Makapuku Forum

Makapuku Forum

20210625_074012.jpg
20210625_074042.jpg
 
Mahakama Kuu ya Tanzania imetengua hukumu ya Mahakama ya Kisutu iliyowatia hatiani Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na wenzake nane. Yaagiza faini walizolipa zirudishwe.
20210625_122518.jpg
 
Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Mwigulu Nchemba (katikati) akimiminiwa kitakasa mikono na mbunge mwenzake kwa ajili ya kujikinga na virusi mbalimbali, walipohudhuria kikao cha 59 cha mkutano wa Bunge la Bajeti jijini Dodoma leo.
20210625_122758.jpg
 
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetengua hukumu ya kesi ya uchochezi dhidi ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe na wenzake na kuamuru warejeshewe kiasi cha TSh. Mil. 350 walicholipa kama faini.

Uamuzi huo umetolewa leo na Jaji Irvin Mgeta ambapo Mbowe na wenzake walihukumiwa Mahakama ya Kisutu March 10, 2020 kulipa faini ya shilingi milioni 350 za Tanzania ambazo ni sawa na dola elfu kumi na tatu.

Mbowe na wenzake walihukumiwa baada ya kutiwa hatiani kwenye makosa 12 ikiwemo la kufanya maandamano, Washtakiwa wengine kwenye kesi hiyo walikuwa ni Esther Matiko, Mchungaji Peter Msigwa, Salum Mwalimu, John Mnyika, Halima Mdee, John Heche, Ester Bulaya na Dk Vicent Mashinji.

Hukumu hiyo iliyochukua takribani saa 4, kuanzia saa 7 mchana hadi saa 11 jioni, ilitolewa na Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba baada ya kusikiliza ushahidi wa Mashahidi 23 baina ya utetezi na Serikali.
20210625_134944.jpg
20210625_134959.jpg
 
Kwenye hii post kuna Wabunge watano wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliochaguliwa kuwa Wabunge wa Bunge la Afrika (PAP) wakiliwakilisha Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wabunge hao ni Nape Nnauye, Jerry Slaa, Ng’wasi Kamani, Toufiq Salim Turky na Anatropia Theonest.
20210625_135222.jpg
20210625_135241.jpg
20210625_135256.jpg
20210625_135313.jpg
20210625_135333.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom