Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais wa Afrika Kusini amelaani marufuku ya kusafiri iliyowekwa dhidi ya Nchi yake na Nchi nyingine Jirani za Afrika kutokana na aina mpya ya kirusi cha Corona Omicron huku akisema hatua hiyo inavuruga uchumi wa Nchi hizo.

Ramaphosa amesema amesikitishwa sana na hatua hiyo na kutaka marufuku hiyo kuondolewa haraka.

Ramaphosa amesema kwa Nchi tajiri badala ya kuweka marufuku wanapaswa kusaidia kuinua uchumi wa Nchi zenye kirusi hicho kipya na kuwapa chanjo za kutosha, Uingereza, EU na Marekani ni miongoni mwa walioweka marufuku ya kusafiri.
Screenshot_20211129-170559_Instagram.jpg
 
Tunarudi tulikotoka? hakuna anaepinga kwamba corona imeitesa dunia mpaka Nchi kadhaa kuamua kufunga mipaka yake kwa muda mrefu na kuiachia juzijuzi tu hapa ila kirusi kipya kilichogundulika South Africa wiki iliyopita kimezua kizaazaa na hadi sasa kuna Nchi 44 zimetangaza zuio dhidi ya Nchi za Afrika ikiwemo South Africa.

Japan yenyewe haijatangaza zuio kwa Nchi hizo za Afrika pekee bali kwa Nchi zote ambapo zuio hili la muda halitoruhusu Msafiri kutoka Nchi yoyote duniani kuingia Japan kuanzia kesho November 30 hadi huku Waziri Mkuu Fumio Kishida akisema ni dharura ya kujikinga na balaa kubwa zaidi.

Kishida hajasema zuio hili litakwenda hadi lini lakini amesema mmoja kati ya Watu 32 walioingia Japan wakitokea kwenye Nchi 9 za Afrika zilizotajwa kuwa na kirusi kipya kiitwacho ‘omicron’ amekutwa na corona lakini haijatajwa kama ni corona ya kirusi hiki kipya.
Screenshot_20211129-170715_Instagram.jpg
 
Rwanda imetangaza kusitisha safari zake za ndege kwenda Johannesburg na Cape Town South Africa, Lusaka Zambia na Harare Zimbabwe na kurejesha masharti ya karantini ya siku 7 kwa wote wanaotoka kwenye Nchi hizi.

Rwanda imeungana na Nchi nyingine zaidi ya 15 zikiwemo Uingereza na Marekani kuzuia Wasafiri kutoka Nchi hizo kutokana na kirusi kipya hatari cha corona ambacho kimegundulika South Africa hivi karibuni.
Screenshot_20211129-170847_Instagram.jpg
 
Mbunge wa Jimbo la Muheza Mkoani Tanga, Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA amesema atahakikisha vitongoji 210 kati ya 494 vya halmashauri hiyo ambavyo havijafikiwa na umeme vinafikiwa ili viweze kuondokana na changamoto ya giza.
Screenshot_20211129-171008_Instagram.jpg
 
Mwanamfalme Charles wa Uingereza akiwasili katika visiwa vya Barbados ambapo nchi hiyo inajiandaa kumuondoa Malkia Elizabeth kama mkuu wa nchi.

Katika sherehe za kuitangaza Barbados kama Jamhuri huru zitakazofanyika leo usiku, zitajumuisha gwaride la kijeshi na sherehe za kumuapisha Gavana Mkuu wa sasa Sandra Mason kuwa Rais.
Screenshot_20211129-171137_Instagram.jpg
 
Mahakama Kuu Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi imekubali pingamizi la mawakili wa Serikali la kutopokea barua kama kielelezo cha ushahidi wa upande wa utetezi katika kesi ndogo ndani ya kesi kubwa ya ugaidi inayomkabili mwenyeki wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake watatu.

Uamuzi huo umetolewa leo Jumatatu Novemba 29, 2021 na Jaji Joachim Tiganga na kueleza kuwa mshtakiwa huyo wa Mohamed Ling'wenya hajaweza kuieleza mahakama ni kwa nini barua hiyo inamhuri wa naibu msajili.

Jaji ameeleza kuwa katika mazingira hayo mahakama imeshindwa kuelewa kama hiyo barua aliyotaka kuitoa ndio hiyo iliyopelekwa kwa RPC.
Screenshot_20211129-171248_Instagram.jpg
 
“Tulipofika uwanjani tuligundua kuwa kutokana na hali ya hewa nyasi zimejaa maji ilibidi tuingie kwa mpango mwingine, kwenye soka muda mwingi sio tu mpango ulionao bali ni wewe kuwa na mipango mbadala."
.
"Tulijua jinsi walivyopaswa kucheza na hali hii ya hali ya hewa ilikuwa nzuri kwa mtindo wao wa uchezaji. Ilikuwa mbaya kwa mtindo wetu wa uchezaji lakini hata hivyo tulibadilika haraka. Tulionyesha ujasiri, tulipambana tangu mwanzo hadi mwisho. Tulifunga mabao matatu na nadhani tulistahili kufunga hata manne au matano. Hawakutengeneza nafasi, labda moja tu.

- Kocha wa Simba, Pablo Martin.

Nyieee mmemsikia kocha wetu
Screenshot_20211129-172755_Instagram.jpg
 
MORRIS KURUDI UWANJANI DIRISHA DOGO
.
Mchezaji mkongwe wa Azam FC Aggrey Morris, amesema anatarajiwa kurejea uwanjani kwenye dirisha dogo la usajili unaotarajiwa kuanza Disemba 15 hadi Januari.
.
Morris ni miongoni mwa wachezaji watatu waliosimamishwa na klabu yao hivi karibuni kwa muda usiojulikana ikielezwa sababu ni utovu wa nidhamu. Wengine ni Mudathir Yahya na Abubakari Salum ‘Sure boy’.
.
Akizungumza na SA kuhusu kurejea kwake uwanjani, Morris aesema anatarajia kurudi kwenye dirisha dogo ila hakutaka kusema ni klabu gani.
Screenshot_20211129-172948_Instagram.jpg
 
Bosi GSM kusajili Mashine mbili, Ataka Vikombe !!
.
Taarifa za ndani Yanga inataka kuongeza mashine mbili za maana katika dirisha dogo la usajli na tayari tajiri wao Ghalib Mohamed majina ya nyota hao yamefika katika meza yake kupitia kikao kilichofanyika na kocha Nabi.
.
Nafasi hizo mbili ambazo zinatakiwa kuongezwa ni mshambuliaji wa kati na kiungo mchezeshaji huku pia wanaendelea kupiga hesabu za kuongeza kipa mmoja mzawa.
.
SA tunafahamu kwamba katika kikao hicho Ghalib alisisitiza kwamba msimu huu anataka kuona makombe mawili, lile la Ligi Kuu na la FA yanatua Jangwani.
Screenshot_20211129-173114_Instagram.jpg
 
Geita yaifuata Simba mapema
.
Wakati Simba jana ikiwa Uwanja wa Mkapa ikicheza mechi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Red Arrows ya Zambia. Geita Gold FC ilikuwa Kwenye basi ikiwafuata Wekundu wa Msimbazi hao.
.
Geita imekuja Dar es Salaam kuweka kambi ambapo itacheza mechi mbili za ligi, Desemba 1 dhidi ya Simba na Desemba 5 dhidi ya KMC.
.
Akizungumzia maandalizi ya mchezo huo, kaimu kocha mkuu wa chama hilo, Fred Felix Minziro ameeleza kuwa tayari maandalizi ya mwanzo yamemalizika na sasa wanakuja Dar es Salaam Kumalizia Kisha kukipiga na Simba.
Screenshot_20211129-173312_Instagram.jpg
 
Farhan Jr

Clatous Chama hajatumika na Kocha Ibenge kwenye kikosi cha RS Berkane kwa michezo minne hivi sasa

Sio kweli kwamba Chama ni majeruhi bali kwasasa Kocha ameanza kumtoa kwenye mipango yake nchini Morocco

Clatous Chama tayari amewasilisha maombi rasmi ya kuondoka kikosini hapo na mchakato unaendelea kama nilivyoarifu hapo awali

Chama anaweka kificho kikubwa juu ya dili hili na hayupo tayari kutoa taarifa zake binafsi kwakuwa bado ana mkataba na Berkane, huku akihitaji kuagana kwa amani kabisa

Mchakato wa kuvunja mkataba unahitaji utulivu Mkubwa na kuheshimu kila hatua na kuendelea kuzingatia ratiba za timu, Chama amekuwa hivyo tangu siku ya kwanza

It's Happening

Screenshot_20211129-173430_Instagram.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom