Makapuku Forum

'Tumeumizwa sana' ni kauli ya mmoja wa makomandoo aliyekuwa mlangoni kuzuia mashabiki kuingia uwanjani kushuhudia mazoezi ya Yanga yanayoendelea muda huu katika uwanja wa Sokoine Mbeya.

Yanga kesho itakuwa uwanjani saa 10:00 kumenyana na Mbeya Kwanza katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC.
Screenshot_20211129-195421_Instagram.jpg
 
Ralph Rangnick licha ya kuwa ni Kocha Mkuu wa Manchester United lakini pia amepewa nafasi ya kusaka wachezaji (vipaji) kwa ajili ya Manchester United

Katika eneo hilo yeye ni bingwa, anasifika kwa jicho kali la kung'amua vipaji na kuvigeuza kuwa Mastaa wa dunia
Screenshot_20211129-195550_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Mpira wa miguu ni zaidi ya kazi bali maisha halisi ya watu duniani kote! Huwa napenda kutumia msemo maarufu wa "One thing about football is not about football"

Lionel Messi alivyokuwa Barcelona alifunga bao kisha akavua jezi ya Barcelona na ndani alivaa jezi ya Newell Old Boys ambayo Diego Maradano alicheza

Alifanya hivyo kutuma salaam zake za pole na heshma yake kwa Maradona ambaye ni Gwiji wa soka duniani, lakini hiyo haikuwa stori kubwa

Stori ni hiyo jezi ya Newell Old Boys! Imetengenezwa na ADIDAS na Mdhamini wake ni YAMAHA, Kampuni ya vyombo vya usafiri kutoka Japan

Kumbuka: Barcelona wanadhaminiwa na NIKE ambao ni washindani na ADIDAS, isitoshe Barcelona wana udhamini wa RAKUTEN ni Kampuni ya vifaa vya umeme na mauzo mtandaoni

Kwakuwa mpira wa miguu ni Mchezo wa kiungwana na ni maisha halisi! Licha ya kwamba Messi ni kama alipiga tangazo wakati anatoa heshma yake kwa Maradona ila si klabu, si NIKE wala RAKUTEN ambao walipiga kelele

Kuna muda maisha ni muhimu zaidi kuliko pesa na biashara, kuna wakati heshma ya mpira wa miguu ni bora zaidi kuliko pesa na biashara, hii ndio maana na THE GAME IS FAIR PLAY

Screenshot_20211129-195819_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom