Makapuku Forum

Makapuku Forum

Polisi nchini Uganda walifunga barabara kadhaa jijini Kampala wakati mtoto wa Rais Yoweri Museveni aitwaye Muhoozi Kainerugaba akisherehekea siku yake ya kuzaliwa.

Muhoozi ni Luteni Jenerali wa Jeshi la Wananchi wa Uganda ametimiza miaka 48
Screenshot_20220424-170856_OGInsta%2B.jpg
 
Baada ya filamu ya Royal Tour kuzinduliwa katika miji ya New York na Los Angeles Marekani, gari lililoonekana likiendeshwa na Rais Samia Suluhu Hassan katika filamu hiyo, limekuwa kivutio kipya cha utalii katika Hifadhi ya Serengeti.

Gari hilo aina ya Toyota Land Cruiser Hardtop lililoongezwa ukubwa kwa ajili ya shughuli za kitalii, Samia alionekana akiliendesha akiwa na mtayarishaji wa filamu hiyo, Peter Greenberg.

Kwa mujibu wa tovuti ya Toyota, aina hiyo ya gari kwa sasa inauzwa Sh198.9 milioni.

Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (Tanapa) imeliarifu Mwananchi kuwa, baada ya uzinduzi wa filamu hiyo watalii wa ndani na nje waliotembelea hifadhi ya Serengeti wamehamasika kuliona.
Screenshot_20220424-171000_OGInsta%2B.jpg
 
CAF CONFEDERATION CUP
.
ORLANDO Vs SIMBA SC (Agg 0-1)
19:00
Orlando Stadium
.
Orlando wamekuwa timu tishio wanapocheza mechi katika uwanja wao wa nyumbani na kinyume chake Simba wamekuwa dhaifu ugenini. Katika mechi 10 za mashindano ya klabu Afrika Orlando Pirates wamecheza nyumbani wameibuka na ushindi mara sita na kutoka sare nne.
.
Hali ni tofauti kwa Simba mechi 10 za mwisho walizocheza ugenini, wameibuka na ushindi mara 2, sare 2 na kupoteza michezo 6. Nani anatoboa leo __!!View attachment 2199014
Mungu wabariki Orlando.
 
: "Vijana walicheza vizuri, walimiliki mpira kwa asilimia kubwa, lakini bahati haikuwa upande wetu, kosa dogo limetugharimu tumetolewa, malengo yetu yalikuwa kutwaa ubingwa.”

- Manqoba Mngqithi, Kocha wa Mamelodi Sundowns View attachment 2199011
Ametoa kauli ya kimchezo kama mwalimu mkuu
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Abdulrahman Kinana amesema Nchi ya Tanzania imeharibiwa hivyo wapewe muda ili kuweka vitu katika njia inayotakiwa.

Kinana ameyasema haya kwenye iftar ya miaka 18 ya kampuni ya usafirishaji ya @silent_ocean_ltd ambayo iliwaalika Watu mbalimbali wakiwemo Wafanyabiashara.

Kinana ametoa maagizo hayo baada ya Wafanyabiashara kuiomba Serikali kuwatekelezea sehemu ya mambo ambayo yamekuwa kikwazo kwenye biashara.

“Hii Nchi imeharibiwa sana sana, imeharibiwa na vikao, Nchi imeharibiwa na mchakato, tutaifanyia kazi, nchi imeharibiwa tupeni muda, tunataka vitendo” ——— amesema Kinana.View attachment 2199025
Kauli zao za kipuuzi kweli kila mtu anasema imeharibiwa nan aliharibu kama sio wao
 
Ummy Msika (45), mkazi wa kata ya Bomambuzi manispaa ya Moshi Mkoa wa Kilimanjaro amepata madhara mwilini baada ya rafiki yake kudaiwa kumpa maji ya uponyaji ‘upako’.

Msika aliyelazwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa ya Mawenzi amesema wakati akiumwa mguu rafiki yake alimwambia atampa maji hayo ya uponyaji kwa ajili ya kunywa na kupaka.

Ameieleza Mwananchi Digital leo Jumapili kuwa baada ya kunywa maji hayo Aprili mosi, 2022 kutibu tatizo lake la mguu alianza kuumwa na kupoteza hamu ya kula, kuanza kuwashwa sehemu za siri na kwamba kila kukicha tatizo lilikuwa likizidi na hali yake kuwa mbaya na ndugu zake walimchukua na kumpeleka hospitali.

Naye mmoja wa madaktari anayemhudumia mwanamke huyo kwa sharti la kutotajwa jina lake amesema wanaendelea kumpatia matibabu kadri ya uwezo wao.
View attachment 2199083
Duuuh
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom