Makapuku Forum

Makapuku Forum

M/kiti wa CHADEMA Freeman Mbowe leo kwenye kongamano la BAVICHA Tabata amezungumza kuhusu hitaji la Katiba mpya ———> “Katiba yetu ina mapungufu, miaka mitano iliyopita imetupa funzo kubwa ukiwauliza wa CHADEMA na wa CCM wote wamejifunza, jambo muhimu ambalo ni Katiba mpya iliyo bora"

“Tunapendekeza kuwe na Bunge la Katiba na lisiwe Bunge hili linaloendelea sasa wala wasituambie Bunge hili la sasa ndio liunde Katiba, ichukuliwe rasimu ya Warioba na Katiba na kisha iundwe rasimu ya Katiba mpya, sio gharama na tukiamua tutapata Katiba mpya mwkaa huu”——— Freeman Mbowe.

“Mapendekezo ambayo tungemwambia Mama kwenye mkutano na yeye, kwanza tunapendekeza Katiba Mpya, Mama aunde Tume ya Katiba na isiwe Tume ya CCM wala CHADEMA peke yake iwe Tume shirikishi itakayotambua makundi muhimu”

“Madai ya Katiba tutadai asubuhi, mchana hadi usiku, kama wanataka tukae mezani turidhie kama wasiporidhia tutakutana Barabarani, hatutoridhia kushiriki Uchaguzi wowote bila kuwa na Katiba au Tume ya Uchaguzi”

“Katiba ni mali ya wananchi na sio mali ya Viongozi, miongoni mwa mambo ambayo Rasimu ya Katiba ya Warioba ilibainisha ni kupunguza majukumu ya Rais , Warioba alipendekeza tuwe na Tume Huru ya Uchaguzi, Tuwe na Mgombea Huru” ———Mbowe.
20210701_195410.jpg
20210701_195427.jpg
20210701_195443.jpg
 
Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam imepokea kesi ya kupinga uchaguzi wa Shirikisho wa Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na imemtaka Rais wake Wallace Karia, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi na Bodi ya Wadhamini ya Shirikisho hilo kufika Mahakamani hapo kujibu hoja za kwanini uchaguzi wa TFF usisimamishwe, wito huu ni wa kesho Ijumaa saa 3 asubuhi.
20210701_195707.jpg
 
Dakika chache zilizopita tumeripoti kuhusu Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya DSM kupokea kesi mpya ya kupinga uchaguzi mkuu wa TFF na kumtaka Rais wake Wallace Karia, M/kiti wa Kamati ya Uchaguzi na Bodi ya Wadhamini ya Shirikisho hilo kufika Mahakamani kujibu hoja kesho Ijumaa saa tatu asubuhi kwanini uchaguzi huo usisimamishwe.

Taarifa ni kwamba kesi hiyo imefunguliwa na Ally Saleh 'Alberto' ambaye alikuwa mmoja wa Wagombea kwenye kiti cha Urais wa TFF ambapo uchaguzi huo ulipangwa kufanyika tarehe 8 Agosti, 2021 Tanga lakini hivi karibuni kamati ya uchaguzi ilimpitisha Wallace Karia kuwa Mgombea pekee kwenye nafasi ya Urais baada ya wengine kushindwa kwenye vigezo.

Kesi hiyo ya madai namba 98 ya mwaka 2021, itakuwa chini ya Jaji Kakolaki ambapo Wadaiwa ni TFF, Bodi ya wadhamini na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, Wakili akiwa ni Kiomoni Kibamba.
20210701_195933.jpg
 
Mchekeshaji wa Marekani Bill Cosby aliyesota gerezani kwa zaidi ya miaka miwili ya kifungo alichopewa cha kati ya miaka mitatu hadi miaka kumi jela, ameachiwa huru na Mahakama kuu ya Pennsylvania.

Mwaka 2018, Cosby alihukumiwa hadi miaka 10 jela baada ya kukutwa na hatia ya makosa matatu ya unyanyasaji wa kingono kwa kumlewesha na kumnyanyasa kingono Mwanamke aitwae Andrea Constand mwaka 2004.

Mahakama kuu ya jimbo la Pennsylvania leo Jumatano imetengua hukumu yake na kumfutia mashitaka yake na hivyo kuachiwa huru.
20210701_200304.jpg
 
Imezoeleka kwa baadhi ya Watu Tanzania kutumia page zao za mitandao ya kijamii 'kuchamba' Watu waliowazingua au waliowaudhi, sasa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dr. Faustine Ndugulile amewakumbusha Watu kuacha kufanya hivyo kwani kisheria ni kosa 'kuchamba' Mtu mtandaoni.

Dr. Ndugulile akiwa kwenye uzinduzi wa mpango mkakati wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na tovuti ya Wizara hiyo alisema moja ya vitu Watanzania wanapaswa kufahamu ni kwamba Mtu akitumia mfano Instagram kumsema Mtu vibaya (kumchamba), ni kosa kisheria au kumkashifu Mtu mtandaoni pia ni kosa hata kama account iliyotumiwa kufanya kosa hilo inatumia jina feki Mtu ilimradi account hiyo imefanya uhalifu Mmiliki wake atatafutwa na kuchukuliwa hatua.
20210702_171929.jpg
 
Kesi ya unyang’anyi kwa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa DC wa Hai Lengai Ole Sabaya pamoja na wenzake wawili imeahirishwa mara baada ya Shahidi wa upande wa Jamhuri kupata dharura.

Wakili wa Serikali kwenye kesi hiyo Trasila Gervas ameiambia Mahakama mbele ya Hakimu Salome Mshasha kuwa Shahidi waliyempanga ameshindwa kufika Mahakamani hapo na kuahidi Mashahidi kuwepo kwenye tarehe nyingine itakayopangwa, kesi hiyo imeahirishwa hadi July 16, 2021.

Kwa upande wa kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha namba 27 /2021 inayomkabili Lengai Ole Sabaya na wenzake watano nayo pia imeahirishwa hadi July 16,2021 kutokana na upelelezi kutokamilika na Washtakiwa wamerejeshwa Mahabusu.
20210702_172228.jpg
 
Serikali ya Tanzania imesema ipo kwenye hatua za mwisho za kuanzisha Shule maalum za michezo ambazo zitakua za Msingi na Sekondari katika Mikoa yote nchini na lengo ni kuwa na Shule na Vituo maalum vya kuendelezea vipaji vya michezo (sports academies).

Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa ameyasema haya akiwa kwenye sherehe za kufunga mashindano ya michezo na Taaluma kwa Shule za Sekondari (UMISSETA) yaliyofanyika Mtwara ambapo amesema Shule hizi zitazoanzishwa zitakuwa zinalea na kuendeleza vipaji vya michezo mbalimbali na Serikali itasimamia kwa ukaribu kuhakiksiha zinapatiwa mahitaji muhimu yatakayosaidia kuendeleza vipaji vilivyopo.

Amesema pia Serikali kupitia Chuo cha Maendeleo ya Michezo – Malya, inaanzisha Kituo maalum cha michezo cha kuendeleza vipaji (Centre of Sports Excellency) vitakavyokuwa vinapatikana kutokana na mashindano haya.

Katika mashindano ya mwaka huu ya UMISSETA Mkoa wa Dar es Salaam umeibuka mshindi wa kwanza wa jumla katika michezo yote, Bashungwa amememshukuru pia Rais Samia kwa maelekezo yake ya kuondoa kodi ya VAT, katika kununua na kuingiza nyasi bandia nchini, ili tuweze kujenga na kukarabati miundombinu yetu ya michezo.View attachment 1837952
20210702_172951.jpg
 





Mi ni zawadi nilopewa...
Macho nipepese wapi...
Mi kipofu kwako sioni...

Penzi limetaratadi, napepewa...
Harufu ya marashirashi...
Nikitouch touch shingoni...

Uvae baibui khanga...
Viatu vya kuchuchumia kangaroo...
Kisima tui tanga...

We huba nifukizia pambe tu...
Ukizungushia shanga...
Inashuka inapanda chini juu...

Nishatafuna karanga...
Sasa chumba ndo kiwanda watoto tu iyee iyee....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom