Mechi zinazoendelea kwenye hatua Robo Fainali michuano ya Afrika na kwa kuwa tunapata kuitazama tuna mengi ya kujifunza hata namna tunavyoendesha mijadala yetu au kulaumu tunakuwa na kiwango na ubora wa michuano yenyewe.
Niwatakie kila la kheri wawakilishi wa Tanzania @simbasctanzania na kuwapongeza kwa hatua waliyofikia kwa sasa kwa namna wanavyopambana kwenye hatua ya makundi na kuhakikisha wanaingia Robo Fainali
Hatua ya Robo Fainali ni hatu inayotoa bingwa wa michuano kwa maana hiyo ni hatua yenye vilabu bora kwa michuano husika, so kunahitajika kikosi bora kupambana kupata matokeo ya jumla kwa mechi mbili kwenye hatua hii
ufundi, mbinu uwajibikaji ni wa kiwanga cha juu.
Kama wa Tanzania tunatamani kuona timu zetu zinatwaa ubingwa siku moja japo inawezekana timu kuchukua ubingwa kwa bahati lakini bado tuko mbali kusema tunautaka ubingwa ukilinganisha na vilabu ambavyo mara kwa mara vimekua vikiingia fainali.
Kuhusu mchezo wa wenyewe [Orlando Pirates vs Simba] kwenye karatasi inaonekana Simba wametoka na sio kwa bahati mbaya ni kutokana na matokeo ya Simba kwenye mechi za ugenini na kiwango kilichoonyeshwa na timu pinzani kwenye mechi ya mkondo wa kwanza.
Hiyo haiwazuii kupata matokeo ya jumla ndani ya kiwanja na kusonga mbele japo sio kazi nyepesi, kinachohitajika ni mpango mzuri wa kuicheza mechi kutoka benchi la ufundi na utekelezaji kutoka kwa wachezaji kuhusu viongozi kutekeleza majukumu yao, sina shaka na eneo hili.
KILA LA KHERI SIMBA, KILA LA KHERI TANZANIA.
- Amri Kiemba