Makapuku Forum

Makapuku Forum

Things you like to see

Lionel Messi ametwaa ubingwa wa Ufaransa akiwa na PSG, what a run
Screenshot_20220424-162250_OGInsta%2B.jpg
 
CAF CONFEDERATION CUP
.
ORLANDO Vs SIMBA SC (Agg 0-1)
19:00
Orlando Stadium
.
Orlando wamekuwa timu tishio wanapocheza mechi katika uwanja wao wa nyumbani na kinyume chake Simba wamekuwa dhaifu ugenini. Katika mechi 10 za mashindano ya klabu Afrika Orlando Pirates wamecheza nyumbani wameibuka na ushindi mara sita na kutoka sare nne.
.
Hali ni tofauti kwa Simba mechi 10 za mwisho walizocheza ugenini, wameibuka na ushindi mara 2, sare 2 na kupoteza michezo 6. Nani anatoboa leo __!!
Screenshot_20220424-162728_OGInsta%2B.jpg
 
| Pitso Mosimane:
.
“Ulikuwa mchezo mkubwa. Ningependa kuwashukuru wachezaji kwa kukabili changamoto. Tulifanikiwa kucheza vizuri ugenini na kuwa tayari kiakili kwa mchezo. TUNAJUA jinsi ya kucheza mechi za Ligi ya Mabingwa na tunazidi kuimarika.”
.
“Tunatumai, tutafanya kila tuwezalo ili kushinda taji la Ligi ya Mabingwa ya Afrika kwa mara ya TATU mfululizo. Ninaamini mafanikio kama haya yatakuwa ya kwanza ya aina yake barani Afrika na Misri,”
Screenshot_20220424-162842_OGInsta%2B.jpg
 
MNYAMA KAZI NI MOJA TU LEO, KUTINGA NUSU
.
Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara na wawakilishi pekee wa Tanzania kwenye michuano ya kimataifa, Simba inashuka uwanjani leo kucheza mchezo wa marudiano wa hatua ya robo fainali dhidi ya Orland Pirates
.
Mchezo huo, utakaopigwa kuanzia saa 1 usiku, kwenye Uwanja wa Orlando, Johannesburg, Afrika Kusini, Wekundu wa msimbazi haitaki kurudia makosa ya nyuma na hesabu yao ni moja tu, ni
la kufuzu hatua ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika.
.
Kila la kheri @simbasctanzania
Screenshot_20220424-162935_OGInsta%2B.jpg
 
“Miongoni mwa wachache ambao wanaamini kwamba @simbasctanzania leo wanaenda Nusu Fainali ni pamoja na mimi! Ikiwa naamini hivyo kutokana na matokeo ambayo Simba yuko nayo, wakipata sare ya aina yoyote au ushindi wa 2-1 simba wamepita! Mchezo wa ‘Tusiruhusu Bao’ ndio mchezo ambao @simbasctanzania wanatakiwa kwenda kucheza leo!”

Sababu nyingine ni inayonifanya niamini kwamba @simbasctanzania wanaenda kufuzu hatua ya Nusu Fainali Kombe la Shirikisho leo ni Kocha @pablofrancomartin, experience yake, falsafa na kiburi cha kuamini kile ambacho anakiamini ndivyo vitu vitakavyompa matokeo leo hii!”

“Sababu ya 3 ni jinsi ambavyo Simba SC inachukuliwa kwenye mashindano haya, Naweza kusema Simba kwenye michuano ya Kombe la Shhirikisho Barani Afrika ni kama Farasi Mweusi! Yani watu hawamzingatii sana Simba mbele ya wakongwe kama TP Mazembe, Orlando zinazobebwa na historia zao! Pale ambapo wanaichukulia poa Simba ndipo ambapo Simba atapenya kwenda Nusu Fainali leo hii!” - @jr_farhanjr Mchambuzi wa Michezo kutoka @cloudsfmtz

Screenshot_20220424-163314_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha Duniani (IMF) Bibi Christalina Georgieva, alipowasili Makao Makuu ya Shirika hilo Washington DC nchini Marekani.
Screenshot_20220424-163502_OGInsta%2B.jpg
 
Vyombo vya Habari nchini Korea Kaskazini vimetangaza Taifa hilo kupata kile ilichokiita nguvu isiyoweza kushindwa, ambayo Ulimwengu hauwezi kuipuuza na hakuna anaweza kuisogelea.

Vyombo hivyo vimeongeza kutaja mafanikio hayo kuwa yamepatikana chini ya Kiongozi wa taifa hilo Kim Jog Un, hatua ambayo inaonesha dhahiri ushahidi mwingine wa silaha zake za nyuklia, katika kipindi hiki Serikali ya Korea Kaskasini ikijiandaa na mapunziko ya kijeshi.

Taarifa za Shirika la Habari la Taifa hilo, KCNA zimeorodhesha historia ya mafanikio ya kijeshi ya taifa hilo kuanzia vita vyake dhidi ya Marekani 1950 hadi 1953, makabiliano madogomadogo katika kipindi cha Vita Baridi hadi mwaka 2010.

Kesho Jumatatu ni siku ya kumbukumbu ya miaka 90 tangu kuanzishwa kwa Jeshi la Mapinduzi la Watu wa Korea, na wachunguzi wa kimataifa wanatarajia Korea Kaskazini kufanya gwaride kubwa la kijeshi na ikiwezekana kufanya maonesho mengine ya silaha zake.
Screenshot_20220424-163605_OGInsta%2B.jpg
 
Uturuki imefunga anga lake kwa ndege za kiraia na kijeshi za Urusi zinazosafiri kuelekea Syria, tangzo hilo linaashiria moja ya majibu makali zaidi ya Uturuki, ambayo imejenga uhusiano wa karibu na Urusi licha ya kuwa Mwanachama wa Jumuiya ya kujihami ya NATO, kutokana na mashambulizi ya kijeshi ya Urusi nchini Ukraine katika kipindi cha miezi miwili.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mevlut Cavusoglu, amesema kuwa uamuzi huo aliuwasilisha kwa mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov, na baada ya siku mbili Rais Vladimir Putin wa Urusi alitoa amri ya kutotumia anga hilo.

Uturuki imesema marufuku hiyo itadumu kwa kipindi cha miezi mitatu, hata hivyo hakukuwa na majibu ya mara moja kutoka Urusi kutokana na tangazo hilo, Urusi pamoja na Iran zimekuwa waungaji mkono muhimu wa Rais wa Syria Bashar al-Assad wakati wa vita vya wenyewe kwa wenyewe vya nchi hiyo iliyoharibiwa vibaya.

Uturuki imekuwa ikijaribu kusuluhisha mzozo wa Ukraine na Urusi, ikiandaa mikutano ya wajumbe wa majadiliano wa Urusi na Ukraine mjini Istanbul, na mwingine kati ya Lavrov na mwenzake wa Ukraine Dmytro Kuleba mjini Antalya.
Screenshot_20220424-163706_OGInsta%2B.jpg
 
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM Abdulrahman Kinana amesema Nchi ya Tanzania imeharibiwa hivyo wapewe muda ili kuweka vitu katika njia inayotakiwa.

Kinana ameyasema haya kwenye iftar ya miaka 18 ya kampuni ya usafirishaji ya @silent_ocean_ltd ambayo iliwaalika Watu mbalimbali wakiwemo Wafanyabiashara.

Kinana ametoa maagizo hayo baada ya Wafanyabiashara kuiomba Serikali kuwatekelezea sehemu ya mambo ambayo yamekuwa kikwazo kwenye biashara.

“Hii Nchi imeharibiwa sana sana, imeharibiwa na vikao, Nchi imeharibiwa na mchakato, tutaifanyia kazi, nchi imeharibiwa tupeni muda, tunataka vitendo” ——— amesema Kinana.
Screenshot_20220424-163835_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, ameishutumu mipango ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kutembelea Urusi siku ya Jumanne kabla ya kwenda Ukraine Alhamisi akisema hakuna haki wala mantiki kwa Guterres kwenda Urusi kabla ya Ukraine "Ni kosa kubwa kwenda Urusi kisha ndio aje Ukraine wakati sisi ndio tumevamiwa "

Zelensky pia ametoa onyo kwamba watavunja mazungumzo na Guterres na Wasuluhishi wengine wa vita hivyo endapo Urusi itawaua Wanajeshi wa Ukraine waliosalia katika bandari iliyozingirwa na Warusi ya Bahari Nyeusi ya Mariupol.

April 28, 2022, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa atasafiri hadi Ukraine kukutana na Rais Zelensky wa Ukraine, ambapo anatarajiwa kukutana na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky siku ya Alhamisi, kwa mujibu wa Msemaji wa Umoja wa Mataifa kwa lengo la kurejesha amani kati ya Urusi na Ukraine.

Umoja wa Mataifa umesema kabla ya kwenda Ukraine, Guterres atakutana pia na Rais Vladimir Putin April 26,2022 ambaye atampokea nchini Urusi, ili kufanya mkutano wa kikazi na kupata chakula cha mchana na Waziri wa Mambo ya nje wa Urusi.
Screenshot_20220424-163934_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskyy, ametangaza kuwa leo Jumapili atakutan katika mji Mkuu wa Ukraine na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Antony Blinken pamoja na Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Lloyd Austin.

Zelenskyy ametoa maelezo kidogo kuhusu maandalizi ya mkutano huo huku akisema anatarajia matokeo madhubuti "Sio zawadi tu au aina fulani ya keki tunatarajia vitu maalum na silaha mahususi"

Hii itakuwa ni safari ya kwanza ya Maafisa wa ngazi ya juu wa Marekani kwenda Ukraine tangu vita vilipoanza February mwaka huu.

Itakumbukwa akiwa ziarani Poland mwezi Machi, Blinken aliingia kwa muda mfupi katika ardhi ya Ukraine kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine, mkutano wa mwisho wa Zelenskyy wa ana kwa ana na kiongozi wa Marekani ulikuwa February 19 na Makamu wa Rais Kamala Harris ambao ulifanyika Munich.
Screenshot_20220424-164043_OGInsta%2B.jpg
 
Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky, ametoa tena wito wa kufanya mkutano na Kiongozi wa Urusi Vladimir Putin, katika juhudi za kumaliza vita nchini mwake "Tukutane tuyamalize"

Katika mkutano wake na Waandishi wa Habari, Zelensky amesema haofii kukutana na Putin kama tu kukutana kwao kutasababisha makubaliano ya amani kati ya mataifa hayo mawili.

Rais huyo wa Ukraine amesema tangu mwanzo amekuwa akisisitiza mazungumzo ya amani na Rais Putin.
Screenshot_20220424-164135_OGInsta%2B.jpg
 
Katika kipindi cha miezi miwili ya February na March mwaka huu Watoto wa kike 200 wa Shule za Msingi na 28 wa Shule za Sekondari Mkoani Kigoma wamelazimika Kuacha masomo baada ya kupata mimba wakiwa Shuleni.

Kaimu Afisa Elimu Kigoma David Mwamalasi ameyasema hayo katika uzinduzi wa mashindano ya insha kitaifa kwa Wanafunzi wa Shule za Msingi, mradi utakaotekelezwa na Shirika la World Vision Katika Mikoa 12 Tanzania Bara wenye lengo la Kupinga vitendo vya mimba na ndoa za utotoni Mashuleni.

Katika kipindi cha mwaka 2021 Watoto wa kike 6000 wa Shule za Msingi na 600 wa Sekondari waliripotiwa kuwa Watoro kwasababu mbalimbali ikiwemo mimba, kuolewa na nyinginezo .

Mwamalasi anasema changamoto hizo zimekuwa zikichagizwa na hali ya duni ya maisha na umbali wa miundombinu ya Shule Katika baadhi ya maeneo Mkoani Kigoma.
Screenshot_20220424-164242_OGInsta%2B.jpg
 
Taasisi moja ya utafiti wa kitabibu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imesema maambukizi mapya ugonjwa wa Ebola yamethibitika Kaskazini Magharibi mwa Taifa hilo, haya yanakuja ikiwa ni miezi minne baada ya Taifa hilo kutangaza kumalizika kwa mlipuko wa mwisho wa ugonjwa huo.

Taasisi hiyo imesema Mwanaume wa umri wa miaka 31, alibainika katika mji wa Mbandaka, ambao ni mji mkuu wa Jimbo la Equator, Msemaji wa Wizara ya Afya ya afya ya Taifa hilo amethibitisha ugunduzi huo.

Katika taarifa yake Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema mgonjwa huyo alionesha dalili siku ya Aprili 5 lakini hakufanya jitihada ya kupata matibabu kwa zaidi ya wiki moja na baadaye alilazwa katika kituo cha matibabu ya Ebola juzi Aprili 21 na kufariki dunia siku hiyohiyo.

Mlipuko wa mwisho kutokea nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ulihusisha pia eneo la mashariki ambao ulisababisha maambukizi ya Watu 11 kati ya Oktoba na Desemba na kuwaua sita.
Screenshot_20220424-170226_OGInsta%2B.jpg
 
Wizara ya Afya imetangaza kufanya kampeni ya kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Polio (chanjo ya matone dhidi ya Polio) kwa lengo la kukabiliana na hatariya ugonjwa huo kuingia nchini kutokana na muingiliano mkubwa na Malawi ambao kumetangazwa uwepo wa Polio baada ya Mtoto wa miaka mitatu katika Mji mkuu wa Malawi Lilongwe kugundulika na ugonjwa huo.

"Taarifa hii (ya Mgonjwa wa Polio Malawi) inakuwa ni mara ya kwanza kwa Bara la Afrika kutokea maambukizi baada ya kupita miaka mitano, ambapo ilipelekea ugonjwa wa Polio kutangazwa umetokomezwa katika ukanda wa Afrika mnamo mwezi Agosti, 2020"

"Duniani, ni nchi mbili pekee za Afghanistan na Pakistani ambako ugonjwa wa polio bado haujatokomezwa, hapa Tanzania kwa mara ya
mwisho mgonjwa wa Polio kugundulika ilikuwa mwaka 1996 ambaye alitokea Mkoa wa Mtwara, ilipofika Disemba 2015 Tanzania ilithibitishwa kuwa ni nchi isiyo na ugonjwa wa Polio"

"Malawi imepakana na Tanzania kupitia Mikoa ya Mbeya, Ruvuma, Njombe na Songwe, hii inapelekea kuwepo kwa hatari ya ugonjwa huu kuingia nchini kutokana na muingiliano mkubwa wa kibiashara na shughuli nyingine za kijamii, kampeni ya kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Polio awamu ya kwanza imefanyika katika Mikoa minne ya Mbeya, Njombe, Songwe na Ruvuma na awamu ya pili itafanyika mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuanzia Aprili 28, 2022 hadi 01 Mei 2022"
Screenshot_20220424-170555_OGInsta%2B.jpg
 
Ummy Msika (45), mkazi wa kata ya Bomambuzi manispaa ya Moshi Mkoa wa Kilimanjaro amepata madhara mwilini baada ya rafiki yake kudaiwa kumpa maji ya uponyaji ‘upako’.

Msika aliyelazwa katika hospitali ya rufaa ya Mkoa ya Mawenzi amesema wakati akiumwa mguu rafiki yake alimwambia atampa maji hayo ya uponyaji kwa ajili ya kunywa na kupaka.

Ameieleza Mwananchi Digital leo Jumapili kuwa baada ya kunywa maji hayo Aprili mosi, 2022 kutibu tatizo lake la mguu alianza kuumwa na kupoteza hamu ya kula, kuanza kuwashwa sehemu za siri na kwamba kila kukicha tatizo lilikuwa likizidi na hali yake kuwa mbaya na ndugu zake walimchukua na kumpeleka hospitali.

Naye mmoja wa madaktari anayemhudumia mwanamke huyo kwa sharti la kutotajwa jina lake amesema wanaendelea kumpatia matibabu kadri ya uwezo wao.
Screenshot_20220424-170728_OGInsta%2B.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom