Makapuku Forum

Makapuku Forum

Huyu ndie alikuwa anamuasha Malkia.
Mimi na wewe tukitaka kuwahi kuamka huwa tunategesha alarm. Lakini kwa Malkia ilikuwa tofauti.

Yeye alikuwa na mpiga filimbi wake ndie ilikuwa alarm yake.. Karibu kila siku asubuhi mpiga filimbi alikuwa anakwenda dirishani kwa Malkia na kupuliza filimbi kwa muda wa dakika 15 mfululizo ili kumuamsha Malkia.

Baada ya mazishi ya kitaifa mpiga filimbi wa Malkia alipiga filimbi ya mwisho huku akitoka nje ya kanisa kuashiria kwamba Malkia hatoamka tena. Maziko binafsi yatakayoudhuriwa na wanafamilia na ndugu wa karibu yanafanyika jioni hii kwa saa za Uingereza huko London.

Leo wakati mwili unaingizwa Kanisani maneno haya kutoka kwenye Biblia yaliyosomwa,"Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu; BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA lihimidiwe." Katika kaburi la Malkia kutakuwa na maneno machache tu ELIZABETH WA PILI (1926-2022) wala neno Malkia halitaandikwa..!
Screenshot_20220920-064916_OGInsta%2B.jpg
 
Huyu ndie alikuwa anamuasha Malkia.
Mimi na wewe tukitaka kuwahi kuamka huwa tunategesha alarm. Lakini kwa Malkia ilikuwa tofauti.

Yeye alikuwa na mpiga filimbi wake ndie ilikuwa alarm yake.. Karibu kila siku asubuhi mpiga filimbi alikuwa anakwenda dirishani kwa Malkia na kupuliza filimbi kwa muda wa dakika 15 mfululizo ili kumuamsha Malkia.

Baada ya mazishi ya kitaifa mpiga filimbi wa Malkia alipiga filimbi ya mwisho huku akitoka nje ya kanisa kuashiria kwamba Malkia hatoamka tena. Maziko binafsi yatakayoudhuriwa na wanafamilia na ndugu wa karibu yanafanyika jioni hii kwa saa za Uingereza huko London.

Leo wakati mwili unaingizwa Kanisani maneno haya kutoka kwenye Biblia yaliyosomwa,"Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu; BWANA alitoa, na BWANA ametwaa; jina la BWANA lihimidiwe." Katika kaburi la Malkia kutakuwa na maneno machache tu ELIZABETH WA PILI (1926-2022) wala neno Malkia halitaandikwa..!View attachment 2362250
Nimefurahi kusikia na wao wanafahamu kwamba hatukuja na kitu duniani na kadhalika hatutarudi na kitu, ila moyo uliopondeka ndio tutarudi nao!
 
Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Albert Chalamila amewapiga marufuku watumishi wa kata na mitaa kuwalazimisha wafanyabiashara kufunga maduka yao ili kufanya usafi.

Hayo yamebainishwa leo Septemba 23, 2022 wakati akizungumza na Shirikisho la Umoja wa Wamachinga, Mama Lishe/Baba Lishe, Jamii Mpya, Wanawake Wafanyabiashara, Jukwaa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi na Shujaa wa Maendeleo wa Mkoa wa Kagera, ikiwa ni mwendelezo wa kuzungumza na makundi mbalimbali ya kijamii.

Chalamila ameongeza kuwa “dhana hii ya kuchagua siku moja kuwa ni siku ya usafi inarudisha nyuma ukuaji wa kiuchumi na kupelekea baadhi ya wafanyabiashara kutofungua biashara zao.”
Screenshot_20220924-033358_OGInsta%2B.jpg
 
Baadhi ya wanaume wa Kijiji cha Kambi ya Chokaa Naisinyai pamoja na vijiji vya jirani na eneo hilo wilayani Simanjiro mkoani Manyara wametelekeza familia zao kwa visingizo vya kutafuta malisho ya mifugo na wengine kukimbilia mijini kutafuta vibarua kutokana na njaa iliyosababishwa na ukame wa miaka miwili mfululizo.
Screenshot_20220924-033604_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

DUNIA YA MAINJINIA HERSI @caamil_88 NA FLORENTINO PEREZ DHIDI YA DUNIA YENU (PART ONE)

Asubuhi moja ya 2000 ni Millenia mpya hii akiwa kwenye jengo lake refu la kampuni yake ya ACS jijini Madrid alimwambia Msaidizi wake kuwa ana ndoto za kuwa Rais wa Real Madrid.

Don Perez akiwa ametulia huku akipiga funda la kinywaji baridi kabisa, Msaidizi wake binafsi ambaye ni Mwanamama mmoja mwenye mchanganyiko wa Morocco kwa Mama na Baba ni kutoka visiwa vya Mallorca akamtazama Perez.

Ilibidi asimame kusogea mpaka kwenye meza yake na kumuuliza kwa upole “Umewaza nini na inawezekana vipi?” Ofcourse ndio kazi ya Wasaidizi kama yule wa @hajismanara !

Kumbuka Rais wa Real Madrid wakati huo ni Lorenzo Sanz ambaye ametangaza kuwa anagombea tena na ametoka tu kushinda UEFA, lakini Perez hakujali hilo na alishakuwa na mpango wake wa kuteka hisia za Wanachama.

Alianza kwanza kwa kufanya utafiti juu ta Staa mkubwa wakati huo nchini Hispania, ambapo majibu yalikuwa ni Luis Figo ww Barcelona ambaye ni raia wa Ureno, nyota ambaye hata wachezaji wa Real Madrid walimuogopa sana.

Perez mchana mmoja akamuita Mwandishi Luis Alberdo ofisini kwake, akamsainia cheque ya kusafiri mpaka Barcelona kwa ajili ya kufanya tafiti na kurejea na taarifa zote muhimu kuhusu Figo na Barcelona, tazama Mafia anavyofanya kazi zake kimafia dhidi ya dunia yenu ya mahindi kwa chumvi

Walipata taarifa za siri kuwa Figo hana furaha ndani ya Barca, licha ya kupendwa sana na Mashabiki, licha ya kipaji kikubwa na mafanikio yote aliyoleta ila Viongozi hawakumpa thamani anayostahili, hivyo anaenda EURO 2000 nchini Ufaransa akiwa hana furaha kabisa, ripoti ilifika mezani kwa Perez, akaweka miwani yake sawa na kuangusha kete moja.

Don Perez moyoni mwake akajisemea kuwa Luis Figo ndio kete yangu ya turufu ili nishinde uchaguzi huu kwa mara ya kwanza dhidi ya Gwiji Lorenzo Sanz, tazama akili ya Engineer Perez kwenye jambo zito la kutingisha duniani, mkasa huo maarufu huitwa “The transfer that changed world football”

Tayari anataka kutangaza sera zake kuelekea uchaguzi, anawaza atamfikiaje Figo na Wakala wake Jose Viega ili amnase Mreno huyo? Patamu hapo!

ITAENDELEA…
Screenshot_20220925-161328_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

BAADA YA RAIS HERSI WA YANGA KUSEMA YANGA INAENDESHWA KWA HASARA, NIKAIKUMBUKA HII POST AMBAYO NILITUKANWA SANA! TUJIKUMBUSHE

・・・
Jana niliandika kitu kuhusu MO Dewji kisha nikazima data nikapumzika kwakuwa ilikuwa usiku sana, naamka napitia comments, Insta mpaka WhatsApp nahisi hatujaelewana.

Naomba siku moja nikipata wasaa nitawapa vitu kutoka kwenye kitabu kimoja nachomalizia kukisoma “FOOTBALL IS NOTHING THAN A PRESTIGIOUS GAME”

Ni kitabu kizuri sana kinachozungumzia mpira kuanzia Pre Bosman na Post Bosman era, kinazungumzia kuwa mpira sio biashara kama ambavyo wengi wanadhani bali ni Mchezo wa sifa tu.

Kitabu kinasema Matajiri wanaowekeza kwenye mpira au Matajiri wanaosimamia mpira wameingia kama sehemu ya sifa kwa timu zao na kuhakikisha timu zinapata furaha kwakuwa ni furaha yao pia.

Leo hii watu wanasema Simba ina Wadhamini ambao wanahesabika wote, lakini duniani kuna klabu kama Real Madrid na Barcelona, Manchester United na bado zina madeni, unafahamu ni kwanini? Hiyo ni homework.

Leo hii Real Madrid ili uwe mgombea wa Urais lazima uwe na sifa ya kukopesheka kwenye benki zinazotambulika na mamlaka, ambazo ni EURO MILLION 124 ambayo ni sawa na 15% ya bajeti ya Real Madrid kwa mwaka, unafikiri ni kwanini? Homework hiyo naiacha.

Juzi Rais wa Barcelona Joan Laporta na Mhazini wa klabu Ferran Olive walitoa zaidi ya Pauni Million 20 ambazo ni pesa zao binafsi, ili Jules Kounde asajiliwe kwenye mfumo wa LA LIGA, unafikiri ni kwanini? Simply ni kuwa mpira bado sio biashara mnayoisema na hauna hela hivyo.

Nachomaanisha ni kuwa sahau kuhusu hizo pesa za Wadhamini ambazo zinatoka kwa mkupuo sio zote kwa pamoja, sahau kuhusu TV rights, sio rahisi kuendesha timu za mpira na zikapata matokeo, ukihitaji timu ipate matokeo lazima uende nje ya bajeti, huo ndio ukweli.

Kwa mwaka Simba bajeti yao ni BILLION 12, hiyo ni bajeti ya kwenye makaratasi tu tena ya timu moja ya Kiume, hujataja Simba Queens na timu za vijana, can you imagine? Hizo pesa zinatoka wapi?

Ni rahisi sana kumwondoa MO kwenye equation kwasababu zenu binafsi ila mpira sio biashara duniani kote, FOOTBALL IS A PRESTIGIOUS GAME.

Screenshot_20220925-161541_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Siku moja Malkia Elizabeth alikuwa matembezini na Mlinzi wake mmoja tu Bwana Dick Griffin kwenye vilima karibu na Kasri la Balmoral huko nchini Scotland 󠁧󠁢󠁳󠁣󠁴󠁿.

Malkia alikuwa anapenda sana kutembea maeneo hayo kwakuwa ana Historia nayo kubwa sana ikiwemo kuchumbiwa hapo na Prince Phillip enzi za uhai wao, hivyo jioni hiyo ya 2005 alikuwa anatembea tu eneo hilo.

Ghafla mbele yake aliwaona wanandoa wawili wa Kimarekani ambao nao walifika eneo hilo kupata barizi kidogo na kutazama mandhari mazuri ya kasri la Balmoral, wale Wamarekani wakawasogelea Malkia na Mlinzi wake.

Inasemekana kwasababu za kiusalama kuna muda mwonekano wa Malkia ilikuwa ngumu kumtambua kidogo kama una haraka sana hiyo wale Wamarekani wakawasalimia wote wawili, Malkia na Mlinzi wake.

Kisha wao wakajitambulisha kuwa ni Watalii kutoka Marekani na wamekuja kula maisha lakini pia kuliona kidogo Kasri la Malkia, kisha yule Mwanaume akamuuliza Malkia Elizabeth bila kujua “Na wewe ni nani na hapa unafanya nini”

Malkia akajibu kwa utulivu tu kuwa yeye anaishi London na amekuja eneo hilo kwakuwa ana nyumba yake ya mapumziko, wala hakutaja kasri wanalolisifia wala hakusema kuwa yeye ni Malkia tazama picha juu ya picha.

Mmarekani akamuuliza tena, una muda gani tangu umeanza kuja hapa, Malkia akamjibu kwa usahihi kabisa kuwa ni zaidi ya miaka 70 kwakuwa ni eneo analolifahamu tangu mdogo, na ni kweli Eliza hapo anapajua vyema sana!

Kwakuwa wale Wamarekani walikuwa na shauku sana ya kumwona Malkia hata kwa mbali, Malkia akawaambia “Ila huyu wa pembeni yangu anafanya kazi kwa Malkia kwa muda mrefu sana”

Basi Wamarekani kusikia hivyo wakamsogelea Dick Griffin (Mlinzi wa Malkia) kisha wakampa Malkia camera na kumwambia “Tupige picha na Mlinzi wa Malkia” Malkia akawapiga picha vizuri tu ila Mlinzi wake akawaambia haya nanyi pigeni na Bibi yangu, wakapiga nae pia, kisha wakaaga na kuondoka.

Malkia akamtazama Mlinzi wake baada ya wale kuondoka kisha akamwambia “Wakifika Marekani watafahamu ukubwa wa ile picha ya mwisho” kisha akacheka na wakaendelea na matembezi yao Mlimani.

Kuna funzo kubwa sana hapa

Screenshot_20220925-161920_OGInsta%2B.jpg
 
UBORA WA AL HILAL
.
Chini ya kocha Florent Ibenge, Al Hilal imekuwa ikipendelea zaidi kushambulia kutokea pembeni mwa uwanja ikiwatumia zaidi mawinga hatari Mohamed Abdelrahman na Makabi Lilepo ambao wana kasi na uwezo mkubwa wa kupiga chenga na kumiliki mpira huku mshambuliaji wa kati wakipendelea kumtumia Waleed Bakhet.
.
Silaha yao kubwa ni kushambulia katika dakika zote za mchezo jambo ambalo limewafanya wawe na wastani mzuri wa kufunga bao katika kila mchezo.
.
Wachezaji tishio katika kikosi cha Al Hilal ni Lilepo, Abdelrahman, Claude Singone, Abdul Ajagun na Abdelrazig Omer.

…………………………
Screenshot_20220925-162111_Instagram%20Lite.jpg
 
DE AGOSTO MAKALI YAO
.
De Agosto ni timu yenye kundi kubwa la wachezaji wanaopenda kumiliki mpira kutokana na ufundi iliyonayo na imekuwa ikipendelea kupiga pasi nyingi fupifupi za harakaharaka pindi inapojenga mashambulizi.
.
Ni hatari katika kufunga kwa kutumia mipira ya krosi na mara nyingi imekuwa ikikabia wapinzani kuanzia mstari wa mbele, kwa lengo la kuwalazimisha wafanye makosa, kisha iwaadhibu.

…………………
Screenshot_20220925-162221_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom