

Farhan Jr
Nimeamka leo asubuhi na mapema sana, napokea simu kutoka Bibi zangu huko nyumbani Morogoro, wanasema usiku wa jana hawajalala wanasikia vishindo kutoka milima ya Uluguru, vishindo tena vikubwa
Wananiambia Machifu wameumia, Machifu wanaumizwa na kitukuu chao Tepsie Evance, Mababu na Mababu wanasema hapati kile anachostahili, licha ya kuufanya mpira uwe mchezo rahisi sana ila bado hapewi heshima
Napokea simu kutoka kwa Wazee wa mila kutoka Mto Kilombero na Ruaha wanasema jana usiku maji yalikauka yote mtoni, haiwezekani Tepsie amefunga na kuassist na kwenye kiwango bora sana ila Farhan hujaandika kitu, wamechukizwa
Sauti kutoka mto Kilombero zinasema “Mwambieni Farhan aandike kuhusu Tepsie, aandike ili Mdogo wake asijisikie mnyonge, mwambieni aandike kwakuwa sisi ndio tunampa huo utashi” Naam! @tepsie_59 asubuhi hii nakuandikia Fundi
Nitaandika sana bila kuchoka ila Mambuyi wa Wapogoro kule Epanko, Mbangayao na kilele cha mlima Ndororo wasichukie, nitaandika kuhusu Mchawi huyu wa soka kutoka Morogoro, nitaandika bila kuchoka
Ghafla napokea simu kutoka safu za milima ya Udzungwa naambiwa maporomoko ya Sanje jana yalikauka, naambiwa chura wa Kihansi pale Mlimba walipotea, ni adhabu tumepigwa kwakuwa sijaandika kuhusu Tepsie
Nawaahidi Mababu zangu na Bibi zangu hapo Morogoro kuanzia Mbuga, Ulanga mpaka Kinole Morogoro! Nitaandika na sitoacha, Tepsie atarudi nyumbani kama Legend siku moja na mimi nitarudi nyumbani kama Ngugi siku moja ni ahadi
Babu na Bibi zangu msishushe laana kwenye kizazi hiki, tuendelee kuwapa pongezi @morokidsacademy @mtibwaofficial @moroathleticsacademy na Kilombero Soccernet, baraka na neema ziendelee
Fundi sana anaitwa TEPSIE EXCELLENCE oooh sorry! TEPSIE EVANCE

All the best Homeboy @tepsie_59