
Fafhan Jr
Sheikh Ally ngoja tuongee kitu My Brother, tusiongee kama Mwandishi na Rais wa Yanga, bali tuongee kama Braza na mdogo wake, ngoja nikuelekeze kitu tena chepesi sana
Kama una kalamu hapo karibu basi andika jina la ANAS LAGHRARI moja kati ya vichwa na Mastermind nyuma ya European Superleague (siku moja nitaelezea, watu hawamfahamu kabisa) ana umri mdogo wa miaka 37 hii ndio Injini ya Perez, Rais wa Real Madrid ni watu wa karibu mno.
Jioni moja baada ya European Superleague kufeli, Kijana Laghrari wakati yupo na Perez kwenye mgahawa mmoja jijini Madrid akamuuliza “President tayari FIFA wamekugeuka, UEFA wamechukizwa na La Liga hawataki kukusikia, utaishije na timu yako?” Lilikuwa swali kwa Perez
Perez akapiga fundo moja kwanza la wine kisha akamwambia “Kijana wangu mdogo, hakuna kitu chochote ambacho FIFA au UEFA wanaweza kuipa Real Madrid na hakuna tatizo lolote mimi nisipokuwa karibu na wao” akaweka nukta kisha akaendelea
“Nachopaswa kukifanya kama Perez ni kuwekeza sana kwenye timu, kusajili vizuri na kubeba makombe na hiyo ndio njia pekee ya kuwakumbusha juu ya uwepo wangu na uwepo wa Real Madrid” akamaliza kisha akamtazama tena Laghrari
“Kwenye hii dunia ya mpira Kijana wangu kinachodumu ni mafanikio na historia, nitabeba makombe na kuweka historia, Rais wa FIFA atanipa mkono na Rais wa UEFA atanisalimia” akamaliza Rais Perez
Sheikh Ally umeipata hiyo historia? Umeelewa maana yangu? Well maana yangu ni kuwa una kazi mezani, una kazi ya kuhakikisha Yanga inazidi kuwa bora, endelea kubeba makombe, endelea kuonesha utofauti, watu watakuja mezani
Huu sio muda wa kulalamikia chochote, kujuta kwa chochote bali ni muda wa kuisuka upya ndoto ya Wananchi, kurekebisha panavuja na kuwapeleka Wananchi nchi ya ahadi, ndio jukumu ambalo unalo mikononi, ingia ofisini ongoza njia
In football its all about merit, you know the way Bro

GOD BLESS YOU