Makapuku Forum

Makapuku Forum

farhan jr

SIMBA SPORTS CLUB VS BUSINESS & NETWORKING

Leo namalizia sehemu ya mwisho! Juzi na jana tulikuwepo eneo la biashara, tumesema mengi nadhani tulielewana japo kwa uchache! Tuje kwenye NETWORKING

Networking ni kama connection, hiki kitu kilikuwa kinakosekana kwenye klabu ila ujio wa CEO mpya ndipo alipoanza napo, anaweza asiufahamu sana mpira ila anafahamu Biashara ya mpira

Alifahamu klabu ipo Localized (ndani ya nchi) yeye akalazimika kusafiri ili kuikuza brand ya Simba, hapa tunaconnect na kitu kinaitwa BRAND AWARENESS, ni kama ufufuo wa brand iliyolala

Niwakumbushe kitu nchini kwetu Simba kama Brand inafanywa INFLUENCING tu kwakuwa ina hadhi yake, ila nje ni AWARENESS kwakuwa haijulikani sana, CEO yupo kwenye mission ngumu mno

Kwanini CEO anapambana na Networking? Kwakuwa anajua hata Uwekezaji hauna maana kama mtakwama eneo hili, hata mafanikio ni ngumu kupatikana

Mtu anaweza kuuliza kivipi? Awali nikwambie kitu kuhusu aina za Networking kwa klabu zote duniani! Kuna Club vs Big Clubs, Clubs vs Agency (Mawakala), Clubs vs Federation (Mashirikisho) na Club vs Media

Tuanze na klabu dhidi ya Klabu kubwa! CEO wa Simba alienda Mamelodi Sundowns (Mabingwa wa Afrika na Afrika Kusini), alienda Cairo kwa Al Ahly (Mabingwa wa kihistoria Afrika na Mabingwa wa Misri) kisha connection yake na FAR RABAT

Kwanini alienda huko? Ni hii hoja ya Networking, kutafuta uwanja rafiki (common ground) kati ya Simba na Miamba, hapa kuna target zaidi ya tatu alilenga, mosi Brand awareness, elimu na connection (Masoko na Mauzo)

Simba imefaidika na nini hapo? Nikukumbushe japo kidogo tu, ulisikia lawama zozote Simba alivyoenda kucheza Cairo na Ahly? Ulisikia lawama Ahly alivyokuja nchini? Hii ni network inayozaa maslahi ya pamoja

CEO kwenye eneo hilo hilo!

ITAENDELEA......
Screenshot_20210826-192905_GBInsta.jpg
 
farhan jr

SIMBA VS BUSINESS & NETWORKING (FINAL)

Wacha tumalize hiki kipengele ambacho tulisema nusu yake kuhusu NETWORKING! Nilianzia kwenye CLUB (FEEDER) vs BIG CLUBS! Nikasema mifano ya safari za CEO kule Mamelodi, Zamalek na Al Ahly

Nikawapa mfano namna mechi ya Ahly na Simba ilivyopigwa kwenye fair tofauti na miaka yote bila mizengwe! Ni matunda ya mahusiano, kati ya klabu zenye common interests, mnafahamu Miquisson alihitajika kwanza na Zamalek? Ila akauzwa Ahly

Kwenye hoja hii hata ile agenda ya African Super League, Simba amepewa mazingatio mbele ya miamba mingine ya Afrika, ni Networking! Hata FAR RABAT kucheza nao game wakiwa full mkoko ni respect iliyotokana na Network

Sehemu ya pili ni CLUBS vs AGENCIES (Kampuni za Mawakala), haya ni mahusiano ambayo Simba wameyajenga Afrika nzima, twende kwa mifano hapa! Mnafahamu kuwa Simba alipewa zaidi ya majina 74 ya wachezaji bora Afrika?

Maagent wao waaminifu ambao sio Madalali waliwapa watu sahihi tu! Peter Banda amechukuliwa alikuwa Sherrif Tiraspol inayocheza UEFA CHAMPIONS LEAGUE, yote ni connection sahihi waliojenga kupitia CEO na safu yake

Sehemu ya tatu ni CLUBS VS FEDERATIONS (Mashirikisho) hapa kuna TFF, CAF na FIFA! Hawa wote unapaswa kuwa nao karibu ndio kioo chako! Uliona picha ya CEO na Rais wa CAF, CEO na Rais wa FIFA na CEO na Moise Katumbi (ana cheo kwenye umoja wa klabu duniani)

Ndio network hii Simba anajaribu kujenga nao ndio maana ni rahisi kusema CAF wanaipost sana Simba na Ahly kwenye page zao ni Network tu, TFF wako njema na Simba ni Network tu kati yako na watu wako wa kazi

Hitimisho kwenye hili la Network na mahusiano mazuri kati ya klabu na Mashirikisho basi fuatilieni kisa cha Zamalek na droo anazopitia, mtajifunza kitu ni lazima utii Mamlaka inayowaendesha, that's protocol

Nadhani mumpongeze Mama na Dada yenu, pamoja na Viongozi wenu! NETWORK NETWORK ndio silaha kubwa... MWISHO
Screenshot_20210826-193315_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom