Makapuku Forum

Makapuku Forum

Juzi kati nimejifurahisha tu mwenyewe napenda vitu vizuri nimetoa 1.5 ili mradi moyo wangu uridhike tu kwa kinachotaka

Kwako kinaweza kuwa kitu cha hovyo ila upande wangu moyo wangu umeridhika yaaani halafu sijali chochote pesa inatafutwa tutatafuta tena
 
20210704_065227.jpg
20210704_065207.jpg
 
Katibu Mkuu, Wizara ya Afya - Idara Kuu ya Afya Profesa Abel Makubi amewataka Viongozi na Wasimamizi wa Shule kuzingatia mwongozo wa kudhibiti ugonjwa wa covid-19 ili kujikinga bila kuathiri shughuli za kijamii na kiuchumi ambapo wakati Shule na baadhi ya Taasisi za Vyuo zikitarajiwa kufunguliwa hapo kesho, amesema mwongozo utakaotumika ni uleule uliotumika mwaka jana na umepitiwa upya ili kuendana na mahitaji ya sasa.

Profesa Makubi amesema Serikali inalazimika kuwakumbusha Viongozi wa Shule na Taasisi za Elimu kuimarisha mifumo ya malezi kwenye mabwen na pia kufanya ukaguzi na ufuatiliaji wa mara kwa mara kuhusu afya za Wanafunzi.

“Waandae pia miundombinu ya maji na upatikanaji wa barakoa kama ilivyokuwa mwaka jana na kuchukua hatua stahiki iwapo kutagundulika kuna maambukizi bila hofu wala taharuki vilevile elimu ya kujikinga na ugonjwa huo iendelee kutolewa kwenye maeneo mbalimbali hata nyumba za ibada, shuleni na vyuoni" ——— Profesa Makubi.
20210704_173011.jpg
20210704_173027.jpg
 
Serikali imeanza mchakato wa kutengeneza chanjo ya virusi vya Corona hapa Tanzania ili kupunguza gharama ya kuagiza nje ya nchi na kuzifanya ziwe karibu na Wananchi.

Katibu Mkuu, Wizara ya Afya- Idara Kuu ya Afya Profesa Abel Makubi amesema kiwanda hicho hakitatengeneza chanjo ya UVIKO tu bali na magonjwa mengine.

"Wataalamu tunao wengi na kiwanda hicho hakitatengeneza chanjo ya UVIKO 19 pekee, hata ikiisha tutaendelea kuzalisha chanjo nchini" ——— Prof. Makubi.

Aidha, Prof. Makubi amesema Serikali haina mpango wa kuwauzia Wananchi chanjo ya ugonjwa wa COVID 19 wala kuruhusu Mtu yeyote kuingiza chanjo hiyo kinyume na utaratibu utakaowekwa.
20210704_173132.jpg
 
Emilio Flores Márquez wa Puerto Rico ametajwa na kitabu cha Guinness World Records kuwa Mwanaume mwenye umri mkubwa zaidi duniani baada ya kutimiza miaka 113, yupo kwenye hali nzuri kiafya japo kwa kiasi kikubwa amepoteza uwezo wa kusikia na pia aliwekewa kifaa maalum cha kuusaidia moyo wake kufanya kazi alipofikisha miaka 101.

Mzee huyu anasema ufunguo wa kuishi maisha yenye furaha ni kuutanguliza upendo kwenye maisha yako lakini pia kuepuka kuendekeza hasira mara kwa mara.

Mwanaume aliyekua na umri mrefu zaidi duniani alikua Dumitru Comănescu wa Romania aliyefariki June 2020 akiwa na umri wa miaka 111 na siku 219, vilevile kwa sasa Binadamu mwenye umri mkubwa zaidi duniani kwa mujibu wa rekodi za Guinness ni Kane Takana wa Japan mwenye umri wa miaka 118.

Rekodi ya Binadamu aliyeishi umri mrefu zaidi ikishikiliwa na Mwanamke wa Ufaransa Jeanne Calment ambae alifariki akiwa na miaka 122.
20210704_180445.jpg
20210704_180504.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom