Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amefanya ziara ya kushtukiza kwenye soko maarufu la Kariakoo Dar es salaam ambapo baada ya kujionea hali halisi amezungumza yafuatayo.

“Sijui kama Viongozi wa soko hili la Kariakoo wako hapa!?, kutokana na ziara yangu nimeona kwanza Serikali itusaidie kusimamia kufanya tathmini ya uendeshaji wa soko lote kwasababu hali niliyoiona ndani na nje kwenye vibanda hairidhishi”

“Serikali yetu kuanzia wakati Mpendwa wetu Hayati Magufuli yupo hadi leo lengo letu ni kusaidia Wafanyabiashara wadogo, tuliyoyaona ndani nimengoea na baadhi yenu naona kama usaidizi wa Wafanyabiashara wadogo haupo ila kuna kutengeneza faida kwa Uongozi wa Soko”

“Hata mipango ya uingizaji wa bidhaa nayo haimpi nafuu Mfanyabiashara mdogo, maamuzi yangu ni kwamba tutafanya tena tathmini ya uendeshaji wa soko na tuone kama hili soko lisimamiwe na Uongozi uliopo au Jiji lichukue hili soko”

“Jambo jingine nimeangalia bidhaa zilizomo ndani ni vurugu mechi, huoni bidhaa gani ipo wapi, unamkuta muuza vyerehani yupo katikati ya anayeuza dawa za kilimo, dawa za panya n.k, ukiangalia soko halipo vizuri” ——— Rais Samia Suluhu
20210601_130010.jpg
 
“Soko hili halipo vizuri, niwaahidi Serikali tunakwenda kufanya tathmini ya soko lakini wakati tathmini inaendelea, niagize na naambiwa Waziri wa TAMISEMI alitoa pia hayo maagizo, kuusimamisha kidogo Uongozi wa Soko uliopo (tutaangalia mpaka ngazi gani)”

“Naagiza kuusimamisha kidogo Uongozi wa Soko la Kariakoo uliopo (tutaangalia mpaka ngazi gani), Vyombo vya Serikali vifanye uchunguzi kwanza halafu tutakuja kutoa maamuzi lakini kwa ujumla hali iliyopo hapa haijaniridhisha na tunakwenda kuchukua hatua zinazofaa”

“Naomba muendelee na biashara zenu kwa salama bila vurugu Serikali ipo pamoja nanyi, lakini wanasema abebwae ujikaza, wakati Serikali inawabeba nanyi jitahidini kufuata kanuni zinazowekwa, nimeona vibanda kila mahali tutakaa tuone njia nzuri ya kuwapanga” ——— Rais
20210601_130138.jpg
 
Rais Samia Suluhu Hassan leo amefanya ziara za kushtukiza sehemu mbalimbali Dar es salaam akianzia na sokoni Kariakoo ambako ameusimamisha kazi Uongozi wa soko hilo kisha akaenda Mbagala na sasa ameingia kwenye Hospitali ya Mwananyamala kama anavyoonekana kwenye video hii.
20210601_140546.jpg
20210601_140519.jpg
 
Rais Samia ameendelea na ziara yake Dar es salaam leo ambapo amefika pia Mbagala Zakhem na kufanya ukaguzi wa mradi wa ujenzi miundombinu ya mabasi yaendayo haraka awamu ya pili ambapo amemuagiza Mkandarasi kuongeza kasi ya ujenzi wa mradi huo ambao amesisitiza kasi yake hairidhishi.

“Nilikuwa napitia mafaili ya miradi ofisini nikauona mradi huu wa mwendokasi Mbagala, mradi huu kwa sasa ulikuwa ufikie asilimia karibu 60 na kitu lakini kwa taarifa nilizopata leo mradi upo kwenye asilimia 16 tu, nikasema tuje tuone kinachokwamisha mradi huu”———Rais Samia

“Tumeongea na Wasimamizi wa mradi huu wa mwendokasi Mbagala na pia Wakandarasi na tumeona kinachokwamisha mradi, Serikali bado hatujaridhishwa na kasi yake ingawa mwishomwisho hapa wameongeza speed kidogo, tumekubaliana waongeze kasi zaidi ili mradi umalizike”———Rais Samia

“Tunataka mradi huu wa mwendokasi Mbagala umalizike ili kurahisisha safari zenu Wananchi na tuinue uchumi, Serikali juzijuzi hapa tumembadilisha Kiongozi mkubwa wa mradi huu tumemuweka mwingine ili atusaidie kuongeza kasi ya mradi huu”———Rais Samia, Mbagala
20210601_155556.jpg
 
Rais Samia Suluhu leo ametembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala Dar es salaam kwa kushtukiza na kutoa zawadi ya mashuka 200 kwa ajili ya matumizi ya Wagonjwa huku akiwaahidi Wafanyakazi wa Hospitali hiyo kuwa zawadi nyingine ni yeye kwenda kuangalia maslahi yao.

Jingine ambalo amesema Rais Samia ni kuhusu uvaaji wa barakoa ———> “Watu hapa tumeziba midomo (kwa barakoa) ila wengine tuko wazi (bila kuvaa barakoa) naomba mchukue tahadhari sasa hivi tuko vizuri ila mnasikia huko India mambo yanavyopukutisha Watu yani wamechoma mpaka kuni hamna”

“Mambo haya yanaambukizana tumezuia usafiri wa kuja na kwenda kule ili kuzuia virusi (Corona) visije ila hatuwezi kujua, kila Mtu ajikinge anayekuja nacho humjui”———
20210601_155745.jpg
 
Hizi ni picha za Rais Samia Suluhu leo baada ya kutembelea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Mwananyamala Dar es salaam kwa kushtukiza na kutoa zawadi ya mashuka 200 kwa ajili ya matumizi ya Wagonjwa huku akiwaahidi Wafanyakazi wa Hospitali hiyo kuwa zawadi nyingine ni yeye kwenda kuangalia maslahi yao.
20210601_155905.jpg
20210601_155925.jpg
20210601_155958.jpg
20210601_160017.jpg
 
Mbunge wa Momba Condester Michael Sichalwe ametolewa ndani ya ukumbi wa Bunge ili akabadilishe mavazi yake baada ya Mbunge wa Nyangw'ale Hussein Nassor Amar kuomba muongozo wa Spika kuwa kuna baadhi ya Wabunge wamevaa mavazi yasiyo na maadili.

Spika Ndugai alimtaka Mbunge Hussein Nassor Amar kumtaja mmoja ambaye amemuona ndipo alipomtaja Mbunge wa Momba Condester Michael Sichalwe ambapo Spika alimtaka atoke ndani ya ukumbi wa Bunge ili akabadilishe mavazi yake.

Huyu mbunge alieomba muongozo kwa spika sio bwana smart kweli View attachment 1804592View attachment 1804593View attachment 1804594
huyu wamemuoneaa kiukweli
 
Staa wa Inter Milan na Timu ya Taifa ya Chile Arturo Vidal amekutwa na maambukizi ya virusi vya Corona na sasa yupo hospitali akipatiwa matibabu.

Vidal anapatiwa matibabu lakini anasumbuliwa pia na tonsesi hivyo ni wazi sasa atakosekana katika mchezo wa Chile vs Argentina kuwania kufuzu World Cup Alhamisi hii na vs Bolivia wiki ijayo.

Wachezaji wengine katika kikosi cha Chile wamepimwa na kukutwa negative, Vidal Ijumaa iliyopita alichoma chanjo ya Corona.
20210601_165545.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom