Makapuku Forum

Makapuku Forum

Kwa hoja ya daraja unaweza usiwaelewe Simba ila kwa hoja ya kiwango basi unawaelewa vyema sana Simba
Screenshot_20220801-184415_OGInsta%2B.jpg
 
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi Simba, Salim Abdallah ‘Try Again’ amefichua siri ya usajili wao msimu huu akisema kwa sehemu kubwa umechangiwa na wadhamini wao wapya.
Try Again amesema wakiwa kwenye maandalizi ya msimu huu mpya wapewa fungu ambalo wamelitumia kwenye usajili wao.
“Tumepewa milioni 400 kabla ya kusaini mkataba huu, zimetumika kwenye usajili wetu ambao umefanyika,” amesema Try Again.
Try Again amesema kwenye upande wa udhamini watahakikisha wanasimamia vizuri fedha hizo na kutumika ipasavyo.

Screenshot_20220801-185620_OGInsta%2B.jpg
 
NYOTA wa kimataifa wa Tanzania aliyetua hivi karibuni katika timu ya Al Qadisiyah, Simon Msuva amekiangalia kikosi cha Yanga kisha akatamka kuwa msimu ujao kitakuwa moto balaa, ila akawapa neno kuwa ili watishe kimataifa na kuweka rekodi mpya basi lazima wajipange kikamilifu.

Msuva amejiunga hivi karibuni na klabu ya Al Qadisiyah inayoshiriki Ligi Daraja la Pili, Saudi Arabia baada ya kushinda kesi yake FIFA dhidi ya klabu aliyokuwa akiichezea awali, Wydad Casablanca ya Morocco.

Alisema wachezaji iliowaongeza kikosini wakiwemo Stephane Aziz Ki (ASEC Mimosas) Lazarous Kambole (Kaizer Chiefs), Bernard Morrison (Simba), Joyce Lomalisa (G.D. Sagrada Esperança) na Gael Bigirimana (Glentoran FC) ni wa kiwango kikubwa na kama wataendana kwa haraka na falsafa ya kocha wao basi timu hiyo itakuwa haishikiki.

“Yanga wako vizuri sana kwani nilichofurahi wale wachezaji wao walioipa mafanikio timu hiyo msimu uliopita, asilimia kubwa wamebaki na pia wameongeza majembe hasa ambayo wakishirikiana na waliopo na kupata muunganiko mzuri kwa haraka basi watakuwa moto sana.

“Kufanya vizuri kwenye ligi msimu ujao sina mashaka nao lakini mashindano ya kimataifa ni tofauti kidogo wanatakiwa kufanya maandalizi makubwa na wachezaji wajitoe mara mbili zaidi uwanjani ili kuipa timu hiyo mafaniko.
Screenshot_20220801-185740_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said amefanya uteuzi kwa kuwateua Saad Kawemba kuwa Mkurugenzi wa Mashindano na Walter Harson kuwa Meneja wa Timu.

Katika teuzi hizo Saad amechukua nafasi ya Thabit Kandoro ambaye amemaliza mkataba wake na Walter amechukua nafas ya Hafidh Saleh ambaye amekuwa mratibu wa timu.
Screenshot_20220801-185916_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578] Scanda24

FOOTBALL ECONOMY || Heshima Full Tank [emoji921]
.
#HeshimaFullTank kwako mkuu wa idara ya masoko ya @mbet_tz ndugu yangu, rafiki yangu wa kibiashara @mrlivinglifetz kwa kuwa sehemu ya historia ya kusaini mkataba Ghali zaidi kwenye historia ya udhamini wa klabu za Kariakoo.
.
#HeshimaFullTank iwafikie kwa kupandisha thamani soka la Tanzania kwa udhamini huu wa Thamani kubwa. Sasa ni wakati wa mabadiliko wa vilabu vyetu kujiendesha na kuepukana na kua Omba-omba.
.
#HeshimaFullTank kwa Mashabiki wa Simba, wameamua kukuheshimu kwa kuwa mashabiki wa @mbet_tz kwa maana ya ongezeko la Wafuasi mitandaoni lakini msukumo wa Kubashiei kupitia #MbatTz.
.
HESHIMA FULL TANK [emoji921] @mrlivinglifetz.
.
NB
Bato imehamia kwa wadhamini, nani atatengeneza faida.? Zote ni Betting za Mitandao. Vita ya kibiashara kwenye ushabiki.
.
Screenshot_20220801-183602_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578] Scanda24

FOOTBALL ECONOMY || The Art Of Negotiation [emoji273].
.
Dunia ya leo ya Biashara inawahitaji watu walio na uwezo wa kukupa matokeo kwenye meza ya majadiliano ili kupata mikataba minono. Dunia ya leo inalitambua jina la Barbara Gonzalez.
.
Mwanzoni alipata shida kupambana na MASELA ambao walitaka kumuondoa sababu ya nguvu na namna ya kuiongoza Taasisi. Nguvu yake haikua ndogo katika kuhakikisha maslahi ya klabu yanakua kipaumbele kuliko USELA.
.
●Mkataba wa Jezi za Simba ndio mkataba Ghali zaidi Tanzania.

●Mkataba wa Mdhamini mkuu wa klabu ndio mkataba ghali zaidi Tanzania kwa Sasa.
.
Hii inakuonesha ni kwa kiasi gani Simba wakienda mezani wapo Serious na pesa kuliko maneno maneno ya kwamba wao ni klabu TAJIRI. Ukimuangalia Barbara basi unapaswa uamini uwepo wake ni FAIDA kwenye Mapinduzi ya Biashara katika Soka ya Tanzania.
.
HESHIMA FULL TANK [emoji921] @bvrbvra
.
NB:
Ilikua ni kazi rahisi kumliza MSELA hadi Kamasi.
.
Screenshot_20220801-184212_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578] Scanda24

FOOTBALL ECONOMY || Emotional Intelligence [emoji419]
.
BYUTI BYUTI

Umetoka kuchukua vikombe heshima ya mashindano yote rasmi yanayotambulika na shirikisho, umetoka kufanya Uchaguzi na Usajili makini na kila siku unajinasibu wewe ni timu ya WANANCHI.
.
THEME ya kuelekea siku muhimu ya kufungua msimu unakuja na masihara ya kauli mbiu isowaunganisha wananchi wako. Byuti Byuti Ndio nini na inawakilisha nini katika safari yetu ya ubora na pesa..?

Bora wangeniomba niwape #HeshimaFullTank ili ibebe maono ya Heshima waloiweka kuanzia kwenye makombe hadi kushinda vita za usajili. #HeshimaFullTank ingewakilisha mustakabali wa Kibiashara na kuwafanya wananchi watambe.
.
#HeshimaFullTank[emoji736]️[emoji736]️
#ByutiByuti [emoji777]️[emoji777]️[emoji777]️
.
.
HATUZUILIKI, HATUSHIKIKI

Umetoka kwenye msimu hujashinda kitu chochote, umetoka kwenye msimu mgumu wa mashindano ya ndani na nje ya nchi kisha unasema HATUZUILI, HATUSHIKIKI. Wapo nyuma ya muda kuna sehemu wana shida kwenye kuwasiliana.
.
Kampeni ya mwaka huu ilipaswa kuwaleta watu pamoja sio kuwapa sifa wasokua nayo ni kukejeli mioyo ya ushabiki. Badala yake walipaswa kuwapa nguvu, kuwapa moyo na kuwashikanisha, ilitakiwa itengenezwe THEME kama vile tunarudi kwenye wakati wetu.
.
Wangeniita mimi ningewapa #NguvuMojaExtra ni slogan ya timu lakini ni kuamka kutafuta tena heshima waloipoteza. NGUVU MOJA EXTRA ingewapa mashabiki morali wa kwenda kuipigania timu mara mbili ya ilivyokua na mwisho kuonesha nguvu ya UDHAMINI.
.
Screenshot_20220801-190239_OGInsta%2B.jpg
 
[emoji3578] Scanda24

FOOTBALL ECONOMY || Hard Talk.
.
Yanga inadhaminiwa na Taasisi ilozoea kutengeneza FAIDA na Yanga ni Taasisi ISOFAHAMU maana ya FAIDA. Yanga hawajawahi kukaa wakasema sasa tumepata faida ya thamani ya nembo yetu sababu ni rahisi tu, hawajawahi kufanya biashara ya NEMBO yao.
.
Kinachotokea kwenye mauzo ya JEZI ni kipimo cha Historia ya Yanga, utasikia mbona mwaka fulani hatukupata, mbona kabla ya hawa hatukupata, ni bora hiki kidogo kinachopatikana. Nawakumbusha, wakati huo sio kama huu ambao watu wanajaa kununua jezi kwa bei ya KARAHA.
.
Katika Dunia ya Biashara ni wakati wa Klabu kuhakikisha klabu sio tu inaizidi historia yake kipesa bali klabu inatengeneza THAMANI mpya Sokoni ili kupata pesa nyingi kirahisi. Ni muda wa Yanga kuondokana na Buku Mia Tatu (1300 Tzs) Bali kutengeneza PESA Ya Uhakika inayoendana na HESHIMA ya Nembo.
.
Mwisho wa Msimu Yanga atakua na chini ya milioni mia mbili za mauzo ya Jezi na bidhaa nyingine, sababu ni rahisi tu, Yanga wamekubali kupata gawio la hesabu za mauzo mwisho wa Msimu. Ni ngumu kuona thamanj ya nembo yao kwenye MERCHANDISING sababu ya Ramani wanayotembea nayo. Msambazaji anakadiria aseme ameuza kiasi Gani.
.
AMKENI KUMEKUCHA[emoji419]
.
NB:
Basi watasema CHUKI.
.
Screenshot_20220801-190239_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan amewaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu Dar es aalaam jioni ya leo akiwemo Mkuu mpya wa Mkoa wa Kagera Albert Chalamila na kusema yafuatayo.

“Mwanangu Chalamila mmh mmh mategemeo yangu umekua sasa, akili imetulia, wewe ni Mfanyakazi mzuri lakini mtundu mno, sasa nilikuacha nje kipindi hicho nimeamua kukurudisha naomba ukakue”

“Ukue akili itulie uende ukafanye kazi ukanisaidie katika eneo ulilopangiwa, wala hii haina maana kwamba ndio umemaliza ukikaa hapo umekaa nakuangalia kwa ukaribu sana” ——— amesema Rais Samia leo.
Screenshot_20220801-190622_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia amewaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu Dar es aalaam leo ambapo amesema “Kuna Wamama wawili Wakuu wa Mikoa wapya hapa ambao mlishawahi kuwa Wakuu wa Mikoa zamani (Halima Dendego na Fatma Mwasa) najua kazi zenu mmekaaa nje nadhani kwa miaka mitano/sita na ni imani yangu kwamba hamjasahau mtarudi mkafanye kazi kama mlivyokuwa mkifanya kazi”
Screenshot_20220801-190725_OGInsta%2B.jpg
 
Rais Samia amewaapisha Viongozi mbalimbali Ikulu Dar es aalaam leo ambapo amesema “Makanali hatuwarajii kuvaa kombati mkiwa Wakuu wa Mikoa kwahiyo kombati zipumzike mpaka mtakaporudi Jeshini”

“Mwenzetu Bwana Suleiman Mzee aliyekuwa Kamishna wa Magereza nimeamua kukuleta uraiani, umetoka Jeshini umeingia Jela sasa upo uraiani angalau uone uraiani kuna nini lakini Jeshi unaliacha ulikotoka kule ni uraiani kuna kanuni sheria zake na kila kitu kashirikiane na uliowakuta mkafanye kazi”
Screenshot_20220801-190822_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa awamu ya nne wa Tanzania, Dr. Jakaya Kikwete ameteuliwa kuongoza Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Kenya kutoka Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Ujumbe huo wa Maafisa 52 utakuwa ukiangazia kiwango cha matayarisho na mchakato mzima wa Uchaguzi Mkuu wa Kenya unaotarajiwa kufanyika August 09,2022 na baadaye Maafisa hao watatoa ripoti August 11,2022.
Screenshot_20220801-190918_OGInsta%2B.jpg
 
Club ya Simba SC leo imetangaza thamani ya mkataba wao wa udhamini Mkuu na M Bet kuwa una thamani ya Tsh Bilioni 26.1 katika kipindi cha miaka 5.

CEO wa Simba, Barbara amesema “Leo ni siku kubwa kwa Simba na M-Bet, swali kubwa ni kwanini M-Bet, sababu kubwa ni wameweza kukidhi mahitaji yetu, Washirika wote wa Simba kwa sasa wamejitoa kwa Simba tu”

“Kwa ukubwa wa Simba ni lazima kujihusisha na kampuni ambayo inaongoza kwenye biashara ambayo wanafanya. Mkiangalia takwimu M-Bet wanaongoza kwa ukubwa Tanzania”

"Hii ni mara ya kwanza mdhamini mkubwa anakuwa na senior team pekee, huko nyuma mdhamini mkuu alikuwa kwa timu zote lakini sasa timu zingine tunaweza kuzitafutia mdhamini wake”
Screenshot_20220801-191028_OGInsta%2B.jpg
 
Chama tawala cha African National Congress nchini Afrika Kusini kimethibitisha msimamo wake kwamba Benki Kuu nchini humo inapaswa kutaifishwa, Rais wa nchi hiyo Cyril Ramaphosa amesema hayo baada ya uamuzi huo kufanywa wakati wa kongamano la sera siku tatu zilizopita.

Katika hotuba yake ya kuhitimisha, Ramaphosa amesema kuwa kongamano hilo lilitaja kasoro hiyo ya kihistoria ya kubinafsishwa kwa Benki hiyo kuu na kuthibitisha tena azimio kwamba Benki hiyo inapaswa kumilikiwa kikamilifu na raia wa Afrika Kusini.

Ramaphosa ameongeza kuwa wajumbe katika kongamano hilo walikuwa wameihimiza serikali kufanya hivyo kwa njia na kasi ambayo ingezingatia gharama kwa hazina ya taifa hilo ambayo tayari imetumika kwa kiwango kikubwa.

Tofauti na benki kuu nyingi duniani, benki kuu ya Afrika Kusini inamilikiwa na watu binafsi, mwaka 2017, chama cha ANC kiliazimia kuitaifisha kikamilifu lakini bado hakijatekeleza uamuzi huo.
Screenshot_20220801-191132_OGInsta%2B.jpg
 
Back
Top Bottom