Makapuku Forum

Makapuku Forum

Baraza la Wanawake CHADEMA (BAWACHA) likiongozwa na Katibu Mkuu wa Baraza hilo Catherine Ruge limezindua program maalumu ya haki ambapo pamoja na mambo mengine wametembelea kituo cha kulelea Watoto wanaoishi mazingira magumu cha Samaritan Village na kutoa vitu mbalimbali.

"Tumesema mwaka 2020 ni mwaka wa haki ili Viongozi wapatikane kwa haki na tukasema ili tupate nguvu lazima tuanze na Mungu ndio maana tumekuja kutoa sadaka kwa Watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na tumetoa vitu mbalimbali sukari, mafuta, chakula na sio kwamba tuna vitu sana tumekuja kuonyesha kuna Watu wana uhitaji"-Catherine Ruge, Katibu BAWACHA Taifa.
20210526_164427.jpg
20210526_164407.jpg
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Wankyo Nyigesa amesema Najima Said (14) ambaye ni Mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Mtongani na Mkazi wa Mtongani Mkoani humo amekutwa amejinyonga ndani ya choo nyumbani kwao May 22 2021.

“Upelelezi umebaini kuwa chanzo cha kifo cha Mtoto huyo ni kutuhumiwa na Mama yake kuwa aliiba shilingi elfu tano ikiwa ni pesa ya Mama yake, tunawashikilia Mama wa Marehemu aitwaye Ashura Selemani na Baba Mlezi kwa mahojiano” ———RPC Pwani
20210526_164606.jpg
 
Mkazi wa Umwerani, Kata ya Kongowe, Kibaha Mkoani Pwani Mrisho Omary amefariki baada ya nyumba ya udongo iliyoezekwa kwa nyasi kuchomwa moto na Watu wasiojulikana akiwa amelala na wenzake ndani.

Watu wengine waliokuwa kwenye nyumba hiyo siku ya tukio May 15,20201 ni Mwalimu Ally Shaban na Lusekelo ambapo wote waliwaishwa Hospitali ya Rufaa ya Tumbi na Mrisho akafariki May 17.

“Mwanamke mmoja anaitwa Zuwena alipiga kelele akisema amebakwa na kuibiwa simu na Elfu 30 na Watu hao watatu, Watu hao wakakimbilia kwenye nyumba hiyo ndipo Wananchi wenye hasira kali wakaichoma nyumba moto”———RPC Pwani, Wakyo Nyigesa

“Uchunguzi wa awali unaonesha kulikuwa na ugomvi wa kimapenzi kati ya Zuwena na Watu hao aliowaitishia wizi na upelelezi unaendelea kuwabaini wote waliohusika na tukio hilo”———-RPC Pwani
20210526_164807.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom