Mmmmh mambo mengi muda mchache
Wakati mwingne ukitafakari unaona watu wanaridhishwa ujinga kwenye nyumba zao za ibadaAfisa wa Taliban amesema mlipuko wa bomu kwenye Msikiti na Shule ya kidini kaskazini mwa Afghanistan jana Ijumaa uliua zaidi ya Watu 30, wakiwemo Wanafunzi.
Naibu Waziri wa Utamaduni na Habari wa Taliban, Zabihullah Mujahid, amesema bomu hilo katika mji wa Imam Saheb mkoani Kunduz pia liliwajeruhi Watu 43, wengi wao wakiwa Wanafunzi.
Hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulio hilo, lakini tawi la Dola la Kiislamu nchini Afghanistan lilidai kuhusika na mashambulizi ya mabomu yaliotokea siku moja kabla, likiwemo dhidi ya msikiti wa Kishia katika mkoa wa Mazar-e-Sharif, ambamo Waumini wasiopungua 12 wa Kishia waliuawa.
View attachment 2198336
Daaah marehemu hana sauti ila kuna namna ilitokeaMpiga debe mmoja wa eneo la Makambako Mkoani Njombe amefariki dunia kwa kukanyagwa na tairi za gari katika kichwa chake kutokana na kuanguka wakati akifukuzia basi linalofanya safari zake kutoka Mbeya kwenda mkoani Mwanza kwa lengo la kupata posho yake ya kupakia abiria.
RPC wa Njombe Hamis Issah amesema "Mpiga debe alikuwa amefuata fedha yake kwa ajili ya abiria aliokuwa amewapakia na kwa bahati mbaya ule malango wakati unajifunga alisukumwa na akadondokea kwenye uvungu na tairi za nyuma za gari ambazo zilimpitia”
RPC Issah ametoa wito kwa Wafanyakazi wa maeneo ya stendi kuwa makini na kuangalia usalama wao wakati wa kufanya kazi zao.View attachment 2198339
Kuna watu wana ujasiriMtoto Salah Jackson (5) mwenye ulemavu wa viungo, mkazi wa kijiji cha Makiwaru, mkoani Kilimanjaro amefariki dunia kutokana na njaa na kisha mama yake mzazi kumzika kimya kimya usiku wa manane.
Mtoto huyo anadaiwa kuzikwa na mama yake mzazi aitwaye Rebecca Siowi (30) usiku wa kuamkia Aprili 22, 2022 nyumbani kwa bibi yake walikokuwa wakiishi yeye pamoja na mama yake baada ya mume kumtelekeza na watoto watano.
Tukio hilo liligundulika baada ya mtoto huyo kutoonekana jioni ya Aprili 21 nyumbani alikokuwa akiishi kwa bibi yake, ambapo bibi yake huyo alifanya jitihada za kumtafuta mjukuu wake huyo bila mafanikio ndipo Aprili 22 alipobainika kuwa amezikwa.
Akizungumzia tukio hilo leo Aprili 23, 2022 Kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amekiri kuwepo kwa tukio hilo, akisema baada ya kupata taarifa hiyo kutoka kwa wananchi walifika eneo la tukio kuona sehemu alipozikwa mtoto huyo.
View attachment 2198344

SawaKufwaaaaaa![]()
Ndio umeachiwa!!Sawa