
hii kitaalamu imekaaje
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom