Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kikosi cha leo kwenye mchezo wa kirafiki.

Mchezo umesogezwa mbele kwa dakika 30. #FriendlyMatch #NguvuMoja
Screenshot_20220801-195055_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia amewaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu Dar es aalaam leo ambapo amesema “Nawashukuru walioacha nafasi zao mkaingia nyinyi, tunashukuru mchango wao kwa Taifa wameondoka kwasababu mbalimbali”

“Nawapongeza mlioapa kwa imani mliyopata kutoka Serikalini kwamba mnaungana na safu iliyopo katika kulitumikia Taifa, katika tisa mlioapa wawili ni Wanajeshi ambao wametakiwa kwao na jana niliwapandisha vyeo kuwa Mameja Jenerali kwahiyo wanakwenda kutumikia Jeshi ndio maana nikawachukua Makanali wawili wanakwenda kuwa Wakuu wa Mikoa na nafasi zao zitajazwa na Makanali wengine”

“Wengine saba wametoka kwasababu mbalimbali lakini wengine tutawatumia kwenye nafasi mbalimbali”
Screenshot_20220801-195848_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia amewaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu DSM leo ambapo amesema “Ninapofanya teuzi siangalii kabila la Mtu, rangi ya Mtu, anapotoka Mtu, naangalia sifa uwezo na uaminifu wake kwa Nchi na Serikali ndicho ninachoangalia”

“Katika teuzi hizi kama kuna Mtu hakuridhika kwa namna moja au nyingine yanayoniongoza ni hayo, siangalii makundi kwasababu Mimi pia sina kundi, nadhani mkijitazama mlioteuliwa kama mna makundi yenu mtajikuta kabisa kwamba mko mchanganyiko”

“Mimi nimechagua wenye uwezo ninaohisi watanisaidia, watakwenda kutumikia Watanzania, sasa Anko zetu wale ambao wamekasirishwa na hizi teuzi tunaomba tu watusamehe”

“Uteuzi huu sio mwisho bado tunaangalia utendaji wa tuliowaweka kwahiyo kama uliyeletewa hakuridhishi au hakufai bado tunaangalia utendaji wake na kama mzuri ataendelea kuwepo na kutumikia Taifa, kwahiyo nalofanya ni kuteua Watanzania ambao nahisi hawa tutasaidiana katika kuhudumia Wananchi, kuleta maendeleo katika Taifa hili sina vigezo vingine”
Screenshot_20220801-195948_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia amewaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu DSM leo ambapo amesema “Wakati mwingine unamlaumu Mtu hafanyi vizuri lakini tunajisahau na suala la mafunzo na ndio maana kuanzia kesho kuna mafunzo maalumu ya Wakuu wa Mikoa yatakuwa yanaendelea ili kukumbushana kama kuna popote tumesahu, hatuelewi au hatujui”

“Na Waziri Bashungwa nikuaguze sio kwa Wakuu wa Mikoa tu lakini wote watakaoteuliwa kwasababu tumefanya review ya makundi yote Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Makatibu Tawala wote kwahiyo wote tutegemee kuna mabadilio huko kwahiyo kila watakaoingia wafanyiwe mafunzo kama wanavyofanyiwa Wakuu wa Mikoa”

“Nikukumbushe Waziri Bashungwa umuhimu wa mafunzo kwa Watu wako hawa hata kama utafanya Kikanda, kwasababu kuwakusanya wote sehemu moja kwa siku nne tano huko nyuma kutakuwa hakuna Watu lakini kama utafanya kikanda ili wote wapate mafunzo na tuepuke visingizio”
Screenshot_20220801-200038_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia amewaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu DSM leo ambapo amesema ““Ukifanya vizuri Mungu anakunyanyua anakupeleka pazuri na ukifanya vibaya ipo siku utaadhirika, ipo siku ubaya wako utajulikana nendeni mkahudumie Watu, Mkuu wa Mkoa ndio Mkuu wa hilo eneo walioko hapo chini ndani ya eneo hilo ni wako nenda kawasimamie”

“Rais hana Rafiki kwahiyo na Mwakilishi wa Rais katika eneo lile asiwe na Rafiki, Rafiki yake ni yule anayeitumikia nchi, anayefanya kazi, anayetoa huduma kwa Wananchi huyo ndio Rafiki yako lakini kwenda kutengeneza Marafiki mkakaa huko choma nyama, piga maji halafu kazi kwa Wananchi haifanyiki, hiyo haikubaliki hatukuwateua mkafanye hayo”

“Kama Rais halali wewe usingizi unautoa wapi?, wewe usingizi unautoa wapi?, Mimi mnanitumia meseji saa nane/tisa usiku na ikiingia tu najibu hiyo maana yake kwamba sikulala, sasa wewe usingizi unautoa wapi?”
Screenshot_20220801-211608_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia amewaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu Dar es aalaam leo ambapo amesema “Twendeni tukahudumie Wananchi, Wananchi wanataka huduma zetu ndipo watajenga imani na nyinyi au na sisi pamoja na Mimi, sasa kama upo sehemu umeaminiwa umekaa lakini lengo lako Mimi sitofanya vizuri hapa kwasababu nikifanya vizuri sifa itakwenda ipo siku utaadhurika, tutakujua na utatupisha pembeni”

“Chalamila upo?, upo? wale wanaokuja na mabango sasa kawaambieni tena ‘andikeni tu’ yapo maneno gani nyie andikeni tu njooni nayo kesho, yakija mabango maana yake Wananchi wanalalamika na kama Wananchi wanalalamika wewe Mwananchi niliyekuamini kwenye hilo eneo hufanyi kazi yako”

“Mkisikia Wananchi wanakuja mapema mabango mnayakusanya mnayaweka huko mnawanyima Wananchi mdomo wa kusemea, kama hutaki mabango nenda kafanye kazi”
Screenshot_20220801-211735_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom