Makapuku Forum

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohammedi Mchengerwa Bungeni Dodoma leo amesema "Katika kipindi hiki mafanikio lukuki yamepatikana kupitia BAKITA, naweza kujinasibu kuwa matumizi ya Kiswahili yanazidi kukubalika kitaifa, kikanda na kimataifa ambapo jitihada hizo kwa kipindi cha mwaka 2021/22 zimezaa matunda kwa Kiswahili kuvishwa joho jipya kuwa lugha ya kazi katika Umoja wa Afrika"

"Kiswahili kilipitishwa kuwa Lugha ya Kazi ya Umoja wa Afrika katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali uliofanyika tarehe 5 - 6 Februari, 2022 Jijini Addis Ababa, Ethiopia, hatua hii ni fursa muhimu kwa Wataalamu wetu wa Tafsiri na Ukalimani nchini ambao katika muda mfupi tu tayari Watanzania 65 wamesajiliwa kupata fursa za ajira za muda na za kudumu katika Umoja wa Afrika na Kamisheni zake"

"Pia, kutokana na nafasi ya Kiswahili, kuendelea kushamiri, baadhi ya Vyuo Vikuu vya nje ya Tanzania ambavyo awali havikuwa na programu za Kiswahili vimeanza harakati za kuingiza Kiswahili katika programu zao ambapo tayari kuna makubaliano ya awali ya kushirikiana kati ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Ethiopia, Chuo Kikuu cha Port Harcourt (Nigeria) na Chuo Kikuu cha Joachim Chisano (Msumbiji) katika kufundisha Kiswahili"
 
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa akiwasilisha bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2022/2023, jijini Dodoma leo. Mchengerwa ameliomba Bunge lipitisha bajeti ya wizara hiyo kiasi cha Sh35.4 bilioni kati ya hizo Sh10 bilioni ni kwa ajili ya kukarabati viwanja saba vya michezo ili kukidhi vigezo Tanzania kuandaa mashindano ya kimataifa ikiwemo Afcon 2027. Picha na Edwin Mjwahuzi
 
Mbunge wa Viti Maalumu, Khadija Taya maarufu Keisha akizungumza bungeni alipokuwa akichangia mjadala wa kupitisha makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa mwaka wa fedha 2022/2023, jijini Dodoma leo.

Khadija amelieleza Bunge kuwa wasanii na muziki si kwamba hawapo waliokwenda shule ambapo amewataja baadhi yao wenye stashahada, shahada na shahada ya uzamili. Picha na Edwin Mjwahuzi
 
Wataleta mmomonyoko wa udongo.
 
Auntie si ugombee ubunge jamani, hebu acha kuota ndoto ndogo ndogo.
 
Kwamba unaniona Mikocheni Mara ya tatu hii?
Dah!!! Huyo unayemuona usinifananishe naye kabisa...

Jioni niwe wapi ndugu? Najua wewe Weekend end yako ni J3
Enjoy...

Umeshafika 25?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…