Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,971
"Ni imani yangu kwamba hadi kufikia January 15,2022 madarasa yatakamilika kama Waziri Ummy alivyosema na January 17,2022 Watoto wetu waingie madarasani, na naamini madarasa yatakabidhiwa bila kuwa na harufu ya rangi ili wasije kupaliwa tukazalisha matatizo mengine"
"Niwashukuru Viongozi wote kwa usimamizi mzuri uliofanyika kwenye mradi huu, na nawashukuru Wenyeviti wa CCM kwa kusimama na kutetea Mkopo ulioleta maendeleo, walipotokea wa kuhoji mlisimama mkajibu mkijua kwamba kinachofanyika ni utekelezaji wa Ilani, Ilani ile wenyewe ni nyinyi na sasa mna mambo ya kwenda kifua mbele kwa Wananchi kuwaambia Chama kimefanya hiki"
"Niwashukuru wote wengine waliokuwa wanajibu kwenye mitandao n.k, Gavana wa Benki Kuu na Timu yake wakakaa kwenye TV na kufanya ufafanuzi mzuri sana kuhusu mikopo, uwezo wa kukopa, deni tulilonalo na uwezo wa kulipa" ———Rais Samia, Ikulu Dar es salaam leo
"Niwashukuru Viongozi wote kwa usimamizi mzuri uliofanyika kwenye mradi huu, na nawashukuru Wenyeviti wa CCM kwa kusimama na kutetea Mkopo ulioleta maendeleo, walipotokea wa kuhoji mlisimama mkajibu mkijua kwamba kinachofanyika ni utekelezaji wa Ilani, Ilani ile wenyewe ni nyinyi na sasa mna mambo ya kwenda kifua mbele kwa Wananchi kuwaambia Chama kimefanya hiki"
"Niwashukuru wote wengine waliokuwa wanajibu kwenye mitandao n.k, Gavana wa Benki Kuu na Timu yake wakakaa kwenye TV na kufanya ufafanuzi mzuri sana kuhusu mikopo, uwezo wa kukopa, deni tulilonalo na uwezo wa kulipa" ———Rais Samia, Ikulu Dar es salaam leo