Makapuku Forum

Makapuku Forum

Mahakama nchini Morocco imemhukumu Mwanaharakati kifungo cha miaka minne jela baada ya kumchukiza Mfalme Mohammed wa sita kwenye mtandao wa kijamii.

Rabie Al Ablaq amehukumiwa kifungo cha miaka minne jela kwa kumkosoa Mfalme mtandaoni, kesi hiyo ilifunguliwa Aprili 11 baada ya kupost mtandaoni video zinazokosoa tofauti za kijamii na ufisadi nchini humo.

Mwanaharakati na Mwanahabari huyo mwenye umri wa miaka 35 pia alipigwa faini ya dirham 20,000 ($2,000).

Human Rights Watch imesema Al Ablaq alitiwa hatiani kutokana na video mbili zilizopostiwa Facebook na YouTube mnamo Septemba na Novemba 2021 ambapo alimzungumzia Mfalme na kulinganisha hali yake binafsi na umaskini ulioenea nchini Morocco.View attachment 2203687
Africa ni sehemu ya jehamu ukisema ukweli
 
Screenshot_20220428-142438_OGInsta%2B.jpg
 
MAMELODI MABINGWA MARA 5 MFULULIZO
.
2017/18 — Mamelodi
2018/19 — Mamelodi
2019/20 — Mamelodi
2020/21 — Mamelodi
2021/22 — Mamelodi
.
Klabu ya Mamelodi Sundowns imeweka Rekodi ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa mara ya TANO mfululizo. View attachment 2203743
Ligi bora hutoa washindani bora

Ligi ukiona mmoja anachuku mfululizo ujue ubora wa ligi ni mdogo sana

Na hilo inakubidi uangalie uwekezaji wa timu pinzan na huyo bingwa
 
FISTON Mayele alitoa ahadi mbili ambazo moja ilikuwa ni kuifunga Namungo FC ambayo ameikamilisha na ya pili ni ya kupachika bao katika mechi ya watani wa jadi, Yanga na Simba itakayochezwa Jumamosi kuanzia saa 11 jioni kwenye Uwanja wa Mkapa, Dar es Salaam.

Lakini, wakati watu wakisubiri kuona kama mshambuliaji huyo atatimiza ahadi hiyo au la, ameweka rekodi ambayo bila shaka upande wa pili wakiisikia hawawezi kumdharau mshambuliaji huyo na watalazimika kumuandalia ulinzi wa ziada ili asiwaletee madhara.

Rekodi hiyo ya Mayele ambayo sio taarifa nzuri kwa Simba kuelekea mechi baina yao Jumamosi ni ile ya kuhusika moja kwa moja na mabao saba katika michezo sita mfululizo ya Ligi Kuu ambayo Yanga imecheza kabla ya mchezo huo wa watani wa jadi.
Screenshot_20220428-144346_OGInsta%2B.jpg
 
MWAMUZI Ramadhan Kayoko amepewa kazi kuchezesha mchezo wa Kariakoo Derby kati ya Yanga na Simba utakaochezwa April 30, kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa.
Kayoko atasimama katikati huku akisaidiwa na Frank Komba (Dar es Salaam), Mohamed Mkono (Tanga), wakati Elly Sasii (Dar es Salaam) atakuwa mwamuzi wa mezani.
Screenshot_20220428-144453_OGInsta%2B.jpg
 
LICHA ya kwamba mkataba wake unaelekea ukingoni huku akihusishwa na kurejea Azam, kipa namba moja wa Simba, Aishi Manula juzi usiku alitamka kauli ambayo ni wazi msimu ujao atakuwa Msimbazi.

Kipa huyo baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere wakitokea nchini Afrika Kusini walikotolewa na Orlando Pirates alisema; “Tuna kazi kubwa msimu ujao.”

“Binafsi naona tunapiga hatua kuanzia robo fainali ya kwanza mpaka ya tatu kuna maendeleo makubwa, kwa hiyo naona msimu ujao tunaweza tusiishie tulipoishia leo bali tukaanzia hapa,” alisema Manula ambaye habari za chinichini ni Azam walimwekea cheki mezani mwezi mmoja uliopita na wanamsikilizia yeye.
Screenshot_20220428-144606_OGInsta%2B.jpg
 
Muonekano wa ndani na nje ya ukumbi wa Simba Hall, AICC, jijini Arusha ambapo Rais Samia Suluhu Hassan atafanya uzinduzi wa 'The Royal Tour' leo Aprili 28, 2022 kuanzia saa 8:00 mchana.

Uzinduzi huu utahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na Wadau wa Sekta ya Utalii nchini.View attachment 2203666
Mambo ya Usindusi utafanyeka hapa Auntie( kwa sauti ya Zumaridi)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom