

Scandal24
FOOTBALL ECONOMY || Wana wa Uzao Wetu

.
Angalia picha ya kikosi cha Simba, hiyo picha ilipigwa 1.06.2003 pale Cairo Misri, angalia tena na kisha mwishoni utamuona Bishoo aliyesuka, hana papara na wakati huo unaweza kudhani ni moja ya mastaa wa Kinaijeria na ndiye aliyeongoza mapambano ya kuwatoa Zamaleki, kama humjui huyo ndiye SELEMAN ABDALLAH MATOLA.
.
Miaka zaidi ya 20, ameishi akiujua utamaduni wa wanasimba, ametumika kama Mchezaji, Nahodha na sasa kocha msaidizi, anaujua utamaduni wa klabu na bila shaka yeye ndiye mlizi sahihi wa mifumo na Utamaduni wa klabu ya Simba Kuonesha hayupo hapo bahati mbaya angalia wachezaji wangapi wamepita ila yeye Yupo.
.
Tumeamua kuishi kwenye kasumba ya Roho mbaya, tumeamua kuishi kwenye dunia ya kutoheshimiana kisa tunajuana. Wanaosema Matola afukuzwe hawana Hoja, hoja yao kubwa ni kwa nini wengine wote waondoke yeye abaki..? Haya ni matokeo ya roho mbaya na kasumba yetu ya kupenda aidha wote tukose au nipate yeye akose.
.
Wakati sisi tunawaza namna ya kuwaomba msamaha kina Mkwasa kwa kushindwa kuwaheshimu kuna hawa Vinaja wa SOSHO MEDIA wanaanza Dhambi mpya ya kuwadharau kina Matola. Leo kesho natamani Said Maulid akae Benchi la Yanga, natamani pale Costal Guardiola Mweusi aheshimiwe. Halafu wewe unakuja unamsema hovyo MZAWA.? UNANIUDHI.
.
Simba inafungwa kutokana na mipango ya Uongozi na sio uwepo wa Matola, Matola ni Moyo wa Simba ni alama ya Uzao na kumbukumbu nzuri ya Wana wa Msimbazi. Kashinda kila kitu kama kocha na kama mchezaji, kabla hujaongea basi kuwa na Heshima, Binafsi nampa #HeshimaFullTank

, Yeye ni Alama ya Utamaduni wa wanasimba.
.
VALUE THEM HOME BOYS

.
NB:
Tuishi Upendo, Tuishi Uzawa, Tujifunze kwa Wageni