Makapuku Forum

Makapuku Forum

Screenshot_20220315-051215_Opera%20Mini.jpg
Screenshot_20220315-051302_Opera%20Mini.jpg
 
UEFA CHAMPIONS LEAGUE
.
Man United inaingia kwenye mchezo huu ikijiamini kwa sababu ilishapata sare kwenye mechi ya kwanza ugenini, lakini pia imetoka kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Spurs kwenye mchezo uliopita.
.
Mbali ya yote, inaingia ikiwa na muuaji wa Atletico Madrid, Cristiano Ronaldo ambaye ana rekodi ya kuifunga timu hiyo mabao mengi zaidi alipokuwa Real Madrid na Juventus.
Screenshot_20220315-132954_Instagram.jpg
 
KIIZA: MABEKI WANAKAMIA SANA
.
Baada ya kuitungua Simba na kufanikiwa kuipa pointi tatu timu yake mshambuliaji wa Kagera Sugar, Hamis Kiiza amelia na kukamiwa na mabeki wa timu pinzani katika Ligi Kuu Bara, huku akikiri kuwa ligi msimu huu ni ngumu.
.
“Tangu niwafunge Simba wapinzani wananikamia, lakini wanasahau Uwepo wangu kwenye kikosi sio kigezo cha kufanya kila kitu, nisipofunga kuna mwingine atafunga hivyo kikubwa mchango wangu uonekane na sio kukamilisha tu idadi ya namba ya wachezaji.”

......……..
Screenshot_20220315-133733_Instagram.jpg
 
Uwanja wa Deva unaotumiwa na klabu ya Chester FC ni uwanja pekee wa klabu Duniani ambao unapatikana katika nchi mbili tofauti, uwanja huu una uwezo wa kuingiza watazamaji 6000 na upo mpakani mwa nchi ya England na nchi ya Wales, eneo la kuchezea na majukwaa yapo Wales wakati ofisi za klabu zipo nchini England.
Screenshot_20220315-135550_Instagram.jpg
 
Anaitwa Nicolas Jover alijiunga na Arsenal, Julai 2021 ni Kocha wa mipira iliyokufa (faulo na kona)

Tangu amejiunga na Arsenal zimepigwa kona 121 dhidi yao na hawajaruhusu bao lolote Arsenal lililotokana na kona

Screenshot_20220315-135711_Instagram.jpg
 
Real Madrid wamefunga mabao 10 katika mechi zao tatu za mwisho baada ya jana kumuadhibu Mallorca 3-0

Wanajikita kileleni kwa alama zao 66 huku Sevilla anaemfuata ana alama 56

Weekend hii ni El Classico! REAL MADRID VS BARCELONA
Screenshot_20220315-140105_Instagram.jpg
 
Baada ya sare ya jana, Manchester City dhidi ya Crystal Palace inamfanya Liverpool kuendelea kusogea kama atashinda mchezo wake

Liverpool ataachwa alama moja pekee kama atashinda mechi yake

Pep vs Klopp another show to watch
Screenshot_20220315-140211_Instagram.jpg
 
Mpira wa Afrika una mambo mengi sana, ndio maana kwasasa timu nyingi zimeacha kulalamika bali kucheza mpira na kuwekeza kwenye mpira

Simba wanafanyiwa mengi sana ugenini ila wao wamechagua kuacha kulalamika na kuwekeza kwenye mpira, wakipageuza kwa Mkapa sehemu ngumu mtu kucheza

Kwa Madiba wale Mamelodi Sundowns walizuia mpaka Bus la Al Ahly lisipite, wanajua sio sahihi ila ndio fitna za soka la Afrika, kushinda mchezo haiwi tu ndani ya uwanja

Kabla ya kulalama na kuisema vibaya Simba ambayo haihusiki na maamuzi ya Marefa, jaribu kuvuta picha nao huwa wanafanyiwa mangapi nje ya nchi? Ni vile tu wameacha kulalama na kuamua kucheza mpira
Screenshot_20220315-140320_Instagram.jpg
 
Msemaji wa ofisi ya Waziri Mkuu wa Uingereza, ametoa taarifa ya kusikitishwa na kitendo cha Mashabiki wa Chelsea kuliimba jina la Roman Abramovich na kuonesha wapo sambamba nae

Mashabiki wa Chelsea wamekuwa wakiipinga serikali waziwazi, huku wakitaja jina la Roman kwenye mechi ya pili mfululizo
Screenshot_20220315-140501_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom