Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais wa Burundi, Evariste Ndayishimiye amemfukuza kazi Waziri wake Mkuu, Jenerali Alain-Guillaume Bunyoni na mmoja wa watu wenye nguvu na ushawishi zaidi nchini humo, Gabriel Nizigama.

Ndayishimiye amewafukuza kazi wawili hao leo Jumatano Septemba 7, 2022 baada ya shutuma za jaribio la 'mapinduzi'
Screenshot_20220907-183142_OGInsta%2B.jpg
 
Maisha ya wakazi wa Jiji la Dar es Salaam yameendelea kukumbwa na wasiwasi, baada ya vikundi vya uhalifu maarufu Panya Road kurudi tena na kuvamia nyumba 24 za wapangaji wa mtaa wa Kabaga Kinyerezi kisha kuwajeruhi nakupora mali zao.

Kwa mujibu wa wananchi wa Kabaga wameeleza tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana Jumanne Septemba 06, 2022 saa 8 usiku katika maeneo hayo ambapo raia wanne wamejeruhiwa na kwa sasa wapo hospitali ya Amana wakipatiwa matibabu.

Hata hivyo, alipotafutwa Kaimu Kamanda wa Kanda hiyo, Wiliam Mkonda kujua uhalisia wake, amekiri kutokea kwa tukio hilo huku akieleza "Taarifa za tukio hilo nilisha zielezea toka jana."
Screenshot_20220907-183314_OGInsta%2B.jpg
 
Watu wawili wamefariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa katika kata ya Kwedizinga wilayani Handeni, Mkoa wa Tanga baada ya gari aina ya Toyota Hiace kuligonga lori.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa Tanga, Sofia Jongo amesema tukio lilitokea saa 12 asubuhi, leo Jumatano Septemba 7, 2022 ambapo hiace ilikuwa ikijaribu kupita lori eneo ambalo alama haziruhusu kupita hali ambayo dereva alishindwa na kuligonga lori hilo.

Amesema gari aina ya Toyota Hiace lilikuwa likijaribu kupita lori ambapo dereva alishindwa kasi na kujikuta analigonga lori hilo kwa nyuma, na kusababisha kifo cha dereva wa Hiace na abiria wake mwingine.

Rip Mtana jamani tutakumbuka tu kwa ucheshi wako na vituko vyako Mungu aitie nguvu familia yako
Screenshot_20220907-183411_OGInsta%2B.jpg
 
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mussa Azzan Zungu amekutana na kufanya mazungumzo na Spika wa Bunge la Wawakilishi la Ufalme wa Morocco (House of Representatives), Rachid Talbi EL Alami jijini Rabat, Morocco.

Zungu ambaye yupo nchini Morocco kwa ziara ya kikazi ya siku tano, katika mazungumzo hayo wamejadili kuimarisha uhusiano wa kibunge na kiuchumi kati ya mataifa hayo mawili.

Pia, Zungu amefanya mazungumzo na Rais wa Bunge la Councilors (House of Councilors), Naam Miyara pamoja na Waziri wa Kilimo, Uvuvi, Maendeleo ya Vijijini na Misitu wa Morocco, Profesa Mohammed Sadiki.

Screenshot_20220907-183549_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi nchini limeanza kuchunguza tuhuma za maofisa wa jeshi hilo kutumia mafuta ya umma kujaza katika magari binafsi zikiwamo daladala.

Uchunguzi huo umeanza ikiwa ni takribani siku sita zimepita tangu Rais Samia Suluhu Hassan kuonya matumizi mabaya ya mafuta kwa jeshi hilo, akisema yamekuwa yakitumika kinyume na makusudio.

Rais Samia alisema hayo Agosti 30, mwaka huu wakati akifungua kikao kazi cha maofisa wakuu wa polisi na makamanda wa mikoa mkoani Kilimanjaro.

Jana, Mwananchi ilizungumza na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Ramadhan Kingai, aliyesema uchunguzi umeanza.
Screenshot_20220907-183643_OGInsta%2B.jpg
 
Meneja wa Kisinda, Nestor Mutuale ameliambia Mwanaspoti kwa njia ya simu akiwa DR Congo kwamba amesikiliza sakata hilo na kugundua ni siasa za soka la Tanzania.

Mutuale alisema kitu pekee ambacho kingemzuia Kisinda kuichezea Yanga kwa sasa ni hati yake ya uhamisho wa Kimataifa (ITC) ambayo amelihakikishia Mwanaspoti tayari ipo pale makao makuu ya TFF.

Meneja huyo alikiri kutokana na kanuni za ndani za TFF, Yanga inapaswa kumuondoa mchezaji mmoja ambaye alishaanza kusajiliwa changamoto ambayo inaweza kumalizwa kwa Yanga kukaa mezani na mamlaka hiyo ya soka hapa nchini. “Nimeona hilo sakata lakini naona ni siasa za soka hapo Tanzania, hata wachezaji wangu wamekuwa wakiniambia na nimekuwa nikiona TFF haiko sawa na Yanga iko siku watasababisha matatizo makubwa kwa Tanzania,” alisema.

“Hilo tatizo linatakiwa Yanga kukaa pamoja na TFF kuangalia maslahi ya mpira wa Tanzania na sio kuharibu kwa kuzuia mchezaji asicheze,FIFA haina shida ndio maana ikatoa ITC kilichobaki Kisinda kucheza ni mambo yenu ya ndani.
Screenshot_20220907-183903_OGInsta%2B.jpg
 
Katika hali inayoonyesha vita vya kampuni za uwindaji nchini, Serikali imeingia katika lawama ya upotevu wa mapato na kuzisababishia hasara kampuni sita zilizoshinda zabuni ya uwindaji kwa wenyeji na wageni wakazi iliyoendeshwa Agosti, 2021.

Taarifa ilizozipata Mwananchi zinaonyesha kampuni zilizoshinda zabuni hiyo ni pamoja na A Class Hunting and Safari Limited iliyoshinda katika kitalu cha Talamai (Manyara), Nundu Hunting Safari iliyoshinda kitalu cha Kisarawe (Pwani), Monster Daggaboy hunting Ltd iliyoshinda kitalu cha Simbanguru Igwamadete (Singida).

Nyingine ni Mbogo Wild Meat Butcher iliyoshinda kitalu cha Matundu Forest (Morogoro), Suleiman Masoud Suleiman aliyeshinda katika kitalu cha Kilwa (Lindi) na kampuni ya Jungle Butcher iliyoshinda kitalu cha Ipemba Mpezi (Tabora).

Hata hivyo, licha ya kampuni hizo kushinda na kulipia ada ya Sh282.50 milioni, hazikupewa zabuni hiyo baada ya kampuni ya Tachaco Hunting Safari Group Ltd – (TACHA) kulalamika kuwa mnada huo uliingiliwa, kudukuliwa na kwamba haukuwa wazi wala huru.

Akizungumza na Mwananchi kwa niaba ya kampuni hizo, Murugenzi Mkuu wa A Class Hunting and Safaris Limited, Japhari Mohamed alimtaja aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Damas Ndumbaro (sasa Waziri wa Katiba na Sheria) kuwa ndiye aliyesimamisha mnada huo kinyume na utaratibu.

Mwananchi lilimpomtafuta Waziri Ndumbaro kwa simu alisema suala hilo iiulizwe Wizara ya Maliasili na Utalii.
Alipotafutwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Pindi Chana alimtaka mwandishi kumtafuta Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Eliamani Sedoyeka, ambaye alikiri kuwepo ucheleweshwaji wa suala hilo na kuwa tayari kampuni hizo zimeshajulishwa.
Screenshot_20220907-184036_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amempongeza Waziri Mkuu mpya wa Uingereza na kiongozi wa Conservative, Liz Truss.

Liz Truss au kama lilivyo jina lake kamili, Mary Elizabeth Truss (47) aliyechaguliwa juzi Jumatatu Septemba 5, 2022 anakuwa Waziri Mkuu wa tatu mwanamke katika historia ya Uingereza baada ya Margaret Thatcher na Theresa May (65).

Katika salamu zake za pongezi kupitia mtandao wake wa Twitter leo Jumatano Septemba 7, 2022, Rais Samia amesema “Natoa pongezi zangu za dhati kwa mheshimiwa Liz Truss kwa kuwa Kiongozi mpya wa chama cha Conservative na Waziri Mkuu wa Uingereza.

Tanzania inatarajia kuendeleza urafiki wake wa muda mrefu na Uingereza katika kukuza uhusiano wetu wa kiuchumi na kidiplomasia.”

Kiongozi huyo mpya anachukua nafasi ya Boris Johnson ambaye jana Jumanne, Septemba 6, 2022 aliwasilisha barua ya kujiuzulu uwaziri mkuu kwa Malkia Elizabeth II (96) huko kwenye kasri ya Balmoral iliyopo Scotland na nafasi hiyo kukabidhiwa kwa Waziri Mkuu Liz Truss.
Screenshot_20220907-184131_OGInsta%2B.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, imemhukumu mkazi wa Kijiji cha Dongo, wilayani humo, Yeremia Chidaka (60), kifungo cha miaka 30 jela baada ya kumkutia hatiani kwa kuzini na mwanawe wa kumzaa mwenyewe miaka 16.

Hukumu hiyo imetolea na Hakimu Mkazi Mosi Sasy leo Jumatano, Septemba 7, 2022 baada ya mtuhumiwa huyo kukiri kosa akisema hataki kuisumbua mahakama kwa kuwa aliamua kuzini na mtoto wake mwenyewe hakutaka aolewe na mtu ambaye alimwona na mahusiano naye ya karibu.

Alidai amlipomuuliza mke wake kuhusu wazo la kutaka mtoto wao asiolewe, mwanamke huyo alimweleza kwa dhihaka kama hutaki aolewe na Wakamba amuoe yeye mwenyewe jambo ambalo aliamua kuzini naye hadi alipompa ujauzito.

Alipotakiwa kujitetea, Chidaka aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa shetani alimpitia kutenda kosa hilo.

Mwendesha Mashtaka wa Polisi Mahakamani hapo, Wilfred Mollel akisema Jeshi la Polisi halina taarifa kama mthumiwa huyo aliwahi kufanya kosa lingine na kumwomba hakimu kumpa adhabu inayostahili.
Screenshot_20220907-192416_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amewataka Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI kutoacha kutumia dawa za kufubaza virusi vya ugonjwa huo (ARVs) na pia kusitisha ngono zembe kutokana na kasi ya maambukizi iliyopo kwa sasa.

Waziri Ummy amesema kumekuwa na kusuasua Kwa matumizi ya dawa za ARVs Kwa Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI jambo ambalo ni la hatari.

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Wananchi katika kituo Cha Afya Disunyara Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha alipofanya ziara ya siku Moja akiambatana na Mkurugenzi wa Mfuko wa Kimataifa wa kusaidia mapambano dhidi ya HIV, kifua kikuu (TB) na malaria (Global Fund), Peter Sand.

"Katika Watu 100 Tanzania wanaoishi na Virusi vya UKIMWI, 95 wanatumia dawa tumeona kusuasua Kwa matumizi ya ARVs kwasababu Watu wanaacha kutumia dawa”

"Wakati tunakaribia kuushinda UKIMWI tunaanza kurudi nyuma hata kama huumwi unaona vimepungua usiache kutumia dawa"
Screenshot_20220907-192529_OGInsta%2B.jpg
 
Taarifa zinasema kuwa kwenye simu ya dakika 10 kati ya Kocha Tuchel na Wamiliki ni kuwa aliomba nafasi ya pili kikosini hapo ila Maboss hawakuwa tayari na hawajaridhishwa na mwenendo wake.

Baadhi ya taarifa zinasema alipoteza mahusiano mazuri na Wamiliki baada tu ya kukataa kuidhinisha usajili wa Cristiano Ronaldo wakati wao walishakubaliana kila kitu na nyota huyo.
Screenshot_20220907-193326_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Kutoa namba ya mtu bila idhini yake ni kosa kisheria, kutuma picha ya mtu sehemu bila idhini yake ni kosa kisheria lakini tunaishi kwenye jamii ya kustiriana na kusikilizana licha ya uwepo wa sheria.

Sheria inatisha sana na wengi tungekuwa magereza leo hii kama kila kitu kingefuata misingi yake, sheria na kanuni ni msumeno ambao unakata kote kote bila kujali.

Uliwahi kutokea mzozo mkubwa sana kati ya LA LIGA na miamba miwili ya Hispania yaani Real Madrid na Barcelona, walipingana juu ya vitu vingi sana na siti ya Javier Tebas ilikuwa ya moto sana.

LA LIGA walitumia sana mabavu na kutotaka kuelewana na miamba hii miwili lakini ikatokea siku walihitaji sana ushiriki wa Real Madrid na Barcelona haswa kwenye suala la kuuzwa kwa maudhui ya ligi hiyo.

Ndipo hapo Tebas aligundua ulazima wa mahusiano mazuri na kusikilizana kwakuwa sheria na kanuni ni ngumu mno ukizifuatisha nukta kwa nukta, zinatisha sana sana, walikaa chini na kumaliza tofauti zao.

Niwarejeshe nyuma kidogo kuhusu tukio la mechi ile ya Simba na Yanga ambapo haikuchezwa kwasababu mmoja alifuata sheria na utaratibu lakini ilipaswa kutumika busara eneo lile, nawakumbusha sana suala la busara.

Mpaka ile mechi kurudiwa ilikuwa busara tu, ingetokea sheria imesimamiwa?? Maana yake mechi isingechezwa, narudia kuwa sheria na kanuni ni ngumu mno tukisema tuzifuate nukta kwa nukta.

FIFA licha ya sheria zao ngumu sana na misimamo yao lakini wanasema MCHEZAJI ANAPASWA KUCHEZA MPIRA ili alinde kiwango chake, kwakuwa wanajua sheria ni ngumu mno ukifuatisha kila kitu.

Niombe tu Yanga na TFF busara iwaongoze katika hili, what goes around comes around, Nawapenda sana Ndugu zangu, hakuna bingwa kwenye sheria na hakuna ukubwa kwenye busara

Screenshot_20220907-193718_OGInsta%2B.jpg
 
Farhan Jr

Niliandika kuhusu BUSARA lakini sikueleweka, ni ngumu kueleweka kwakuwa watu wanasahau mapema sana kuhusu ‘hatari’ ya sheria hata Hakimu anaiogopa sana.

Mmewahi kufikiria japo kwa uchache wakati Simba anagomea kuvaa nembo ya Mdhamini, kama TFF wangetumia hiyo sheria ingekuwaje? Sheria inatisha sana, haifai hata kuifuata kwa 100%.

Nilitegemea BUSARA mbili zitumike kwa TFF kwanza, ndio ni jukumu Mama la TFF kuomba ITC lakini kama Mwanao Yanga alikuwa nje ya muda wewe kama Baba kwanini hukumwambia mapema? Msahihishe ni Mwanao wa kumzaa.

Yaani Mwanao anataka kuoa na unafahamu ana wake wanne tayari, anakuja kuomba ridhaa ya kwenda kuoa utakubali aende bila kumuelimisha kuwa haiwezekani? Mpe elimu

BUSARA ya pili kwa TFF huyo Yanga ni mtoto wako kuhusu hilo sakata kuna Kiongozi yoyote wa Yanga (Anayetambulika) alizungumzia kwenye media? Mna njia zenu za mawasiliano na shauri lipo kwenye kamati kwanini msingesubiri kutoa taarifa baada ya kamati?

Naomba kidogo leo niwape ukubwa wa neno busara, naomba sote tukasome andiko moja na anaetaka nimtumie link “How LaLiga economic controls go beyond Financial Fair Play” lina madini sana.

Hii ni baada tu ya Financial Fair Play kutambulishwa Ulaya, LA LIGA wakakaa na klabu zao zote kuona namna gani hii sheria haiwaumizi na kuhakikisha klabu zao zinafanya vyema, tumeelewana?.

Alisimama Jose Guerra ambaye ni Cooperate General Director wa LA LIGA alisema kuna vitu havipo kwenye FFP tutaviongeza lakini walilegeza baadhi ya vifungu na ndio maana Barcelona kasajili sana licha ya kuanguka kiuchumi, ni kifungu hicho.

Wenzetu klabu zao kwanza na wanazilinda kivyovyote vile, wanatumia sana busara kwenye sheria kwakuwa wanajua wazi wakisimama hapo hakuna aliye salama eneo hilo.

Ni ngumu kueleweka ila makaratasi yapo ila kwa ground hayatumiki sana, Chelsea, Leicester na Man City walipaswa kupigwa rungu la FFP, mnaelewa kilichotokea? PENDANENI BABA NA MTOTO WAKO!

Screenshot_20220907-193718_OGInsta%2B.jpg
 
Erling Haaland ameweka kambani au ametoa assists katika KILA mechi ya EPL na Champions League amecheza akiwa na Manchester City:
.
vs. West Ham
vs. Bournemouth
vs. Newcastle
vs. Palace
vs. Forest
vs. Villa
vs. Sevilla
.
Ni JINI.
Screenshot_20220907-194754_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom