Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220607-062926_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20220607-062949_Opera%20Mini.jpg
 
Mbunge wa Ubungo, Prof. Kitila Mkumbo ameiomba Serikali kutazama upya sheria inayoruhusu watu kufanya shughuli zao saa 24 huku akisema sheria hizo zimepitwa na wakati hivyo zinapaswa kutazama upya.

Prof. Mkumbo ametoa ombi hilo wakati akichangia mjadala wa makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023.

"Majiji yote duniani hufanya kazi saa 24, hii habari ya kwamba watu asubuhi wasifungue biashara, wasifungue baa na wasifurahi mpaka saa sita mchana ni sheria ya kizamani"

"Hii sheria inazuia furaha ya nchi, Waziri uiangalie, tuibadilishe ili watu wawe na uhuru wa kufurahi wakati wowote maadam wanazingatia sheria za nchi" View attachment 2252747
YEEEEES
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom