Makapuku Forum

Makapuku Forum

Waziri wa Viwanda na Biashara Profesa Kitila Mkumbo akiambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dr. Hashil Abdallah wamekutana na Waagizaji na Wazalishaji mafuta ya kula Nchini Tanzania ili kujua kinachosababisha kupanda kwa bei ya mafuta hayo ambapo wameweka mikakati ya muda mfupi na mrefu ya kukabiliana na uhaba wake.

“Tunafahamu kutokana na upungufu wa malighafi, Viwanda vyetu vya ndani vya alizeti haviwezi kuzalisha kwa kiwango ambacho kinakidhi mahitaji ya ndani, Nchi nzima inahitaji tani 570,000 na sisi tuna uwezo wa kuzalisha tani 210,000 pekee, ili kufidia upungufu huu tunaagiza nje”

Profesa Mkumbo ametaja changamoto kubwa zinazosababisha kupanda kwa bei ya mafuta kuwa bei ya mafuta ya mawese katika soko la Dunia kupanda ambapo mwaka jana katika soko la Dunia yaliuzwa USD 600 kwa tani moja lakini kwa sasa wanauza USD 1200 kwa tani.

Sababu nyingine kwa sasa Waagizaji wanaagiza mafuta yaliyochakatwa kutoka nje sababu viwanda vitatu vikubwa vya Tanzania havifanyi kazi sababu ya mabadiliko ya kodi kipindi cha nyuma, waagizaji walikuwa wakiagiza mafuta yaliyochakatwa na wanaeeleza kuwa ni mafuta ghafi, serikali ili kudhibiti na kulinda viwanda vya ndani iliongeza kodi mpaka 35% ya uingizaji ya mafuta yaliyochakatwa.

Waziri Profesa Mkumbo ameeleza kuwa kuanzia mwezi huu wa tano hadi mwezi saba kuna mavuno makubwa ya alizeti ambayo yatasaidia kupatikana malighafi kwa viwanda vya alizeti hivyo uzalishaji wa mafuta utaongezeka na kusaidia bei ya mafuta kushuka.

Mwenyekiti wa wenye Viwanda vya mafuta ya kula Gulam Dewji ameeleza kuwa kupanda kwa bei ya mafuta Tanzania kunatokana na bei ya mafuta kwenye soko Dunia hivyo ameiomba Serikali kupunguza kodi ya uagizaji wa mafuta kwani kwa sasa kodi ya mafuta yaliyochakatwa ni 35% na kodi ya mafuta ghafi ni 25% ambayo hupitishwa kiwandani kuchakatwa hivyo kodi kubwa ya mafuta ghafi ndio imesababisha wafunge viwanda na waagize mafuta yaliyochakatwa.
20210510_201433.jpg
 
Waziri Bashungwa ameagiza kituo cha Kitaifa cha Data kinachosimamia N-card kuwarejeshea tiketi zao kwenye mfumo wa kadi za kuingilia uwanjani Mashabiki wote wa Simba na Yanga 43,947 ili siku ya kurudiwa mechi wakae uwanjani eneo lilelile walilolilipia awali.
20210511_144329.jpg
 
Makubaliano yamefikiwa kwenye kikao kilichoongozwa na Waziri Bashungwa kwamba mechi ya Simba na Yanga irudiwe "Wizara inaliacha swala hili katika taratibu za TFF na Bodi ya Ligi ili wakae haraka iwezekanavyo na kutoa tarehe ya kurudiwa kwa mechi hiyo"
20210511_144524.jpg
 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa kupitia kwa Watendaji wa Simba na Yanga amewaomba radhi Mashabiki wa soka kwa kusogezwa na baadaye kuahirishwa kwa mechi, pia amewaomba kuwa watulivu na kuiamini Serikali kuwa ilikuwa na nia njema na sababu za msingi iliposhauri mechi isogezwe.
20210511_144622.jpg
20210511_144638.jpg
20210511_144656.jpg
 
Watu 11 wameuwawa kwa kupigwa risasi kwenye mji wa Kazan, Urusi ambapo miongoni mwao ni Wanafunzi na Mwalimu mmoja, mmoja wa Washukiwa wa mauaji hayo ni Kijana ambae hajafikisha umri wa miaka 20, Mamlaka zinasema ni Mmiliki wa silaha aliyesajiliwa.

Watu 16 wakiwemo Watoto 12 na Watu wazima wanne ni miongoni mwa waliowaishwa Hospitali baada ya kujeruhiwa kwenye taharuki hii ambayo ilisababisha wengine kujiokoa kwa kutokea madirishani.
20210511_145006.jpg
20210511_145023.jpg
20210511_145040.jpg
20210511_144904.jpg
20210511_144944.jpg
 
Shabiki wa Yanga Mwanariadha Mang’suli Hussein (45) aliyekimbia kwa miguu kutoka Kigoma mpaka Dar kwa kutumia siku 22 kwa ajili ya kuja kuitazama mechi ya Simba na Yanga amesema GSM ambao ni Wadhamini wa Yanga wamemuahidi tiketi ya Ndege kurudi Kigoma.

Mang’suli ambae nyumbani ni Kigoma anajishughulisha na kazi ya kutengeneza bustani za Watu mbalimbali amesema kama mechi isingeahirishwa hii ndio ingekua mara yake ya kwanza toka amezaliwa kushuhudia mechi ya Simba na Yanga.

Mang’suli alishindwa kufika Dar kuiwahi mechi baada ya kuumwa na tumbo kuanzia akiwa Dodoma, pia anasema akiwa njiani alirushiwa nyuki na Watu asiowafahamu waliokua wamepakizana kwenye pikipiki ambapo hakutaka kulumbana nao bali akaendelea na safari.
20210511_151144.jpg
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dr.Hassan Abbas amekutana na Menejimenti ya Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) jana Dar es Salaam ambapo kwa pamoja wamejadiliana kuhusu namna ya utekelezaji wa majukumu ya BASATA likiwemo jukumu la msingi la kufufua na kukuza Sanaa nchini, kuandaa matamasha mbalimbali kwa Wasanii, Uboreshwaji wa kanuni za Baraza pamoja na utoaji wa Tuzo kwa Wasanii.
20210511_151321.jpg
20210511_151339.jpg
20210511_151403.jpg
 
Mamlaka ya Chakula na Dawa Marekani (FDA) imeidhinisha matumizi ya dharura ya chanjo dhidi ya Virusi vya Corona ya BioNTech-Pfizer kwa Watoto kuanzia miaka 12 na kuendelea.

Dr. William Gruber, Mtaalamu wa chanjo ya BioNTech/Pfizer na magonjwa ya Watoto kutoka Cincinatti Marekani amesema———“tuna furaha kubwa kusikia kwamba FDA imepanua matumizi ya dharura ya chanjo ya BNT162 B2 kwa Watoto wa miaka 12 hadi 15, huu ni wakati wa nafuu kubwa kwetu, kwa kuzingatia uwezo wetu wa kupambana na janga la COVID-19”

Chanjo ya BioNTech-Pfizer ni chanjo ya kwanza kuruhusiwa kutumika kwa Watoto wa chini ya miaka 16 nchini Marekani.

Taarifa ya FDA imesema takribani maambukizi ya Corona milioni 1.5 kwa watoto wa kati ya miaka 11 na 17 yameripotiwa kwenye taasisi ya kudhibiti magonjwa ya kuambukiza (CDC) nchini humo tangu Aprili mwaka jana hadi Aprili 30 mwaka huu.
20210511_151513.jpg
 
Katika kile kinachoonekana kuwa ni kuzidi kuimarika kwa ushirikiano na mahusiano mazuri kwa Nchi za Afrika Mashariki, Serikali ya Kenya imeruhusu mahindi ya Uganda kuingia nchini mwake.

Wizara ya Afya ya Kenya imesema mahindi hayo yamefanyiwa vipimo na hayana sumu, tayari Malori 20 kutoka Uganda ambayo yalizuiwa mpakani kwa siku kadhaa yameingia Kenya.

Itakumbukwa Rais Samia alipofanya ziara rasmi ya siku mbili nchini Kenya Wiki iliyopita, Rais Kenyatta alisema ———“Kuhusu hayo mahindi ambayo yamelala hapo mpakani (mwa Kenya na Tanzania), Waziri nakupa wiki mbili, yote iwe imefunguliwa (Malori yaruhusiwe kupita) na maneno yaishe, hakuna haja ya kuumiza Watu wetu”.
20210511_151645.jpg
 
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Hawa Mchafu amedai baadhi ya Wanaume wa Tanzania wanatumia nguvu kubwa kujadili habari za Simba na Yanga kuliko hata kujadili afya zao.

Hawa amesema kama nguvu hiyo ingetumika kujadili masuala ya afya ikiwemo kupima UKIMWI huenda vita dhidi ya UKIMWI ingekuwa nyepesi.

Mbunge huyo ametoa kauli hiyo leo May 11, 2021 bungeni Dodoma wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Afya mwaka 2021/22.

Kuhusu ukeketaji, amesema Wanaume wanatakiwa kutangaza hadharani kwamba hawawezi kuwaoa wanawake waliokeketwa lakini kukaa kwao kimya bado ukatili huo utaendelea “wanaume wakisema ladha ya waliokeketwa ni tofauti na wasiokeketwa, jambo hilo litakwisha mara moja na kubaki historia”
20210511_151842.jpg
 
Kampuni ya Monarch Tractor ya Marekani imeunda Trekta ya kwanza duniani inayotumia umeme badala ya mafuta.. inaweza kulima, kukata mazao na kuvuna huku ikifanya kazi kwa saa 10 mfululizo baada ya kuchajiwa na haihitaji Dereva, inaweza kuendeshwa kwa rimoti.

Ni trekta ambayo wakati iko kazini shambani inaweza pia kukusanya taarifa mbalimbali ikiwemo za afya ya mazao, hitilafu kwenye umwagiliaji wa mazao na kubadilika kwa rangi ya mazao.

Monarch imetangaza kwamba itaanza kuuza Trekta hizo miezi miwili ijayo kwa Wakulima wa California, Washington na Oregon kwa bei ya $50,000 ambayo ni zaidi ya milioni 115 za Kitanzania.
20210511_153516.jpg
20210511_153532.jpg
 
Rais Samia Suluhu amefanya uteuzi wa Majaji wa Mahakama ya Rufani 7 na Majaji wa Mahakama Kuu 21 ambapo miongoni mwao wa Majaji wapya wa Mahakama kuu ni Biswalo Eutropius Mganga ambae kabla ya uteuzi huu alikuwa Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP)
20210511_163224.jpg
20210511_163243.jpg
20210511_163301.jpg
20210511_163320.jpg
 
Rais wa Sudani Kusini Salva Kiir atangaza bunge jipya.

Bunge la sasa linahusisha wabunge kutoka kundi la waasi wa zamani, Sudan People’s Liberation Movement linaloongozwa na Makamu wa Rais wa kwanza Riek Machar na kutoka vyama vingine vya kisiasa.

-
Kwa mujibu wa makubaliano ya amani ya mwezi Septemba mwaka 2018, vyama mbalimbali vilitakiwa kuchagua wawakilishi wao ili waweze kuteuliwa na rais.

-
Bunge la Kitaifa la Mpito (TNLA), ambalo lilipanuliwa Jumatatu kutoka wabunge 400 hadi 550, lina wabunge 332 kutoka chama cha SPLM cha Rais Kiir na viti 128 kutoka SPLM-IO cha Bw Machar.

-
Huku vya ma vingine kama cha South Sudan’s Opposition Alliance (SSOA) viti 50, vyama vingine viti 30 na wafungwa wa zamani viti 10.

-
Kwa mujibu wa makubaliano hayo, 35% ya viti vinapaswa kwenda kwa wanawake.
Bunge hilo lilivunjwa siku ya Jumamosi.

20210511_163559.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom