Makapuku Forum

Makapuku Forum

Aliyekuwa kipa wa Yanga, Ramadhani Kabwili yupo nchini Rwanda kukamilisha taratibu za kujiunga na Rayon Sports ya nchini humo.

Kabwili leo, atasaini mkataba wa mwaka mmoja na Rayon na kesho huenda akatambulishwa kama mchezaji mpya wa kikosi hicho.

Kipa huyo baada ya kutemwa Yanga sasa ni mchezaji huru.

Screenshot_20220818-034807_OGInsta%2B.jpg
 
Wachezaji wapya Simba wameanza Ligi Kuu NBC kwa kishindo baada ya kuisaidia timu yao kupata ushindi wa 3-0 dhidi ya Geita Gold kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.
Wachezaji Mosses Phiri na Augustine Okra wakiwa ndio mchezo wa kwanza kwenye ligi wameifungia Simba mabao mawili ya uongozi huku bao la tatu likifungwa na Chama kwa mkwaju wa Penalti baada ya Okra kuchezewa rafu eneo la hatari.
Kwa ushindi huo Simba ilioupata kwenye mchezo wake wa kwanza wa Ligi umeifanya kuzishusha Mbeya City na Yanga kwenye kilele cha msimamo kwa idadi ya mabao.

FT: Simba 3-0 Geita Gold
' Okrah
️' Phiri
' Chama (P).
Screenshot_20220818-034921_OGInsta%2B.jpg
 
Golkipa namba moja wa Simba, Aishi Manula amerudi uwanjani baada ya kutoonekana kwenye mechi kadhaa za timu hiyo kutokana na majeruhi aliyopata akitumikia timu ya taifa.

Simba ilikua inamtumia golkipa namba mbili, Beno Kakolanya katika mechi za Pre-Season, na hata mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga waliyopoteza kwa mabao 2-1.
Screenshot_20220818-035026_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa amekutana na Watendaji Wakuu wa Klabu za Ligi Kuu ya NBC Simba, Yanga, Azam FC na Ruvu Shooting kujadili mambo mbalimbali ikiwemo namna bora ya ushindani, kuzingatia weledi, nidhamu na maadili.
Screenshot_20220818-035121_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220818-035143_OGInsta%2B.jpg
Screenshot_20220818-035158_OGInsta%2B.jpg
 
Khalid Chukuchu

Three points , with 3 Goals , Three Point Sealed and Delivery to Msimbazi .

Nimeutaza mchezo kwa Uzuri sana na Leo mwalim Maki alifanikiwa sana nje ya uwanja , “ research “ juu ya Ubora wa Geita Gold , Ubora wa Kelvin Yondani akutaka mchezo mchezo uchezwe ndani aliwaekea kina Sakho na Banda pembeni lengo ni kuua muundo wa Kuzuia wa Geita alifaniokiwa Mikimbio ya Banda ilimpa wakati mgumu Datus Peter Yondan akawa anatamani kwenda kumkaba akaawa anaacha Nafasi kwa Phiri kucheza mwisho siku wakafanikiwa .

Nimependa mechi kati ya uwanja Okoyo , Kagoma , Nashon waliwauliza maswali magumu kina Mkude walifanya vitu kwa hataka Energy yao ikamshinda Kabisa Mkude , Maki akaona nafasi ya Okrah sababu ya kuvunja mid Block system ya Geita , Pace na Mikimbio ya Okrah “ Unbelievable ” alikimbia kulia , Kushoto , Kati mwisho kabisa akaitoa Geita kwenye muundo wa Kuzuia .

Kuna Shida moja nimeona , inawezekana Dejan ajajua mijongeo ya viungo wa Simba sc au Viungo hawajua Movement za Dejen ila Jamaa anajua mpira “ Pressing , Movement , jamaa anaitaji muda tu .

Yusufu Kagoma the Man is Baller ️, uwezo wake wa kupiga pasi ni wajuu sana , Mtulivu , na anajua kusoma mchezo .

Wonder Kid Peter Banda is phenomenon , anafanya kila kitu kwa usahihi , Take ons zake ni za Hatari kuliko za Sakho nzuri zaidi namna anavyoweza kushambulia” Half Space “

Simba sc wanakwenda Kileleni mwa Msimo wa NBC

Chama Ana Class

Screenshot_20220818-035432_OGInsta%2B.jpg
 
MSIKIE ULIMBOKA kuhusu Mzunguuuu!!
.
Mchezaji wa zamani Simba, Ulimboka Mwakingwe anasema Dejan ni mmoja wa washambuliaji wazuri ila amecheza mechi mbili zilizokuwa na ushindani mkubwa na uhitaji wa matokeo mazuri.
.
“Nimeona mikimbio yake na aina yake ya kucheza ni moja ya mastraika wanaopenda kuwekewa pasi kwenye njia na kufunga kama itatokea kuna kiungo wa Simba akamjulia katika hilo atafanya vizuri,” anasema Ulimboka.

……………
Screenshot_20220818-035927_OGInsta%2B.jpg
 
Ingawa Nabi ameonyesha tamaa ya kumtaka Fredericko Dario tayari Yanga imeshakamilisha idadi ya wachezaji 12 wa Kigeni wanaohitajika Kikanuni na kama akimpata atalazimika kumpunguza mchezaji mmoja.

……………
Screenshot_20220818-040032_OGInsta%2B.jpg
 
MMESIKIA?? Ronaldo Ruksa Kuondoka
.
Kocha wa Manchester United, Erik ten Hag ameripotiwa kutoa ruhusa ya kuuzwa kwa staa wa timu hiyo na Ureno, Cristiano Ronaldo, 37, katika dirisha hili.
.
Ronaldo mkataba wake wa sasa unatarajiwa kumalizika mwisho wa msimu huu. Staa huyu amekuwa akihitaji kuondoka kwa muda sasa.

………….
Screenshot_20220818-040633_OGInsta%2B.jpg
 
KLOPP: SI BURE TUNAROGWA
.
Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp amesema kwa utani kwamba wachezaji wake wanarogwa walipopata sare dhidi ya Crystal Palace katika mchezo wa Ligi Kuu England uliofanyika juzi Jumatatu.
.
Liverpool imekuwa ikiandamwa na majeruhi wengi msimu huu ambapo ilikosa mastaa wake kadhaa kwenye uteuzi wa kikosi chao kilichomenyana na Crystal Palace.
.
“Hii wiki hatari sana. Nimeshuhudia wiki nyingi zaidi hii, lakini naweza kusema kuna mchawi kwenye hili jengo. Ona, kila siku kuna mtu anashindwa kufanya mazoezi kwa sababu zisizoeleweka kabisa,” alisema Klopp.

…………….
Screenshot_20220818-040729_OGInsta%2B.jpg
 
JUST IN: Staa wa Barcelona Memphis Depay, 28, na Uholanzi yupo tayari kuvunja mkataba na Barcelona ili kukamilisha uhamisho wake wa kujiunga na Juventus katika dirisha hili. Mkataba wake unatarajiwa kumalizika mwakani.
Screenshot_20220818-040817_OGInsta%2B.jpg
 
Mambo 10 nilioyaona SIMBA vs GEITA

1: POINTI 3. MABAO 3 .. CLEAN SHEET SIMBA ARE BAAACK Ushindi wenye Faida kubwa kwenye kujenga hali ya kujiamini kwenye kikosi..

2: ZORAN ni kama alisubiri kuiona Geita mpya inavyofanana. Alivyowaona, akawasha Taa Nyekundu. ‘SUB’ iliyobadili mchezo ni ile ya Mkude kuingia OKRAH.. Kwanini?

3: Geita walikuwa na mpango wa kuzuia kwenye Mid Block wakiwa kwenye umbo la 4-4-2 .. Lakini baadae wakabadili kwenda kwenye Low Block [Kukabia chini] .. Hapa ndipo Zoran aliporusha karata yake kwa kuleta mtu anayeweza kutembea na mpira na sio kupiga pasi

4: OKRAH ana uwezo mkubwa wa kuficha mpira akikimbia. Kasi yake ilikuwa silaha ya kuivunja Line ya 2 ya ulinzi ya Geita kuvamia eneo la Tatu la mwisho la uwanja.. Mkude & Chama Simba ilipiga pasi.. OKRAH AKALETA KASI

5: Sub ya Okrah ni kama ilipeleka ujumbe kwa Minziro kuwa sasa mchezo uko wazi. Simba katikati wana kiungo mmoja tu mwenye uwezo wa kukaba.. Kanoute pekee. Nini alifanya Minziro?

6: Akadandia mtumbwi wa vibwengo! Akamtoa Okoyo na kumleta Chikola. Geita nao wakaufungua mchezo! QUALITY IKATAKIWA KUAMUA MCHEZO! Faida ikawa kwa Simba hapa

7: CHAMA.. WHAT A PLAYER Ile ni Sanaa ya Soka. Mpira uko kichwani mwake, mguuni ni maamuzi Kwenye nusu nafasi bado anaweza kunusa hatari kwa mpinzani.. ASISTI YA KWANZA MSIMU HUU

8: GEORGE MPOLE & LYANGA walipoteza ‘Link’ yao! Walicheza kwa presha kubwa na kushindwa kutumia Faida ya Edmund John uwanjani.. Henock alipovutika upande wa kushoto wa Geita, Mpole na Lyanga walitakiwa kuiona hio kama faida kwa kutengeneza movements nyuma yake

9: PETER BANDA anajua boli. Nimependa pia jituhada za Sakho.. Rudi tena litazame bao la Phiri.. Utaona rahisi namna alivyofunga Lakini ile Movement aliyoifanya inakupa jibu ni mtu hatari kiasi gani

10: Kelvin Nashon Kipa wa Geita anatakiwa kuongeza umakini zaidi.. Mechi kubwa huwa zinaamuliwa na details ndogondogo sana!

Nb: Chama mmoja ni sawa na ……
Screenshot_20220818-041143_OGInsta%2B.jpg
 
Imeandikwa na @swalehmawele

FT: Simba SC 3-0 Geita Gold

Bila shaka ni ushindi muhimu sana kwa Simba ili kujenga saikolojia ya ushindi katika akili za wachezaji, leo substitution moja ya kocha Zoran Maki ilikuja kubadilisha taswira ya uchezaji kwa Simba katika eneo la mwisho na kuanzia hapo mambo yakaanza kuwa mazuri upande wao, kivipi?.

Simba ilitengeneza shape ya 4-1-3-2 wakati ambao wanatengeneza mashambulizi, kocha alianza na Jonas Mkude kama kiungo wa kati mshambuliaji mbele ya Sadio Kanoute, Mkude alisogea katika mstari wa viungo watatu katikati ya Pape Sakho na Peter Banda na kuifanya timu iwe na 3-2 katika eneo ambalo Geita Gold wanazuia zaidi.

Hapa lengo lilikuwa ni kuifanya timu iwe na wachezaji wengi ambao wana akili ya kushambulia zaidi ( creating overloads with offensive minded players ), ni kama walitaka kuizunguka safu ya ulinzi ya Geita Gold kwa kuwa na wachezaji wawili nyuma yao ( Chama & Phiri ) na kuwa na wachezaji watatu mbele yao ( Mkude, Banda & Sakho ).

Wapi Simba ilifeli? ni katika usahihi wa Jonas Mkude katika kupiga pasi, pasi nyingi za Mkude zilikuwa ni square, hakuwa na ujasiri wa kupiga pasi ambazo zingeifunga difense line ya Geita Gold kutokea chini ( penetration passes ) na pia hakukuwa na mikimbio sahihi ambayo ingeitanua safu ya ulinzi ya Geita Gold ambayo ilikaba katika low block.

Geita Gold wamepoteza mechi ambayo walionyesha ujasiri na usahihi katika transitions zao, katika system ya 4-4-2, waliuharakisha mpira kupita kwenye eneo la kiungo ( midfield zone ) ili kuzikwepa pressing na 1 v 1 kwa wachezaji wa Simba, walifanikiwa lakini tatizo likawa katika ujasiri wa kuifunga back line ya Simba chini ya kamanda Mohammed Ouattara.

Nikivaa viatu vya Dejan naiona presha kubwa, kuna kitu anataka kitokee lakini mara nyingi hapokei pasi sahihi, eneo la ushambuliaji utaulizwa kuhusu magoli.
Kuna maswali magumu kama Zoran ataendelea kutumia double ten ya Chama na Okrah, Chama anatuliza timu na Okrah anaifanya ikimbie, kuna aina mbili hapo za kutengeneza mashambulizi.

Yule Yusuph Kagoma mtu, Yahya Mbegu kama juzi kama jana.
Nafikiri Geita Gold hawakucheza vibaya sana, kilichokuja kuamua ni quality.
Screenshot_20220818-035432_OGInsta%2B.jpg
 
Kutana na Kinyozi Julius Muchoki maarufu kama Julius the Axe Man kutoka Mji wa Kiambu nchini Kenya ambaye ananyoa Watu nywele kwa kutumia shoka kwa zaidi ya miezi sita sasa.

Kwenye mahojiano yake maalum na @AyoTV_ ameeleza yote ikiwemo alivyoanza, anavyofanya, usalama kiafya na jinsi anavyoingiza pesa sasa hivi kuliko zamani.

Interview yake yote ipo kwenye Youtube ya millardayo au bonyeza link kwenye bio yangu ikupeleke moja kwa moja kuitazama.
Screenshot_20220818-041748_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Zambia Hakainde Hichilema amewataka Watumishi wa Serikali wanaotaka wapewe magari ya kifahari aina ya Toyota Land Cruiser VX kwa ajili ya kuyatumia kwenye kazi wasau hilo na kama wanaona yana umuhimu sana basi wajinunulie wao lakini sio kwa pesa za Serikali.

Hichilema amehoji “Kwanini mnatumia pesa kumnunulia Meya VX? hiyo pesa ya kumnunulia Meya VX inaweza kuweka vyoo katika masoko yote kwenye miji yenu, piteni katika mstari huo.... Meya bado anaweza kuendesha gari zuri kama vile Hilux double cabin sio lazima gari liwe VX, mkitaka kuendesha VX nunueni kwa pesa zenu”

Kwa upande mwingine Rais huyu ambaye hakutaka kupokea mshahara wa Urais kwa miezi nane akisema kilichomsukuma kuingia madarakani sio pesa bali uzalendo wa kuijenga Nchi yake, aliwataka pia Watumishi wa Serikali wanaotaka kuongezewa mishahara wafikirie Wananchi ambao wanateseka kabla ya kutaka nyongeza hiyo "Unapoona mshahara unaingia kwenye akaunti yako ya benki kumbuka ni Mama Mjane amenilipa mshahara huu kwa hiyo kabla ya kuomba nyongeza jiulize vipi kuhusu yule anayekulipa mshahara wako wa sasa? Mtoto wake anakaa chini darasani.” ——— Hakainde Hichilema.
Screenshot_20220818-041859_OGInsta%2B.jpg
 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ametatua mgogoro wa ardhi uliodumu kwa miaka mitatu katika eneo la Boko-Dovya, wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam baina ya Aloyce Mwasuka na Salutari Massawe.

Katika mgogoro huo unaohusisha viwanja namba 393, 395 na 370 kwenye kitalu G (Boko Dovya) vilivyoko njiapanda ya Mbweni, Massawe alijenga ukuta ambao ulikuwa unazuia matumizi ya barabara na hivyo kumfanya Mwasuka apitie kwa jirani yake Bi. Oliver Semuguruka (kiwanja na. 395) ili aweze kufika nyumbani kwake (kiwanja na. 393).

Akizungumza na Watendaji wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, watendaji wa Wilaya ya Kinondoni katika kikao alichokiitisha leo Jumatano, Agosti 17, 2022 ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na hatua aliyoichukua Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe ya kusimamia uvunjaji wa ukuta huo ili kupisha eneo la barabara.

“Ninakushukuru Mkuu wa Wilaya na timu yako kwa kuchukua hatua tangu jana ili kusimamia haki ya wananchi wasio na uwezo, haki ni ya kila mmoja, mwenye uwezo na asiye na uwezo. Ile barabara iboreshwe ili wananchi wote wanufaike”
Screenshot_20220818-041952_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi limemkamata Gamariel Swai (43) Mfanyabiashara na mkazi wa Mbezi kwa tuhuma za kuuza spea za magari zilizoibwa kwenye magari ya watu mbalimbali, duka lake lipo Mtaa wa Songea, Ilala.

Awali Jeshi la Polisi tarehe 23 Julai 2022 lilipokea taarifa ya wizi wa vifaa vya gari huko maeneo ya Kivule bombambili Ukonga ambapo Sifael Msemwa (38) mkazi wa Bombambili aliibiwa vifaa vya gari yake aliyokuwa ameiegesha nyumbani kwake aina ya Toyota Prado yenye usajili namba. T. 429 BKK ambavyo ni side mirror 03, power window 04, control box na betri la gari”

“Tarehe 15 Agosti 2022 baada ya upelelezi alikamatwa mtuhumiwa Gama Swai na katika upekuzi katika duka lake Namba 21 lililopo mtaa wa Songea, Ilala alikutwa na side mirror 02 na power window 04 zilizoibwa toka katika gari hilo Toyota Prado”

“Aidha vilikamatwa vifaa vingine mbalimbali vya magari dukani hapo vinavyodhaniwa kuwa ni vya wizi kutokana na kutokuwepo na maelezo ya kutosha kuhusiana na vifaa hivyo”

“Taa za mbele 93 za magari ya aina mbalimbali, taa za nyuma 130 za magari ya aina mbalimbali, power window 189 za magari ya aina mbalimbali, side mirror 62 za magari ya aina mbalimbali, show za mbele za magari 07 mbalimbali, show za ndani za magari 35 za aina mbalimbali, mikono ya milango (vitasa) 26 za magari, rejeta 01 na betri moja”
Screenshot_20220818-042042_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi limemkamata Gamariel Swai (43) Mfanyabiashara na mkazi wa Mbezi kwa tuhuma za kuuza spea za magari zilizoibwa kwenye magari ya watu mbalimbali, duka lake lipo Mtaa wa Songea, Ilala.

Awali Jeshi la Polisi tarehe 23 Julai 2022 lilipokea taarifa ya wizi wa vifaa vya gari huko maeneo ya Kivule bombambili Ukonga ambapo Sifael Msemwa (38) mkazi wa Bombambili aliibiwa vifaa vya gari yake aliyokuwa ameiegesha nyumbani kwake aina ya Toyota Prado yenye usajili namba. T. 429 BKK ambavyo ni side mirror 03, power window 04, control box na betri la gari”

“Tarehe 15 Agosti 2022 baada ya upelelezi alikamatwa mtuhumiwa Gama Swai na katika upekuzi katika duka lake Namba 21 lililopo mtaa wa Songea, Ilala alikutwa na side mirror 02 na power window 04 zilizoibwa toka katika gari hilo Toyota Prado”

“Aidha vilikamatwa vifaa vingine mbalimbali vya magari dukani hapo vinavyodhaniwa kuwa ni vya wizi kutokana na kutokuwepo na maelezo ya kutosha kuhusiana na vifaa hivyo”

“Taa za mbele 93 za magari ya aina mbalimbali, taa za nyuma 130 za magari ya aina mbalimbali, power window 189 za magari ya aina mbalimbali, side mirror 62 za magari ya aina mbalimbali, show za mbele za magari 07 mbalimbali, show za ndani za magari 35 za aina mbalimbali, mikono ya milango (vitasa) 26 za magari, rejeta 01 na betri moja”
Screenshot_20220818-042042_OGInsta%2B.jpg
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam limemkamata Maarifa Hadith Matala (45), Dereva wa daladala, mkazi wa Kimara Suka Golani Wilaya ya Ubungo kwa tuhuma za mauaji ya mpenzi wake, Sharifa Twaha Nyamaishwa (31), Kondakta wa Daladala aliyekuwa mkazi wa Kimara Suka Golani Wilaya ya Ubungo kwa kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili na kumuua.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Muliro Jumanne amesema “Tukio hilo limetokea tarehe 16 Agosti 2022 huko maeneo ya Kimara Suka, na mara baada ya tukio hilo Mtuhumiwa alitoweka”

“Jeshi la Polisi baada ya kupata taarifa hiyo lilianza upelelezi na ufuatiliaji wa haraka na kufanikiwa kumkamata Mtuhumiwa Mkoani Lindi alipokuwa amejificha”

“Uchunguzi wa awali umebaini kuwa wapenzi hao walikuwa na migogoro inayosababishwa na wivu wa kimapenzi na kupelekea kugombana mara kwa mara, na mwili wa marehemu ulikutwa na majeraha, uchunguzi wa shauri hili unakamilishwa na Mtuhumiwa atafikishwa Mahakamani haraka iwezekanavyo baada ya tuhuma hizo za kikatili uliovuka kiwango”
Screenshot_20220818-042456_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom