Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,077
- 464,004

Farhan JrCLATOUS CHAMA UPDATE|
Taarifa za kuwa Simba wamemalizana na Wakala wa Chama Jijini Lusaka Zambia sio za kweli na wala hawakukutana
Chama Bado ni Mchezaji wa Berkane kwasasa, hivyo Mawasiliano ya timu yoyote inayomtaka Chama ni lazima yapitie kwenye klabu yake
Ni klabu moja pekee mpaka sasa iliyojaribu kuhitaji huduma ya Chama kupitia kwa Wakala na klabu yake moja kwa moja ila Mchezaji huyo hayupo tayari kujiunga nao
Chama anaendelea kuheshimu mkataba wake na suala lake la kutaka kuvunja mkataba kwa makubaliano ya pande mbili ameendelea kulifanya kwa ufasaha mpaka sasa
Chama Bado ana Mawasiliano na Simba ya karibu na tayari aliwaelezea Nia yake ya kurejea nchini na wao wamebariki hilo kama nilivyosema mwanzo
Ila dau la Chama sokoni ni kubwa hivyo Kuna kete mbili tu za kusukuma, kete ya kwanza ni mutual agreements kisha Chama awe huru ajiunge na Simba ama kete ya pili wamchukue kwa mkopo
Mpaka sasa kete ya kuvunja mkataba kwa makubaliano ya pande mbili yapo vizuri sana ijapo ugumu upo kidogo kwa upande wa Berkane haswa Viongozi ambao wanamtazama Chama kwa picha kubwa sana
Simba wanajitahidi sana kukaa mbali na hilo Ili lisiwatibue Waarabu kuhisi Wana mkono nalo, Chama pia anajitahidi kulifanya private
Akili na moyo wake ni Simba pekee, only Simba is the destination kwa taarifa za Watu wake wa karibu sana! It is going to happen and it will surely happen

