Pablo aende kwa kuiheshimu Yanga, pamoja na kwamba mechi za watani huwa haitabiliki lakini kuna nyakati lazima uheshimu form ya mpinzani wako kwa wakati huo.
Bahati nzuri kocha wa Simba ana machaguo mengi sana lakini lazima aende na tahadhari akijua Yanga ipo kwenye kiwango bora na ina wachezaji wazuri sana hasa katika eneo la kiungo na wanaweza kubadilika kulingana na mpinzani amekuja vipi.
Nadhani sehemu ambazo zitakuwa na mapambano ni sehemu za pembeni ya uwanja. Ndio sehemu ambayo hizi timu mbili zimekuwa na watu washindani zaidi.
Sioni utofauti wa madaraja [class] wa wachezaji wa Simba na Yanga isipokuwa ni viwango [form] ya wakati huu.
Yanga inafaida kwa kuwa wachezaji wake wapo kwenye form kwa wakati huu. Wachezaji wa Simba wanatafuta form yao ili kurudi walivyokuwa misimu mitatu iliyopita.
Pembeni Yanga inamtumia Djuma Shabani, Moloko, Shomari Kibwana au Fari sehemu ambazo kutakuwa na upinzani kutoka kwa Mohamed Hussein na Kapombe sehemu ambazo pia Simba inategemea hukohuko.
Ambaye atafanikiwa kwenye maeneo hayo ya pemebeni ndio naona italeta tofauti ya mchezo. Eneo la katikati Yanga wana faida ya kulimiliki lakini bado wanategemea kupeleka mipira pembeni.
Kuelekea mchezo wa KariakooDerb kwangu Yanga ni favourites na sababu zipo mezani, ukizichambua unaona wazi kabisa Yanga ni favourites kwenye huu mchezo.
- Yanga inaongoza msimamo wa Ligi [pointi 19]
- Yanga imefunga magoli mengi zaidi kuliko Simba [Yanga imefunga magoli 12, Simba imefunga magoli nane].
- Kocha wa Simba Pablo Franco bado hajapata kikosi cha kwanza anachokiamini
Katika mechi kadhaa ambazo tayari Pablo ameiongoza Simba ametumia mifumo tofautitofauti na wachezaji tofauti, vs Ruvu 4-4-2, vs Geita Gold 4-3-3, vs Red Arrows 4-2-3-1.
Hata mashabiki wa Simba sasa hivi ukiwaambia wakutajie kikosi cha Simba cha Kocha Pablo Franco watatofautiana.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.