Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220801-182725_OGInsta%2B.jpg
 
WATANO WA STARS WAKWAMA
.
Kikosi cha Simba kitamaliza kambi yake Ismailia, Misri bila ya uwepo wa nyota wake watano waliokuwa katika kikosi cha Taifa Stars tangu wiki mbili zilizopita.
.
Kocha wa Simba, Zoran Maki amesema alitamani kuwaona wachezaji hao katika kambi hiyo ila kutokana na ratiba ya michezo ya timu ya taifa imekuwa vigumu kwake.
.
Zoran amesema ambacho anaamini kama mchezaji ameitwa katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi yoyote ile, basi huyo kuna kitu anacho.
Screenshot_20220801-182939_OGInsta%2B.jpg
 
NABI ANUKIA FAR RABAT
.
Yanga bado haijawapa mikataba mipya makocha wao, lakini kama kuna kitu kitawashtua basi ni ujio wa ofa moja kubwa kwa kocha mkuu Nasreddine Nabi ambaye kama hawatajiongeza dakika yoyote atayeyuka kutokana na fedha ndefu iliyowekwa na waarabu kutoka Morocco [emoji1173]
.
Taarifa za uhakika kutoka Morocco ni kwamba klabu ya AS FAR Rabat inasaka saini ya kocha huyo raia wa Tunisia [emoji1249] kwa nguvu kubwa akarithi mikoba ya kocha wa zamani wa Simba, Sven Vandenbroeck ambapo kwa sasa ametua Abha Club ya Saudi Arabia.
.
Yanga bado haijawapa mikataba Nabi na wasaidizi wake Cedric Kaze, Milton Nienov wa makipa na wengine katika benchi hilo ukiwa ni mtihani mkubwa wa Rais mpya wa Yanga Injinia Hersi Said.
Screenshot_20220801-183145_OGInsta%2B.jpg
 
Masikini! Mudathiri Bye Bye Azam
.
Taarifa kutoka Kambini Misri ni kwamba klabu ya Azam FC imeachana rasmi na kiungo wake wa muda mrefu, Mudathir Yahya Abbas.
.
Taarifa zaidi zinasema Muda anaungana na wachezaji wengine kama Charles Zulu, Paul Katema na Never Tigere kuagana na klabu hiyo.
.
Kuondoka kwa Mudathir kunahitimisha miaka zaidi ya kumi ya utumishi wake Chamazi.
Screenshot_20220801-183244_OGInsta%2B.jpg
 
Jina la Werner latua Newcastle
.
Newcastle United imeingia kwenye mazungumzo na mabosi wa Chelsea ili kuangalia uwezekano wa kuipata huduma ya straika wa timu hiyo na Ujerumani, Timo Werner, 26, kitika dirisha hili.
.
Huduma ya staa huyu pia inawindwa na RB Leipzig. Msimu huu amecheza mechi 31 za michuano yote, akafunga mabao 11 na kutoa asisti sita. Mkataba wa staa huyu unatarajiwa kumalizika mwaka 2025.
.
Chelsea imekuwa ikitaka kumuuza kwa sababu haonekani kuwa kwenye mipango ya kocha wa timu hiyo Thomas Tuchel.
Screenshot_20220801-183350_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578] Jemedari Said

THIS HAS NEVER HAPPENED BEFORE...!!

Hongera sana Simba SC @simbasctanzania , hongera sana @mbet_tz !!

Huu ni udhamini MKUBWA KULIKO WOWOTE kwa Klabu cha mpira cha Tanzania [emoji1241]

KLABU KUBWA NCHINI, UDHAMINI MKUBWA KUWAHI KUTOKEA..!!
Screenshot_20220801-183446_OGInsta%2B.jpg
 
FUNGA KAZI, M-BET WAFANYA KUFURU KWA SIMBA SC

"M-Bet ni kampuni namba moja ya michezo ya kubashiriki sasa tunashirikiana na klabu namba moja Tanzania."

"Tunaamini kama M-Bet tukishirikiana na Simba tutajitangaza ndani na nje ya Tanzania."

"Mwaka wa kwanza - Bil 4.670
Mwaka wa pili - Bil 4.925
Mwaka wa tatu - Bil 5.205
Mwaka wa nne - Bil 5.514
Mwaka wa tano - Bil 5.853

Jumla ni Bilioni 26, milioni 168 na Tsh. 5,000."- Mkurugenzi wa Masoko wa M-Bet, Allen Mushi (@mrlivinglifetz).

#SimbaNaMBet #SimbaWeek #SimbaDay #NguvuMoja
Screenshot_20220801-183602_OGInsta%2B.jpg
 
Senzo Mbatha hajafanya lolote Tanzania iwe kwa Simba au Yanga zaidi amejinufahisha yeye binafsi na kutengeneza CV yake ila kwa hapa Tanzania amepita kama watu wengine.

Jemedari Said.
Via EFM Radio ( Sports HQ ).
Screenshot_20220801-183813_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578] Juma Ayo

MAONI HURU:

[emoji871]Hakika sikutegemea kusikia bilion 26 kwenye Mkutano wa simba leo,hii ni babkubwa sana huwezi kuacha bilion 26 ukachukua bilion 12 mpira ni biashara kubwa sana hapa nawapongeza simba.

[emoji871]Ukiachana na mkataba mnono huu Lakini simba hamjatutendea haki leo ,kukataa maswali ni kuendelea kutufanya wote tubaki na mtazamo unaofanana
Hatukuambiwa pesa zitalipwaje ? (Installment) kwa mwezi? ,miez? Au mwaka?
[emoji871]Wadhamini wenyewe hawajatuambia faida wanazopata kwa mwaka ili tufanye majumuisho ya fedha inayoingia na bilion 4 zitakazotoka?
Hatujaambiwa bonus za simba zitakuaje endapo wakifika katika hatua muhimu za mashindano?

[emoji871]Binafsi naweza kuuliza kwa namna nyingine lakini kupitia public conference unaposaini mkataba mkubwa kama huu ni muhimu sana kutoa nafasi ya maswali ili majibu yapatikane, tunapokosa majibu ya maswali yetu athari yake tunarudi kuuliza kwenye platforms na media outlets, hii inawafanya walaji wetu (wasikilizaji/watazamaji ) kubaki njia panda. @ahmedally_ @bvrbvra
Screenshot_20220801-183446_OGInsta%2B.jpg
 
KWA NINI M BET??

M Bet wameweza kukudhi mahitaji yetu, Simba tunajivunia kuwa timu bora Tanzania na Afrika, kwa hiyo lazima tufanye kazi na kampuni ambayo pia ni kubwa na bora kwenye eneo lake.

M Bet wameona ukubwa wa Simba na thamni yake ndani na nje ya nchi.

Commitment ya M Bet kwa Simba, wana-support vitu vingine vingi nje ya uwanja mfano mzuri ni Simba Day.

Mkataba upo kwa ajili ya senior men’s team [timu ya wanaume ya wakubwa] kwa hiyo tukiamua kutafuta mdhamini wa Simba Queens, Simba U17 na U20 tuna nafasi hiyo.

— @bvrbvra, CEO SIMBA
Screenshot_20220801-184212_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom