Makapuku Forum

Makapuku Forum

na mganga wetu anko Obe alimtapelii ....
EWnla3rVAAEil71.jpeg

Ha ahahaha hahaha, anko banana, mganga yeye ndo alitutapeli. Anakutafuta sana
 
Mkuu wa Wilaya ya Rorya Juma Chikoka maarufu Chopa Mchopanga leo amepokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Tarime Luteni Kanali Michael Mangwela,

DC Mchopanga amesema Mwenge huo unatarajia kukagua na kuzindua miradi tisa yenye thamani ya zaidi ya Tsh. Bilioni 2.
20210624_183751.jpg
 
"Wana Kisarawe mkikubali tukawa Timu moja tunashinda, Jokate amefanya mengi na kuacha alama, ametengeneza mtaji tunaanzia pale, ameleta Shule, Utalii, Uwanja wa Basketball, nimuahidi miradi kama aliiacha hatua 10 mimi nitaifikisha hatua 50”

"RC alituambia tuwe na vipaumbele yani vision ya kila Wilaya ukiacha vision kuu ambayo ni Ilani, Mimi nina mambo makubwa matatu, ambayo yote yanategemeana, katikati ujuzi, hatuwezi kuendeleza utalii kama Vijana wetu hawana ujuzi” ———
20210624_191020.jpg
 
Rais wa Uganda Yoweri Museveni ametangaza kuwa kesho Ijumaa June 25,2021 ni siku ya mapumziko ya kitaifa Nchini humo na pia yatafanyika maombi ya kitaifa kwa mara ya nne toka corona iingie Nchini humo.

Maombi ya kesho ni ili kumuomba Mungu aisaidie Nchi hiyo kuondokana na majanga mbalimbali ikiwemo corona wakati huu ambapo Nchi hiyo inapambana na wimbi la tatu la corona.

Maombi yatafanyika Ikulu ya Entebbe lakini Viongozi wengine wa Dini wameombwa kufanya maombi hayo na Waumini wao kupitia mtandao wa zoom.
20210624_191445.jpg
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo amemtaka Mbunge wa Mbogwe, Nicodamus Maganga ahudumie Wananchi akizingatia utaratibu wa Nchi na iwapo anataka kulipwa kwa dola kama alivyoongea Bungeni juzi basi ahamie katika Nchi zinazofanya hivyo.

Kwenye mahojiano na millardayo Chongolo amesema ———> “Wananchi wamemtuma Mbunge kuwasemea changamoto zao zikiwemo za maji, elimu, umeme, barabara, hospitali, mazingira ya kufanyia biashara na huduma nyingine za jamii kama Ilani ya uchaguzi ya CCM 2020/2025 inavyoainisha na sio kujizungumzia yeye binafsi, huo ni ubinafsi na CCM kamwe haitovumilia”

Mbunge Maganga alisimama Bungeni juzi na kuwataka Wabunge kuwaeleza Wananchi ukweli kuwa mishahara na posho wanazolipwa hazitoshi na hata jana akiongea na millardayo alisisitiza ———> “Mitandaoni tumekuwa tukitukanwa sana kuwa tunalipwa na hela yetu haikatwi kodi, wamesahau kuwa mpaka huyu kuitwa Mbunge amepitia njia gani”

“Vilevile huyu Mbunge anafuatwa na Watu wangapi kwa mfano Mimi naishi jimboni kila asubuhi lazima utakuta Wananchi huyu Mtoto ameishiwa damu, wengine ukawasalimie Hospitali utaona aibu tu kuwachangia, sasa ukiangalia mshahara wa Mbunge ni Milioni 3.8” ——— Maganga. View attachment 1828735
20210624_191655.jpg
 
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Daniel Chongolo amemtaka Mbunge wa Mbogwe, Nicodamus Maganga ahudumie Wananchi akizingatia utaratibu wa Nchi na iwapo anataka kulipwa kwa dola kama alivyoongea Bungeni juzi basi ahamie katika Nchi zinazofanya hivyo.

Kwenye mahojiano na millardayo Chongolo amesema ———> “Wananchi wamemtuma Mbunge kuwasemea changamoto zao zikiwemo za maji, elimu, umeme, barabara, hospitali, mazingira ya kufanyia biashara na huduma nyingine za jamii kama Ilani ya uchaguzi ya CCM 2020/2025 inavyoainisha na sio kujizungumzia yeye binafsi, huo ni ubinafsi na CCM kamwe haitovumilia”

Mbunge Maganga alisimama Bungeni juzi na kuwataka Wabunge kuwaeleza Wananchi ukweli kuwa mishahara na posho wanazolipwa hazitoshi na hata jana akiongea na millardayo alisisitiza ———> “Mitandaoni tumekuwa tukitukanwa sana kuwa tunalipwa na hela yetu haikatwi kodi, wamesahau kuwa mpaka huyu kuitwa Mbunge amepitia njia gani”

“Vilevile huyu Mbunge anafuatwa na Watu wangapi kwa mfano Mimi naishi jimboni kila asubuhi lazima utakuta Wananchi huyu Mtoto ameishiwa damu, wengine ukawasalimie Hospitali utaona aibu tu kuwachangia, sasa ukiangalia mshahara wa Mbunge ni Milioni 3.8” ——— Maganga. View attachment 1828735View attachment 1828736
Nasubiri magazeti ukileta niite
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom