Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,974



Mikono ya kihamu ya Farhan Jr
Huwa tunasema barani Ulaya na duniani kote wenzetu wapo mbali na hakuna Afisa Habari anaepiga kelele, well tupo sahihi ila kuna kitu yatupasa tukifahamu
Sio kweli kwamba klabu duniani zinaendeshwa kwa makaratasi tu nikimaanisha Press Release pekee bali kuna watu maalum wenye vitengo maalum kwa ajili ya Mashabiki na Wanachama
Miaka kadhaa nyuma Mwanafunzi kutoka chuo cha Rotterdam School of Management, anaitwa Michael Vantoff, alifanya tafiti yakinifu kuhusu mtu anaitwa MKURUGENZI WA MASHABIKI au Meneja wa Mashabiki
Alifanya tafiti yake kwenye klabu za EPL hapo nchini England, ambazo karibia zote zina Mtu wa aina hiyo, ambae kazi yake kubwa ni kuwapa wajumbe wa bodi na Wakurugenzi hali halisi ya Mashabiki huko nje
Huyu ndie Muhamasishaji wa Mashabiki wote, huyu ndie anatumika mpaka kubalance upepo wa kimtandao (social Networks) na kuibua ari kwa Mashabiki, ni Mtu ambaye anafanya kazi nyingi za nje ya uwanja
Wale Mamelodi Sundowns wana Meneja wa Mashabiki anaitwa Alex Shokoena, yeye ndie anafatilia vikundi vya ushangiliaji, magroup ya WhatsApp na kila kitu kwa niaba ya bodi, ndio maana huwa tunasema wenzetu hatuwajui Maafisa Habari wao
Pale Yanga walikuwa na Antonio Nugaz, yule ndio kama Meneja wa Mashabiki, yeye alipaswa fanya yanayohusu Mashabiki na Afisa Mawasiliano anafanya yanayohusu klabu na Bodi
Simba kwasasa hawahitaji Afisa Mawasiliano au Habari kama Haji bali wanahitaji kuongeza nguvu kwenye kitengo cha Mashabiki na Wanachama, ndicho kitengo unachoweza kuwapa wakina Brother Mwijaku na wengine
Kwenye football panahitaji kelele, karaha na fujo ndio mtazamo wa familia ya mpira, ila wapewe watu Maalum kwenye kitengo maalum
Ulaya sio kwamba wapiga kelele hawana, bali ni watu tofauti na Afisa Habari

