Mahakama Kuu Kanda ya Tabora imemuhukumu kutumikia kifungo cha kwenda Jela miaka minne Lameck Essau Meza (38), Mkazi wa Sikonge baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kumuua bila kukusudia Mke wake, Dafroza Paul.
Lameck Meza alimpiga Mkewe na kumsababishia kifo chake, hii ni kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa Mahakamani.
Upande wa Jamhuri umeieleza Mahakama kwamba hii ni Mara ya pili kwa Lameck kuua bila kukusudia kwani alishawahi kusababisha kifo cha Mke wake wa kwanza kwa kumpiga na alihukumiwa kifungo cha miaka minne pia.
View attachment 1782280