Makapuku Forum

Makapuku Forum

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo May 3, 2021 amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Mstaafu wa Nigeria Olusegun Obasanjo.

Mazungumzo hayo yamefanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma ambapo Rais Mstaafu Obasanjo ametoa salamu zake za rambirambi kwa Rais Samia kufuatia vifo vya waliokuwa Marais wa Tanzania ambao ni Hayati Benjamin Mkapa na Hayati Dkt. Magufuli.

Obasanjo amempongeza pia Rais Samia kwa kupokea kijiti cha kuwa Rais wa Tanzania na amemtakia heri katika majukumu yake, katika mazungumzo yao wamezungumzia hali ya usalama Afrika na umuhimu wa Wakuu wa Nchi kujadiliana na kutafuta suluhisho la mipango migogoro ambayo inasababisha vifo vya Watu wasio na hatia hasa Wanawake na Watoto

Viongozi hao wamezungumzia masuala ya maendeleo hasa katika uchumi na kusisitiza umuhimu wa Nchi za Afrika kuongeza ushirikiano na kuondoa vikwazo vya biashara na uwekezaji.
20210503_165456.jpg
20210503_165514.jpg
 
Ni raia wa Uturuki na ndiye mtu mrefu zaidi duniani, ana urefu wa futi 8 na inchi 3 au mita 2.51.

Sultan mara ya kwanza alitajwa kuwa mtu mrefu zaidi duniani mwaka 2009 wakati alitimiza urefu wa futi 8 na inchi moja mwaka 2009 na kuingia kwenye rekodi za kitabu cha Guinness World Records
20210503_171159.jpg
 
WOMAN TREE (NAREEPO

Ni mti wa maajabu unaopatikana huko THAILAND kwa lugha ya THAILAND unaitwa NAREEPOL kwa maana⠀
NAREE - mwanamke ⠀
POL - mti⠀

Maajabu ya mti huu ni kuzaa matunda yenye umbile la mwanamke akiwa amefunika sehemu ya siri ya mbele kama inavyoonekana pichani apo juu.

Matunda ya mti huu hayafai kwa matumizi ya binadamu (hayaliwi)
20210503_171359.jpg
 
BILL HAAST maarufu kama SNAKE MAN raia wa Marekani

Alizaliwa mwaka 1910 wakati alipokuwa kijana alikua akijichoma sindano zenye sumu za nyoka tofauti tofauti ili tu aimarishe Kinga ya mwili wake. ⠀⠀
⠀⠀
Baada ya kuzoea kufanya hivyo alikua haogopi tena nyoka aling'atwa na nyoka zaidi ya 172 lakini hakupata madhara yoyote. ⠀⠀
⠀⠀
Alikua anajitolea Damu yake kwa watu walio ng'atwa na nyoka na wote walikua wanapona. ⠀⠀
⠀⠀
Aliishi miaka 101 alifariki mwaka 2011 ⠀⠀
⠀⠀⠀
20210503_171523.jpg
 
Pichani ni Jackie Bibby, Mtaalamu wa kucheza na nyoka (Rattlesnakes). Anashikilia rekodi 5 za Ulimwengu!
1.Kushikilia nyoka wengi kwa kinywa chake (rattlesnakes13)

2.Kuwekwa katika bafu (bathtub) na nyoka wengi kwa pamoja (195 rattlesnakes)

3.Amelala kwenye begi na nyoka wengi zaidi

4.Kufunga rattlesnake 10 kwa wakati wa haraka zaidi (sekunde 17.11)

5.Kutanguliza kuingiza kichwa kwenye begi lenye nyoka wengi zaidi (24 rattlesnakes)

NB: Rattlesnakes ni miongoni mwa nyoka hatari na wenye sumu Kali sana duniani lakini jamaa anacheza nao kama midoli.
20210503_172028.jpg
 
MTOTO WA MIAKA MIWILI (2) ALIYEZAA

Mtoto wa miaka miwili wa Huaxi nchini China, amefanyiwa upasuaji wa kujifungua baada ya madaktari kugundua kuwa alikuwa na mimba.

Xiao Feng, alipelekwa hospitali baada ya tumbo lake kuwa kubwa kiasi ambacho alijikuta akishindwa kupumua.

Alipolazwa, madaktari walichukua picha za x-rays na MRI ba kugundua kuwa Feng alikuwa amebeba mimba isiyokua na hivyo kuamua kumfanyia upasuaji.

Waliiondoa mimba hiyo changa iliyokuwa na upana wa cm 20 na tayari ilikuwa imeanza kuwa na vidole.

Mimba hiyo ilitakiwa kuwa pacha wa mtoto huyo (yaani mmoja alikulia tumboni mwa mwenzie). Pacha huyo wa sponji angekua na kuwa mtoto wa kiume.
20210503_172524.jpg
 
MWANAMKE MWENYE NGOZI YA CHUI


Mwaka1834 mwanamke wa ajabu zaidi alizaliwa aliyefahamika kwa jina la LOUISE alikuwa wa ajabu zaidi duniani kutokana na kuzaliwa huku ngozi yake ikiwa na madoa madoa kama alivyo chui.

Mwanamke huyu mwenye asili ya kutoka barani afrika alisafirishwa kwenda ulaya wakati wa biashara ya utumwa.

Ngozi yake iliyokuwa namadoa kama ya chui inaonekana ni tatizo la kijenetiksi kwani hata mmoja wa watoto wake alibahatika kurithi ngozi hiyo toka kwa mama yake.
20210503_172706.jpg
20210503_172721.jpg
 
BINADAMU MWENYE SURA MBILI

Edward Mordrake ni Mwingereza aliyezaliwa mwaka 1887 akiwa na sura mbili, moja ikiwa kwenye uso wake wa kawaida na nyingine nyuma ya uso (kwenye kisogo).

Inasemekana kuwa sura yake ya kisogoni haikuweza kula wala kuongea chochote na hata ikijaribu kuongea maneno yalikuwa hayasikiki lakini iliweza kulia, kucheka na kusikia kila neno.

Sura yake ya mbele ya uso imeelezwa kuwa ilikuwa ni nzuri na ya kuvutia (handsome face). Watu waliomuona na kuzungumza naye, wanamsifu Mordrake kwa uzuri wa sura yake ya usoni na tabasamu lake, lakini balaa lipo kwenye sura yake ya kisogoni ambayo ni ya kutisha na kuzeeka mithili ya kikongwe.

Wafanyakazi wa nyumba alimokua anaishi Mordrake walitoa simulizi kwa siri, ambapo walieleza hali ya maisha ya huzuni ya kijana huyo iliyosababishwa na miujiza na mabalaa yaliyoletwa na sura yake ya kisogoni.

Alijaribu kuwaomba madaktari wamfanyie upasuaji wa kuing’oa sura hiyo ya kishetani, lakini sababu za kitabibu zilizoonesha uwezekano wa yeye kupoteza uhai endapo atafanyiwa upasuaji huo, hivyo walikataa kufanya hivyo.

Mwaka 1910 akiwa na umri wa miaka 23, aliaamua kujiua kwa kunywa sumu baada ya kuchoshwa na mikasa hiyo ya sura mbaya aliyoiita kuwa ni ya kishetani.

Kutokana na hadhi ya ukoo wa Mordrake nchini Uingereza, historia ya maisha yake haikuweza kuwekwa wazi ili watu wengine wakajua maisha yake.
20210503_173115.jpg
20210503_173132.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom