Makapuku Forum

Makapuku Forum

JE, WAJUA? CHARLIE CHAPLIN ALISHIKA NAFASI YA 3 KATIKA SHINDANO LA KUMPATA ANAYEFANANA NAYE

Mwaka 1975 liliandaliwa shindano la kumtafuta mtu anayefanana na Mchekeshaji maarufu Charlie Chaplin Katika hali ya kushangaza mchekeshaji huyo raia wa Uingereza alijitokeza kushiriki shindano hilo lililofanyika nchini Ufaransa kisirisiri

Alitegemea kuibuka mshindi na kuufurahisha umati wote uliohudhuria shindano hilo, Lakini matokeo ya shindano hilo yalipotolewa Charlie Chaplin alishika nafasi ya 3
20210503_173405.jpg
 
MUNGU ALIVYOSHITAKIWA MAHAKAMANI

Pichani ni Seneta wa Nebraska, Marekani Ernest Chambers aliyezaliwa mwaka 1937 -(82yrs). Mwaka 2008 alifungua kesi mahakamani kumshitaki Mungu

Alimshitaki Mungu kwa madai kuwa analeta madhara na majanga makubwa duniani kama vile matetemeko ya ardhi, mafuriko, vimbunga na majanga mengine makubwa.
Mahakama ikakubali kufungua kesi yake na endapo atamtafuta Mungu na kumfikisha mahakamani ndipo kesi itasikilizwa.

Baadae Mahakama ilitupilia mbali shitaka lake.
20210503_173525.jpg
 
BINADAMU ALIYEZALIWA AKIWA NA MIGUU MITATU (Three legged man)

FRANCESCO LENTIN alikuwa raia huko nchini Marekani, alizaliwa July 8 1884 katika mji wa Rosilin, Sicily, Italy.

Alizaliwa na miguu mitatu (3) yote ilikuwa inafanya kazi, alizaliwa na sehemu mbili(2) za siri za kiume nazo zote zilikuwa zinafanya kazi na miguu yake ilikuwa na jumla ya vidole 16 na nyayo 4.

Mnamo Septemba 22, 1966 akiwa na miaka 82 alifariki kwa ugonjwa wa mapafu huko Florida ambapo aliacha mke na watoto wa nne (4).

20210503_173701.jpg
 
MOJA KATI YA TUKIO LA AJABU DUNIANI LIKIAMBATANA NA UPENDO, AFUNGA NDOA NA MAITI

Moja kati ya matukio ya kushangaza sana hapa Duniani, ni tukio la kijana mmoja, aliyeomba kufunga ndoa na mchumba wake ambaye alifariki ghafla kutokana na ajali muda mfupi kabla ya kufunga ndoa yao!!

Kijana mmoja Chadil Deffy katika nchi ya Thailand amefunga ndoa na girlfriend wake ambaye amekufa ili kutimiza ahadi yake ya upendo. Kijana huyo mwenye umri wa miaka 29na mchumba wake mwenye umri wa miaka 28 anayeitwa Sarinya Kamsook tukio hili lilitokea mwaka 2019.

Sarinya Kamsook kwa bahati mbaya alifariki katika ajali ya gari, siku moja kabla ya tukio kubwa la harusi yao, Deffy aliamua kuendelea na harusi yao kama ilivyopangwa.

Sarinyaalihusika katika ajali mbaya ya gari, na kupata majeraha makubwa. Madaktali walijitahidi kumhudumia . Hata hivyo madaktari wakiwa katika jitihada za kuokoa maisha yake ili na kuchelewa kumhamishia hospitali nyingi badala ya ile aliyokuwa amelazwa kuna na msongamano mkubwa.

Na alifariki baada ya masaa sita. Ibada hiyo ya harusi iliunganishwa na ibada ya mazishi iliyofanyika katika kitongoji cha Surin, Thailand, kijana Chadil Deffy alimvisha pete mpenzi wake huyo ambaye ni marehemu.

Na tukio hilo likawa ni tukio la kipeke kutokea hapa duniani ambalo ni ibada ya harusi na mazishi kwa wakati mmoja.

"Deffy na Sarinya alikuwa pamoja kwa miaka 10,na hatimaye waliamua kukaa chini. Walikuwa wameahirisha harusi mara kadhaa, kutokana na kutokupata muda muafaka na ukweli kwamba Deffy alitaka kumaliza elimu yake kabla ya kufunga ndoa. Hata hivyo, baada ya kifo cha mpenzi wake Sarinya Deffy aliona hakuna kizuizi cha yeye kutimiza shauku yake ya kufunga harusi na mchumba wake huyo, hivyo aliamua kufunya harusi kabla ya kumzika.

Sherehe hiyo ya Kibuddhist ilifanyiaka katika mji wa Surin kaskazini mwa Thailand. Deffy alisema mbele ya jamaa na marafiki waliokuwepo katika sherehe kuwa ibada hiyo amefanya ili kuonyesha upendo wake mkubwa kwa mpenzi wake.
20210503_173833.jpg
20210503_173850.jpg
20210503_173904.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom