Makapuku Forum

Inakuwaje sio bora ili hali vilabu vyake vinafanya vyema kwenye mashindano ya Caf,ukitaja ligi bora barani afrika na zenye ushindani wa hali ya juu hii ligi ya South ipo kwenye 10
Inatajwa kuwa bora kwa kuwa ligi zetu zina mizengwe mingi mno

Chukulia hapa bongo bila yanga na simba ligi itakuwaje

Ligi zetu nyingi ni za michongo anapo tokea tajiri kuwekeza ndio tunaona zinachukua ubingwa
 
Inatajwa kuwa bora kwa kuwa ligi zetu zina mizengwe mingi mno

Chukulia hapa bongo bila yanga na simba ligi itakuwaje

Ligi zetu nyingi ni za michongo anapo tokea tajiri kuwekeza ndio tunaona zinachukua ubingwa
Ni kweli kabsa mkuu, ila ukweli utabaki wazi kuwa ligi ya South Africa ni bora...kushindanisha na hapa kwetu...

Ndio maana unaona leo hii Mamelodi au Mazembe wanaonesha ushindani wa kweli pale wanapokutana na vigogo kutoka kaskazini kwa sababu ligi zao zina ubora, kuanzia miundombinu, mikataba
 
Rais Samia wakati wa uzinduzi wa filamu ya Royal Tour Arusha leo amesema wakati wa uandaaji wa filamu hiyo wapo Watu mitandaoni walisema amejigeuza Rambo au Arnold Schwarzenegger badala ya kufanya kazi lakini amesema faida ya filamu hiyo ni kubwa.

"Wakati nafanya hili jambo kuna Wadogo zangu, Wanangu kwenye mitandao wakawa wanasema 'Huyu Mama badala ya kufanya kazi amejigeuza Rambo au Schwarzenegger anafanya mafilamu huko anaigiza' lakini nikasema ngoja tuone kitakachotoka"

"Tumeanza kuizindua Marekani, tulipoanza New York ile siku salamu za Watu laki tatu na zaidi wakawa wanapongeza , Los Angeles nako tukapata mrejesho mzuri sana, kufanya jambo kama hili kunahitaji kujitoa, nimetumia siku nane nje ya Ofisi na siku nane kukaa nje ya Ofisi ya Rais ni muda mrefu sana"

"Niwahikikishie hasara ambayo nimeisababisha kwa kutokaa kwenye Ofisi kwa siku nane na kutohudumia Wananchi kwa kipindi kile italipa mara elfu mbili mara hadi mara elfu tatu kutokana na filamu hii, tumefanya vikao na Watu mbalimbali marekani baada ya kuuona filamu wanasema wanataka kuja Tanzania"

auntie maki njooo umsome mama yako kumbe anafatilia mitandao nimecheka sana
 
Hizi ni picha nyingie kutoka AICC, Jijini Arusha kwenye uzinduzi wa Filamu ya Royal Tour ambao umeongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

Kwenye picha hizi kuna muonekano wa Watu mbalimbali wakiwa wamejitokeza kushuhudia uzinduzi huku wengine wakiwa wamevalia mavazi ya asili kuonesha utamaduni wa Kimasai kutoka Tanzania
 
Nje ya ukumbi wa AICC, Arusha Mtayarishaji wa Filamu ya The Toyal Tour Peter Greenberg ameelezea changamoto aliyokutana nayo wakati wa uandaaji wa Filamu ambapo amekiri ilimbidi kwenda na muda maana anafanya kazi na Mkuu wa Nchi (Rais Samia) na ana mambo mengi ya kuyashughulikia na hivyo walilazimika kufanya kazi ndani ya muda mfupi.
 
Rais Samia ameishukuru Timu ya Waandaji wa filamu ya Royal Tour kwa kukamilisha filamu hiyo na kusema haikuwa kazi rahisi kukamilisha filamu hiyo ambayo imerekodiwa ndani ya siku nane.

"Nalishukuru sana kundi la production, haikuwa kazi rahisi, waliniambia weka Urais wako Ofisini, ukija huku ni Tour Guide wewe ni Actress, Urais sisi hatuna habari nao, action moja naifanya mara kumi na mara nyingine nakasirika wanasema 'No, no Samia you have to do it' nikimaliza anasema unatakiwa kurudia"

"Kwa Tanzania tumeanzia uzinduzi Arusha kwasababu ndani ya Arusha ndiko Utalii ulikojikita baada ya hapa tutaenda Zanzibar na Dar es salaam"
 
...mama, wengine hatuna tatizo kabisa na ulichofanya, sema nini ujue, tuambie umelipwa shilingi ngapi kuekiti hii movie, na je part wo itakuwepo au ndiyo imetoka vile.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…