Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amerejea nchini akitokea Uganda ambako mapema leo amehudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Uganda Yoweri Museveni.

Rais Museveni ameapishwa leo kuiongoza Uganda kwa muhula wa sita mfululizo, hii ni baada ya kushinda uchaguzi wa Jan 14, 2021 kwa kuwashinda wagombea wengine 10 katika nafasi ya Urais (akiwemo Robet Kyaluganyi maarufu Bobi Wine) kwa ushindi wa 58%
20210513_044854.jpg
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amezitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania, Mamlaka ya Bandari Tanzania na Mamlaka ya Serikali Mtandao kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuboresha utendaji wa Bandari ya Dar es Salaam, ameyasema hayo alipotembelea bandari hiyo kujionea utendaji.

“TPA endeleeni kuiimarisha bandari yetu, hii ni sura ya uchumi wa nchi yetu, zungumzeni lugha moja ya uwajibikaji, TRA muwepo maeneo yote yanayohitaji uwepo wenu na muda wote Wateja wetu wahudumiwe ili bandari yetu iendelee kuwa bora, Nchi nyingi zinatutegemea”

“Dosari zote za mfumo wa TANCIS zifanyiwe kazi, mfumo usituharibie, mnapoona kuna madhaifu fanyeni marekebisho ya haraka, tunataka Wateja waingie na kutoka kwa muda mfupi”

Vilevile Waziri Mkuu amemuagiza Kamishna Mkuu wa TRA apeleke Watumishi katika mizani ya TANROADS iliyopo Kurasini Dar es Salam ili kurahisisha ukaguzi wa ‘seal’ pale ambapo magari yamezidisha uzito na yanahitaji kukaguliwa.
20210513_125811.jpg
20210513_125835.jpg
20210513_125921.jpg
20210513_125936.jpg
 
UNAAMBIWA Mohamed Ayoub wa Myanmar aliwabeba Wazazi wake kwenye vikapu kama hivi na kutembea nao kwa miguu siku 15 akikimbia unyanyasaji na vita huko Rakhine ambako zaidi ya Watu 9000 waliuwawa huku zaidi ya 750000 wakikimbia makazi yao, hata hivyo Baba yake alifariki baadae.
20210513_130532.jpg
 
UNAAMBIWA Singapore kuna sheria inayokataza yeyote kutembea uchi bila nguo iwe hadharani, ndani ya nyumba yake au pengine, adhabu ni $ 2000 (Tsh. 4,638,000), Mtu akifanikiwa kukupiga picha hata kama ni ndani kwako unapigwa faini au jela miezi mitatu.
20210513_130628.jpg
 
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepata kibali cha ajira 547 kutoka Ofisi ya Rais Utumishi za wataalamu wa kada mbalimbali za afya wanaokidhi vigezo vya kuajiriwa chini ya wizara hiyo na taasisi zake.

Tangazo hilo la ajira limetolewa jana Jumatano Mei 12, 2021 na katibu mkuu wa Wizara ya Afya, Profesa Abel Makubi.

Amesema ajira hizo ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Serikali akibainisha kuwa ajira hizo zinajumuisha nafasi 473 zitakazoratibiwa na wizara wakati nafasi 74 zitaratibiwa na sekretariati ya ajira.

“Wataalamu 74 wa kada mbalimbali wataajiriwa katika maabara kuu ya Taifa na wataalamu 473 wa kada mbalimbali wataajiriwa katika hospitali za kanda za KCMC, Mbeya, Bugando na Benjamini Mkapa, hospitali za rufaa za mikoa na vyuo mbalimbali vilivyopo chini ya wizara ya afya,” amesema.

Profesa Makubi amesema wataalamu 473 chini ya uratibu wa wizara ambao watanufaika na nafasi hizo ni pamoja na madaktari wauguzi, wafamasia, wateknolojia wa dawa, wateknolojia wa maabara, wateknolojia wa mionzi, wateknolojia wa macho, watoa tiba kwa vitendo, maafisa afya mazingira, wasaidizi wa afya, makatibu afya, maafisa istawi wa jamii na maafisa lishe.

“Ajira hizo (473) zitajaza nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliokoma utumishi kutokana na sababu mbalimbali. Waombaji wanasisitizwa kuzingatia maelekezo yote yatakayotolewa na vyanzo rasmi vya taarifa za ajira na utaratibu kupitia tovuti www.moh.go.tz kwa kiunganishi (ajira.moh.go.tz). Maombi ni kuanzia Mei 12 hadi 25, 2021,” amesema.

20210513_131417.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom