MOJA KATI YA TUKIO LA AJABU DUNIANI LIKIAMBATANA NA UPENDO, AFUNGA NDOA NA MAITI
Moja kati ya matukio ya kushangaza sana hapa Duniani, ni tukio la kijana mmoja, aliyeomba kufunga ndoa na mchumba wake ambaye alifariki ghafla kutokana na ajali muda mfupi kabla ya kufunga ndoa yao!!
Kijana mmoja Chadil Deffy katika nchi ya Thailand amefunga ndoa na girlfriend wake ambaye amekufa ili kutimiza ahadi yake ya upendo. Kijana huyo mwenye umri wa miaka 29na mchumba wake mwenye umri wa miaka 28 anayeitwa Sarinya Kamsook tukio hili lilitokea mwaka 2019.
Sarinya Kamsook kwa bahati mbaya alifariki katika ajali ya gari, siku moja kabla ya tukio kubwa la harusi yao, Deffy aliamua kuendelea na harusi yao kama ilivyopangwa.
Sarinyaalihusika katika ajali mbaya ya gari, na kupata majeraha makubwa. Madaktali walijitahidi kumhudumia . Hata hivyo madaktari wakiwa katika jitihada za kuokoa maisha yake ili na kuchelewa kumhamishia hospitali nyingi badala ya ile aliyokuwa amelazwa kuna na msongamano mkubwa.
Na alifariki baada ya masaa sita. Ibada hiyo ya harusi iliunganishwa na ibada ya mazishi iliyofanyika katika kitongoji cha Surin, Thailand, kijana Chadil Deffy alimvisha pete mpenzi wake huyo ambaye ni marehemu.
Na tukio hilo likawa ni tukio la kipeke kutokea hapa duniani ambalo ni ibada ya harusi na mazishi kwa wakati mmoja.
"Deffy na Sarinya alikuwa pamoja kwa miaka 10,na hatimaye waliamua kukaa chini. Walikuwa wameahirisha harusi mara kadhaa, kutokana na kutokupata muda muafaka na ukweli kwamba Deffy alitaka kumaliza elimu yake kabla ya kufunga ndoa. Hata hivyo, baada ya kifo cha mpenzi wake Sarinya Deffy aliona hakuna kizuizi cha yeye kutimiza shauku yake ya kufunga harusi na mchumba wake huyo, hivyo aliamua kufunya harusi kabla ya kumzika.
Sherehe hiyo ya Kibuddhist ilifanyiaka katika mji wa Surin kaskazini mwa Thailand. Deffy alisema mbele ya jamaa na marafiki waliokuwepo katika sherehe kuwa ibada hiyo amefanya ili kuonyesha upendo wake mkubwa kwa mpenzi wake.