Makapuku Forum

Makapuku Forum

Wakati nipo Cameroon kwenye michuano ya CAF, nimebahatika kukutana na wadau mbalimbali wa mpira wa miguu, tumekuwa na vikao rasmi na visivyo rasmi

Nimepata bahati ya kukutana na kuongea na Rais wa CAF Patrice Motsepe, nimeiona dhamira yake ya kuhakikisha tunakuwa na African super cup, ili kufanikiwa inahitaji msuli kutoka kwa wadau wa soka ambao watawezesha super cup

Ila inasisitiza mazingira bora ya uendeshwaji wa soka Afrika ili wadau watakaoingia nao wanufaike na uwepo wa super cup

Ukweli ni kwamba wadau ndio kama NBC, AZAM na GSM, Jana nimesoma sababu zalizotolewa na GSM kuvunja mkataba zipo 8, na hawajazunguka sana wameziorodhesha zote

Kwa walichokiainisha tunahitaji kuanza upya, hakuna kampuni au mdau atakuja kuwekeza kwenye soka letu Tanzania kwa style hii

Hata waliopo pengine wana yao lakini wanavumilia kama ndoa, Ila baada ya waraka wa GSM kutoka jana, image ya uendeshwaji wa soka la Tanzania mbele ya watu ambao wangetamani kuwekeza is not the same anymore, wadau tukae chini tujenge soka letu Tanzania

Shaffih Dauda
Screenshot_20220208-172957_Instagram.jpg
 
Ukiachana na Fainali za AFCON 2021 nchini Cameroon, Rais wa CAF Patrice Motsepe alikutana na wawakilishi wa baadhi ya vilabu kwa ajili ya kuzungumzanao kuhusu mchakato wa African Super League.

Kwa hiyo kwa ngazi ya vilabu kutakuwa na mashindano matatu African Super League, Champions League itakuwa inaitwa Champions Club na Confederation Cup.

Lengo mama ni zuri kwamba Ligi hii itaenda kuvifaidisha vilabu kwa sababu itakuwa na fedha nyingi ambazo zitafanya vilabu viweze kujikimu na kufanya shughuli mbalimbali za kujiendesha.

Changamoto ambazo ziliibuliwa ni pamoja na namna ya uendeshaji wa hiyo Ligi yenyewe. Afrika kuna changamoto nyingi, ukiangalia kwa sasa kwenye mashindano ya CAF Champions League na CAF Confederation Cup vilabu vingi vilalamikia gharama za usafiri kutoka sehemu moja kwenda nyingine.

Al Ahly wakaja na hoja kwamba, CAF inapokuja na shindano jingine wakati CAF Champions League na CAF Confederation Cup zitaendelea kuwepo vilabu vitawezaje kumudu kwa sababu tayari kwenye nchi zao kuna Ligi na mashindano mengine vinashirjki.

Wakashauri ufanyike utafiti kwanza kabla ya kufanya maamuzi ili kupata hibu ambalo litakuwa na faida ili badae kusiwe na mtu wa kujuta.

Ahly wakaja na hoja nyingine kwamba, kwenye msimu mmoja wanawakosa wachezaji wao kwa siku 90 [wawanakuwa nje ya klabu]. Wanaitwa kwenye timu zao za taifa, wakatoa mfano sasa hivi klabu yao ipo kwenye mashindano ya FIFA Club World Cup lakini wachezaji wao wengi wapo kwenye timu zao za Taifa hali inayosababisha washindwe kucheza katika ubora wao.

Wakasema kwenye Ligi yao wanafanya vibaya kwa sababu wachezaji wengi hawapo kwenye klabu. Sasa ukiongeza tena shindano lingine huku ukitegemea wachezaji walewale.

Ahly wanasema licha ya kuwa mabingwa wa CAF Champions League mara kadhaa lakini gharama wanayoitumia ni kubwa, kitu ambacho huwa kinawalipa ni ushiriki wao kwenye michuano ya FIFA Club World Cup ambako ukishinda mechi na kwenda hatua inayofuata unakunja mkwanja mrefu.
Screenshot_20220208-173142_Instagram.jpg
 
TFF NI NYUMBA YA KUPANGA?

TFF ni taasisi yenye kusimamia maslahi ya mpira wetu, TFF sio nyumba ya kupanga ambayo Baba mwenye nyumba aseme hiki tufanye hiki tusifanye hata kama hakina maana

TFF sio nyumba ya kupanga ambayo Mwenye nyumba aseme leo nyama hapana, aseme sitaki Mtu abandike picha ukutani na kuhojiwa kusiwepo! TFF ni mali yetu wote

Shida kubwa iliyopo Shirikisho ni mentality ya nyumba ya kupanga, wakisema kitu sisi Wapangaji tusihoji kwakuwa hatukuchangia tofari wala madirisha, wala hatukutoa mia ya uwanja, SIO KWELI

Wakati mmesaini mikataba yote klabu hawajui kitu zaidi ya kupelekewa figure na kuambiwa watekeleze, hakuna kuhoji bali kutekeleza, huo sio uongozi bali DICTATORSHIP

Klabu zimeenda kutekeleza kitu ambacho hawajui msingi wake, ndani ya miaka miwili wadhamini wawili wanaondoka bila fidia kwa klabu, shida kubwa ikiwa ni ninyi TFF na Mentality za BABA MWENYE NYUMBA

TPLB ipo kwa ajili ya maslahi ya klabu zote ila mmeitoa meno, mmeifanya kama kamati na ninyi mmejipa majukumu yote, TPLB haina Viongozi bali CEREMONIAL LEADERS, Kila kitu kinafanyika Karume

Matokeo yake ndio haya! Mguto hana makosa, Kasongo hana makosa tena wasipewe jumba bovu tatizo lote ni ninyi hapo KARUME, ndio maana siku zote huwa nawaambia bodi iwe huru isajiliwe kama Kampuni

Kila siku agenda lakini mpo kwenye total failure! Nyie msimamie mpira, nyie msimamie timu za taifa, nyie msimamie Ligi, Guys muelewe DIVISION OF POWER haikwepeki, mjitathimini ikiwemo hata kujiuzulu sio kwa ubaya

Kila mkataba kisheria ambao TPLB atasaini ninyi mnapata 10% kisheria, tatizo nini mtake kila kitu mfanye ninyi??? Kuna siri gani ambayo hatuijui

Whenever we are given an oppurtunity to elect leaders, we are given a blank cheque! We elect hyenas to take care of goats

When DIGALA speaks????_______
Screenshot_20220208-173357_Instagram.jpg
 
Afisa wa Shirikisho la Tanzania Jacqueline Kamwamu ameifuta kesi aliyomshtaki Mtendaji Mkuu wa klabu ya Simba Barbara Gonzalez

Jacqueline na Barbara kwa pamoja wamekubaliana kuifuta kesi hiyo kwa maslahi ya mpira wa miguu

Katika mazungumzo baina yao Jacqueline ameridhia pasina ushawishi kufuta kesi hiyo na kwamba wawili hao wanatoka kwenye taasisi ambazo zinategemeana hivyo hakuna sababu ya kuendelea na kesi

Taarifa zinaeleza kuwa Barbara nae amefurahishwa na auamuzi huo na kusema kwamba maamuzi hayo yamezingatia maslahi mapana ya mpira wa miguu na kama haitoshi yamezingatia uhusiano chanya baina ya TFF na Mwanachana wake Simba Sports Club
Screenshot_20220208-173142_Instagram.jpg
 
MURO: WASEMAJI YANGA WASIKURUPUKE KUONEKANA VITUKO
.
“Inashangaza kumsikia Afisa Habari wa klabu akielezea baadhi ya mambo ya msingi ya timu kama shabiki au kuongelea masuala ya ufundi kama kocha wakati kazi hizo si zao.
.
“Hata kama klabu zina utaratibu wa kuwapa fursa ya kuzungumza na kutoa ufafanuzi wa mambo yanayoulizwa na waandishi wa habari, lakini wamekuwa wakienda mbali na mipaka yao.
.
“Ifike wakati wasemaji wa Yanga waonyeshe ukomavu katika kazi wanazopewa, wasikurupuke na kuonekana vituko.”
Screenshot_20220208-174859_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom