Makapuku Forum

Makapuku Forum

Naipenda simba mimi mwenzenu
Screenshot_20210725-194626_GBInsta.jpg
 
Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amemhakikishia Makamu wa Rais Dkt. Philip Mpango kuwa Wakulima wote wa zao la Korosho waliopewa ruzuku ya pembejeo kwa ajili ya kilimo cha msimu ujao hawatodaiwa wala kukatwa makato ili kugharamia pembejeo hizo kwani Serikali imezitoa bure kwa Wakulima lakini amewataka Wakulima kuendelea kuhudumia zao la korosho.

Akizungumza katika mkutano Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara Naibu Waziri Bashe pia ameeleza kuwa ifikapo hadi mapema mwakani (2022) pembejeo zote kwa ajili ya msimu ujao wa kilimo zitakuwa zimeshafika katika maghala ya maeneo husika tayari kuwafikia Wakulima kwa wakati ili kuwaepusha na usumbufu.

Awali Makamu wa Rais, Dkt Philip Mpango ameitaka Wizara ya Kilimo kusimamia ubora wa Korosho na ameahidi kusaidia kuunganisha uongozi wa mikoa inayozalisha korosho pamoja na Balozi za Tanzania nje ya Nchi kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ili kuwezesha korosho ya Tanzania kuuzwa kwa wingi nje ya Nchi.
Screenshot_20210726-131340_GBInsta.jpg
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla amewataka Wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya Ugonjwa wa Covid -19 ambapo amepiga marufuku Wananchi kuingia kwenye vyombo vya usafiri na sehemu za kutoa huduma pasipo kuvaa barakoa.

RC Makalla ametoa maelekezo hayo kufuatia Mwongozo uliotolewa na Wizara ya Afya ambapo amesema watafanya ziara za kustukiza kwenye Vituo vya Daladala, Feri, Stendi, Mabasi ya Mwendokasi, maeneo ya Masoko na sehemu zote za kutoa huduma ili kuangalia Utekelezaji wa agizo hilo.

Makalla amesema Serikali imejipanga kutoa huduma bora za matibabu kwa wagonjwa wote watakaofika Hospitali na kuwataka Wananchi watakaoona dalili za Corona kuwahi vituo vya Afya.
Screenshot_20210726-131510_GBInsta.jpg
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Safia Jongo amesema fisi amevamia makazi ya Watu na kumnyakua Mtoto wa mwaka mmoja na nusu kisha kukimbia nae na kumjeruhia hadi kumsababishia kifo chake.

RPC Safia amesema Wananchi watatu wamejeruhiwa pia wakati wakijaribu kupambana na fisi huyo na Mwananchi mmoja hali yake ni mbaya amelazwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Kitete.

“Askari walipofika eneo la tukio fisi alijaribu kuwashambulia pia wakafanikiwa kumuua, naomba niwatanie Watani zangu Wanyamwezi, risasi 49 zimepotea kumuua fisi, sasa huyu ni fisi wa kawaida au fisi wa Kinyamwezi!?” ———RPC Jongo
Screenshot_20210726-131614_GBInsta.jpg
 
Rais wa Tunisia Kais Saied amemfuta kazi Waziri Mkuu wa Nchi hiyo Hichem Mechichi na amesitisha pia shughuli zote za Bunge, kufuatia maandamano ya Wananchi jana Jumapili wakikilaumu Chama tawala kuwa kimeshindwa kutimiza matakwa ya Wananchi na kuongoza ipasavyo na pia kwamba hakijachukua hatua thabiti za kupambana na Corona.

Chama Tawala nchini humo kimemlaumu Rais na kusema alichokifanya ni sawasawa na kufanya Mapinduzi ya Serikali na kudai amekiuka katiba.
Screenshot_20210726-131726_GBInsta.jpg
 
Wizara ya Afya Tanzania imesema sasa hivi kila Mtu anayeingia kwenye chombo cha usafiri wa umma lazima awe amevaa barakoa (mask) kama ilivyoelekezwa kwenye mwongozo isipokuwa Watoto wenye umri wa chini ya miaka 8 tu.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Profesa Makubi amesema pia ———> "Wasafiri wawezeshwe kunawa mikono kwa sabuni na maji tiririka kabla ya kuingia kwenye vyombo vya usafiri hivyo, viongozi wa mtaa husika wahakikishe kuna vyombo vya kuhifadhia maji na sabuni vya kutosha katika kila kituo"

"Abiria wote waendelee kuelimishwa kuhusu umuhimu wa kutosongamana ndani ya vituo vya Mabasi kupitia walinzi getini, wahudumu wa mabasi na askari wa usalama wa barabarani, aidha boda boda wabebe kwa idadi sahihi (1-2) (siyo mishikaki) na wavae barakoa" ——— Prof. Makubi.
Screenshot_20210726-132540_GBInsta.jpg
 
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imemfutia Kesi na kumwachia huru Dereva Taxi, Mousa Twaleb aliyekuwa akishitakiwa kwa kumteka Mfanyabiashara maarufu nchini Mohammed Dewji maarufu kama 'MO'

Twaleb alifikishwa Mahakamani hapo May 28, 2019 na kusomewa mashitaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi na Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi akisaidiana na Wakili wa Serikali, Wankyo Simon, ambapo ilidaiwa katika shitaka la kwanza Mshitakiwa alijihusisha na genge la uhalifu.

MO alitekwa Oktoba 11, mwaka 2018 alfajiri maeneo ya Hoteli ya Colloseum wakati akienda kufanya mazoezi na alipatikana Oktoba 20, mwaka huo majira ya usiku alipotelekezwa na gari katika eneo la Gymkhana.
Screenshot_20210726-152819_GBInsta.jpg
 
Mchezaji wa Yanga SC, Mukoko Tonombe amewaomba radhi Mashabiki na Viongozi wa Club hiyo kutokana na kosa alilolifanya kwenye mechi ya jana vs Simba na kupelekea kutolewa nje kwa kadi nyekundu.

“Nawaomba radhi Mashabiki, Viongozi na Mashabiki, na Benchi la Ufundi kwa kilichotokea katika mchezo wa Fainali wa Yanga vs Simba kwamba sijakusudia kupewa kadi nyekundu ambayo labda ndio ilikuwa sababu ya kupoteza mchezo huo, naipenda sana Team yangu, Yanga Daima milele nyuma mwiko” ——— Mukoko.
Screenshot_20210726-183815_GBInsta.jpg
 
Simba SC imetua salama Dar es salaam ikitokea Kigoma ilikocheza na Yanga jana na kuifunga 1-0, baada ya kutua tu haya ndio maneno ya kwanza ya Mchezaji Mohamed Hussein15 a.k.a Zimbwe mbele ya Waandishi wa Habari.

'Tunajipanga kwa ajili ya kuchukua tena kombe na kuchukua tena sisi ni kawaida yetu na tutakapokutana nao popote tutajiandaa kikamilifu na kikubwa ni mazoezi tu”

“Derby ni Derby popote tutakapokutana nao Yanga iwe ni ngao ya hisani au kwingine sisi tutapambana, mazoezi, kujitunza na kumuomba Mungu ndio siri ya mafanikio yangu”———Mohamed.
Screenshot_20210726-183935_GBInsta.jpg
 
“Binafsi niliwahi kuwa na msimamo wa kukataa chanjo na niliuweka wazi. Nilipopata taarifa mpya na sahihi nilikimbia kuweka wazi mabadiliko ya msimamo wangu, haswa nikihofia watu kukataa chanjo kwa kuwa tu mtu mmojawapo mwenye ushawishi kwenye jamii kakataa chanjo” ——— Mbunge wa Nzega Vijijini, Hamisi Kigwangalla

“Tumerithi nchi yenye kuruhusu mijadala, ndiyo maana Askofu Gwajima anatumia haki yake ya kusema lakini ukiwa na maadili kidogo tu na ukajua nafasi yako kwenye jamii, utajitenga na uongo na kusimama na ukweli, kwa sasa utajua ukiwa una ushawishi basi utashawishi watu vibaya”

“Askofu Gwajima afanye uungwana azitafute makala za kisayansi asome kwa kina juu ya chanjo; na kama ana mashaka na sayansi yake atafute wataalamu wampe shule ya chanjo. Hata mimi Mbunge mwenzake nimesoma soma kidogo, niko tayari kumfafanulia maeneo kadhaa na kumuondoa shaka”

“Kwenye dunia ya sayansi na usomi, Kama ilivyo kwenye maisha ya kawaida, watu hubadili misimamo kutokana na kupata taarifa mpya, na sahihi zaidi; na ndiyo maana kila siku tunafanya tafiti na kujifunza, na kuboresha. Ndiyo maana leo kuna iPhone 12! misimamo haiwagi kama jiwe”

“Kama ambavyo mimi nilibadili msimamo wangu juu ya Chanjo baada ya ujio wa taarifa mpya za kisayansi juu ya usalama na uwezo wa chanjo, ndivyo ninaamini hata kaka yangu Askofu Gwajima atabadili msimamo wake na kujiunga na serikali kuhamasisha tutumie chanjo kujikinga” ——— Hamisi Kigwangalla.
Screenshot_20210726-184249_GBInsta.jpg
 
“Kauli ya Askofu Gwajima kuhusu chanjo na dhamira ya Serikali kuleta chanjo nchini haikubaliki, ni hatari kupotosha Watu wanaotuamini kuhusu mambo ambayo hatuna utaalam nayo” asema Mbunge wa Bumbuli January Makamba.

“Mjadala kuhusu usalama wa chanjo ni sahihi lakini kiapo kwamba Serikali imeileta kuwadhuru Watu si sahihi” ——— January

January Makamba ameandika hayo kufuatia Askofu Josephat Gwajima ambae ni Mbunge wa Kawe kupinga kitendo cha Serikali kukubali kupokea chanjo ya Corona kwasababu ya kile alichokiita ni mpango wa Mataifa ya nje kuwaangamiza Watanzania na kusema ambao wanaipigia chapuo chanjo hiyo wameshakula hela za watengenezaji wa chanjo hiyo.

“Naomba watanzania wenzangu tusikubali kuchanjwa kwa sababu chanjo hii hatuna uhakika na usalama wa chanjo hiyo, Mimi nina akili timamu ukiona napinga hii chanjo ujue haiko salama"——— alisema Askofu Gwajima.
Screenshot_20210726-184704_GBInsta.jpg
Screenshot_20210726-184732_GBInsta.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom