Makapuku Forum

Makapuku Forum

Baadhi ya wasomi wamesema tabia ya baadhi ya wazazi kuwapeleka watoto wao shule za bweni za msingi kuna hasara nyingi kuliko faida.

Wakizungumza na Mwananchi, wasomi hao wamesema kuwa mwalimu pekee hatoshi kumjenga mtoto kimaisha
Walisema itakuwa bora kama watoto hao wakipelekwa shule za bweni wanapoingia kidato cha kwanza kwa sababu wanakuwa na akili za kujitambua.

Muhanyi Nkoronko ambaye ni mtafiti wa masuala ya elimu alisema watoto wadogo ni vyema waachwe chini ya uangalizi wa wazazi ili wajengwe kimaadili na kuelekezwa nini wanapaswa kufanya katika umri wao.

“Wazazi wengi wanapeleka watoto bwenini kwa kisingizio cha kukosa muda wa kukaa na watoto kutokana na kazi nyingi na wengine eti wanataka wapate muda zaidi wa kusoma lakini hasara ni nyingi zitakazowapata huko ikiwemo watoto kutokuwa wanaeleweka, kupata malezi duni na kujifunza tabia ambazo hazistahili,” amesema Nkoronko

Mwanasaikolojia Seby Wisdom amesema umri wa miaka mitano hadi tisa kwa mtoto huutumia katika kuangalia watu wanaomzunguka wanafanya nini na kuiga baadhi ya tabia zilizozoeleka

“Katika mazingira hayo ikiwa ni nyumbani na mama na baba wanaongea vizuri anajua ndiyo njia sahihi ya kuzungumza na kama wanaongea vinginevyo inakuwa sawa na hilo,” anasema Wisdom.
Screenshot_20220207-133659_Instagram.jpg
 
Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe akiwa anasoma kitabu akisubiria kesi inayomkabili na wenzake watatu kuanza ndani ya Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa Rushwa na Uhujumi Uchumi leo jijini Dar es Salaam.
Screenshot_20220207-133811_Instagram.jpg
 
BODI YA LIGI: KLABU HAZIJAPATA CHOCHOTE KUTOKA GSM
.
Mwenyekiti Bodi ya Ligi Steven Mguto amesema:” "Nikiri kwamba klabu hazikupata chochote tangu tuliposaini mkataba. Mpaka sasa klabu zimeitangaza GSM kwa miezi mitatu hivyo tunasubiri wanasheria wetu walipitie hilo tuone kisheria pia limekaaje,"
Screenshot_20220208-041939_Instagram.jpg
 
Makocha wa wazawa wa Afrika wamefanikiwa kuchukua mataji sita (6) kati ya mataji tisa (9) ya AFCON yaliyopita.

2006: Hassan Shehata
2008: Hassan Shehata
2010: Hassan Shehata
2012: Herve Renard
2013: Stephen Keshi
2015: Herve Renard
2017: Hugo Broos
2019: Djamel Belmadi
2021: Aliou Cissé
Screenshot_20220208-042510_Instagram.jpg
 
Kwa mujibu wa Allan Chonjo, Afisa Biashara Mkuu GSM, amesema GSM ilishawishika sana na TFF pamoja na Bodi ya Ligi na kuridhia kuwa mdhamini mwenza wa Ligi Kuu ili kukuza sekta ya Mpira wa Miguu hapa nchini pamoja na michezo kwa ujumla lakini hili halikuenda kama lilivyokusudiwa.

Chonjo amesema, hayajawa maamuzi rahisi kwa kampuni ya GSM kwani wanatambua ya kuwa vipo baadhi ya vilabu vya mpira vitakavyoumizwa pamoja na wadau mbalimbali na hatua hii na wala haikuwa dhamira yao kufikia uamuzi huo mgumu.
Screenshot_20220208-045012_Instagram.jpg
 
BODI YA LIGI: KLABU HAZIJAPATA CHOCHOTE KUTOKA GSM
.
Mwenyekiti Bodi ya Ligi Steven Mguto amesema:” "Nikiri kwamba klabu hazikupata chochote tangu tuliposaini mkataba. Mpaka sasa klabu zimeitangaza GSM kwa miezi mitatu hivyo tunasubiri wanasheria wetu walipitie hilo tuone kisheria pia limekaaje," View attachment 2112004
Hii nchi ngumu jaman
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom