Makapuku Forum

Makapuku Forum

Watanzania wametakiwa kuendelea kuyaenzi mema aliyoyafanya Rais wa awamu ya tano, hayati John Magufuli wakati wa uhai wake.

Wito huo umetolewa na Askofu wa Afican Inland Church (AIC) Jimbo la Geita, Musa Magwesela leo Alhamisi Machi 17, 2022 kwenye uwanja wa Magufuli Chato wakati wa kuadhimisha kumbukizi ya mwaka mmoja ya kifo cha hayati Magufuli akisema hayati Magufuli ameacha alama ambayo haitafutika mioyoni mwa Watanzania.
#mwaka1wajpm
Screenshot_20220317-133527_Instagram.jpg
 
Rais wa Marekani, Joe Biden amemuita Rais wa Russia, Vladimir Putin mhalifu wa kivita
Screenshot_20220317-133709_Instagram.jpg
 
Baadhi ya wasomi wamesema wanaamini Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Nehemia Mchechu aliliboresha shirika hilo na kuendeleza miradi inayosuasua.

Mchechu, aliyewahi kushika wadhifa huo kwenye shirika hilo aliondolewa Juni 20 mwaka 2018 na nafasi yake kuchukuliwa na Dk Maulid Banyani, aliyeondolewa kwenye wadhifa huo Machi, 14, 2022.

Baadhi ya wasomi waliliambia Mwananchi kuwa uteuzi huo utalipa uhai tena shirika hilo ambalo miradi mingi iliyoanzishwa wakati wa utawala wa Mchechu inasuasua.
Screenshot_20220317-133826_Instagram.jpg
 
Ndani ya Jiji la Dar es Salaam kuna mnyukano. Ni baina ya aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na mfanyabiashara Ghalib Said Mohammed (GSM). Wanagombea ardhi.

Makonda analalamika kuwa GSM anataka kumdhulumu mali yake. Wakili wa GSM, Alex Mgongolwa akatoa ushahidi wa umiliki wa ardhi yenye mgogoro. Kwamba ni mali halali ya mteja wake.

Nani mmiliki? Hilo jawabu litajulikana mbele ya sheria. Msingi wa makala hii ni kumtazama Makonda anayelalamika kuwa anadhulumiwa na mfanyabiashara aliyemwita tapeli. Hana nguvu!

Ikikupendeza, rudi nyuma miaka mitatu tu. Je, ungedhani yule Makonda, mkuu wa mkoa, angekuwa huyu anayesema yupo tayari kupigwa risasi lakini si kushuhudia mali yake ikichukuliwa?

Yule Makonda tishio, mpaka Serikali ya Marekani ikatoa taarifa ya kumpiga marufuku kukanyaga kwenye taifa hilo, kwa sababu waliyoitaja kwamba ni kudhulumu haki ya watu wengine kuishi, ndio huyu asiye na nguvu zozote?
Screenshot_20220317-133938_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom