Makapuku Forum

Makapuku Forum

‘Mtoto wa miujiza' Khadija

Mtoto huyu azaliwa mama yake akiwa amepoteza fahamu baada ya kuugua ugonjwa wa virusi vya corona wakati akiwa mjamzito.

-
Marriam Ahmad alipokuwa na ujauzito wa wiki 29 na hali yake ikabadilika kwa haraka sana. Hapo ndipo daktari wake alipoanza kusema kuwa afanyiwe upasuaji na mwanzo akawa ameonya kuwa kuna hatari Marriam akapoteza fahamu kipindi chote hicho.

-
Lakini pia aliambiwa kuwa mtoto wake anaweza akakosa nguvu ya kunusurika kifo.

Daktari wake alikuwa amesema "huenda asifanikiwe kurejea tena kuwa hai".
-

Lakini cha kushangaza ni kwamba licha ya onyo lilitolewa na daktari kufikia mchana siku iliyofuata, Marriam alikuwa ameamka yaani fahamu zake zimerudi.
"Sikujua nini hasa kimetokea" alisema. "Nilipoamka. Niliona sina chochote tumboni na nikawa mwenye maumivu mengi sana."
-

"Kwa mtazamo wangu, Khadija wangu alikuwa imara kweli. Hakuwa na matatizo yoyote licha ya kuzaliwa akiwa na wiki 29. Walikuwa wakiniambia kwamba atakuwa na kila aina ya matatizo. Lakini alikuwa mzima kabisa. Ilikuwa ni miujiza."
20210511_163751.jpg
20210511_163813.jpg
 
Sophie Scholl ni nani?

Scholl ni msichana kutoka Ujerumani aliyechinjwa kwa kuongoza harakati dhidi ya Adolf Hitler. Alipata umaarufu kwa kusimama kidete dhidi ya dikteta Adolf Hitler, ujasiri ambao hata hivyo uligharimu maisha yake.
-
Baba yao, ambaye alikuwa ni mkosoaji mkubwa wa utawala wa Hitler, alishtushwa sana na mapenzi ya watoto wake kwa dikteta huyo. Ushawishi wa familia na marafiki wa karibu taratibu ukaanza kuathiri maono ya Sophie na kaka yake.

-

Wawili hao walikuwa wanamitazamo ya siasa za kiliberali, hivyo sera za kinazi za Hitler almaarufu kama 'Third Reich' zilikuwa ni kinyume cha falsafa walizoziamini na hawakuweza kwenda nazo sawa, pia walipooona namna ambavyo Wayahudi na wasanii walivyokuwa wakibaguliwa, wakaanza kuutazama utawala wa Hitler kwa jicho la ukosoaji.Mara baada ya Hitler kuivamia Poland , ukosoaji ukawa upinzani.

-
Mwishoni mwa wiki, watu wengi waliadhimisha miaka 100 ya kuzaliwa kwa msichana huyo.

20210511_163957.jpg
20210511_164015.jpg
20210511_164033.jpg
 
Magavana wa kijeshi wa mikoa ya Kivu ya Kaskazini pamoja na Ituri, wameingia madarakani jana JUmatatu, baada ya kuteuliwa na rais Tshisekedi katika nia yake ya kurudisha amani katika mikoa hiyo inayokabiliwa na vita.
20210511_164506.jpg
20210511_164523.jpg
 
Rais wa Uganda, Yoweri Museveni anatarajiwa kuapishwa kesho Jumatano Mei 12, 2021 kuiongoza nchi hiyo kwa muhula wa sita wa miaka mingine mitano. Hatarajiwi kubadilisha mfumo wake wa uongozi wa kimabavu aliouanzisha zaidi ya miaka 35 iliyopita.
20210511_164653.jpg
 
Kundi la wanamgambo la Hamas limefyatua maroketi ambayo ni nadra kuelekea Jerusalem usiku wa kuamkia leo Jumanne, baada ya mamia ya Wapalestina kuumizwa kufuatia makabiliano na polisi wa Israel kwenye eneo la msikiti wa al- Aqsa. Wakati machafuko hayo yakiongezeka na kuzidisha wasiwasi, Marekani, Uingereza na Umoja wa Ulaya wametaka utulivu kurejeshwa Jerusalem.
20210511_164806.jpg
20210511_164824.jpg
20210511_164842.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom