Makapuku Forum

Makapuku Forum

AUBA AVAMIWA, ATISHIWA NYUMBANI KWAKE
.
Watu waliokuwa na silaha walimvamia na kumpiga straika wa Barcelona, Pierre Emerick Aubameyang baada ya kuvunja na kuingia nyumbani kwake.
.
Wezi hao wasiopungua wanne walipanda uzio wa bustani wa nyumba ya Aubameyang huko Castelldefels na kufanya uharifu huo. Aubameyang, 33, alitishiwa bunduki na nondo na alipigwa kidogo kwa mujibu wa taarifa ya polisi. Wezi hao walimtishia maisha mke wa Aubameyang, mrembo Alysha Behague, kwa silaha kali hadi kuwafungulia sefu.
.
Vito kadhaa vya thamani viliibwa nyumbani hapo na watu hao wanne waliondoka na gari aina ya Audi A3 yenye rangi nyeupe. Polisi wa Catalunya kwa sasa wapo kwenye msako wa kuwatafuta wote waliohusika kwenye tukio hilo la kiharifu.
Screenshot_20220830-074950_OGInsta%2B.jpg
 
RONALDO ATAFUTIWA NAFASI CHELSEA
.
Supastaa, Cristiano Ronaldo anaweza kujiunga na Chelsea ndani ya dirisha hili baada ya wakala wake, Jorge Mendes akiripotiwa kurejea kuzungumza na mabosi wa Stamford Bridge ili mteja wake akakipige huko.
.
Kocha Tuchel matumaini yake yalikuwa kuungana tena na Aubamaeyang baada ya kufanya naye kazi Borussia Dortmund. Lakini, shida imetokea sehemu moja tu, Chelsea inataka kumpa Auba mkataba wa mwaka mmoja, wakati mchezaji huyo ili akubali kwenda kukipiga Stamford Bridge anataka dili la miaka miwili.
.
Jambo hilo linatibua mpango na sasa wakala wa Ronaldo amerudi tena Chelsea na kuwataka wamsajili mteja wake, ambaye mipango yake ni kucheza kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu.

……………….
Screenshot_20220830-075318_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom